TANESCO lini mmeanza kutumia magari yenye namba binafsi?

TANESCO lini mmeanza kutumia magari yenye namba binafsi?

JAYJAY

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2008
Posts
8,191
Reaction score
8,490
Ni mara ya pili sasa nakutana na gari ya Tanesco ikiwa na kile kibandiko cha mduara kama yai mlango wa dereva na ikiwa imebeba ngazi maeneo ya huku ninakojibanza ikiwa na namba ambazo sio "SU" bali zile za kawaida.

Mara ya kwanza mida ya saa mbili usiku niliiona gari moja eneo ambalo kulikuwa na Transfoma. Nilijua wanaweza wakawa wahalifu wa miundombinu nikajipa moyo kwa kuwa jirani pana kijiwe cha bodaboda. Mara ya pili nikakutana na nyingine ubavuni imeandikwa Tanesco Shinyanga mida hiyo hiyo ya usiku.

Je, imekuwaje hii? Shirika limebinafsishwa!? Au lina changamoto za fedha kiasi cha kukodisha magari ya watu/kampuni binafsi?
 
Wanakodisha gari binafsi siku hizi. Hii inaweza kuwa ni gharama nafuu kwao maana wamepunguza service ya gari, mshahara na marupurupu ya dereva etc etc
 
Wanakodisha gari binafsi siku hizi. Hii inaweza kuwa ni gharama nafuu kwao maana wamepunguza service ya gari, mshahara na marupurupu ya dereva etc etc
Hamna unafuu, ni ujinga na wizi tu, unakodisha gari kwa 100k per day, kwa mwezi 3m kwa mwaka 36m , kwa miaka mitatu ni 108m. Hiyo pesa wangepata double cabin nzuri kabisa mpya.

Hizi ndio akili za Makamba na Maharage, wizi wizi tu na uswahili.
 
Hamna unafuu, ni ujinga na wizi tu, unakodisha gari kwa 100k per day, kwa mwezi 3m kwa mwaka 36m , kwa miaka mitatu ni 108m. Hiyo pesa wangepata double cabin nzuri kabisa mpya.

Hizi ndio akili za Makamba na Maharage, wizi wizi tu na uswahili.
Gharama za service, kuajiri dereva kumlipa mshahara, paye, nssf, posho za
likizo, kununua matairi, insurance
 
Wanakodisha gari binafsi siku hizi. Hii inaweza kuwa ni gharama nafuu kwao maana wamepunguza service ya gari, mshahara na marupurupu ya dereva etc etc
Kwani
Anaye wako disha hana hizo gharama na faida juu
 
Wanakodisha gari binafsi siku hizi. Hii inaweza kuwa ni gharama nafuu kwao maana wamepunguza service ya gari, mshahara na marupurupu ya dereva etc etc
Kwani madereva wa hayo magari binafsi hawalipwi?
 
Kodi magari kuna faida kuliko Kuwa nayo Yard, Imagine wewe unalipa tu hela hakuna Siku utaambiwa gari bovu, sujui dereva anaumwa sijui kaenda anual leave yani hakuna excuse yoyote ile mzee
 
Hamna unafuu, ni ujinga na wizi tu, unakodisha gari kwa 100k per day, kwa mwezi 3m kwa mwaka 36m , kwa miaka mitatu ni 108m. Hiyo pesa wangepata double cabin nzuri kabisa mpya.

Hizi ndio akili za Makamba na Maharage, wizi wizi tu na uswahili.
miongozo inakataa kaka.procument ya serikal haiend kama unavowaz wewe tu umekaaa hapo unatype type hesab zako.
 
miongozo inakataa kaka.procument ya serikal haiend kama unavowaz wewe tu umekaaa hapo unatype type hesab zako.
Ameuliza kuwa kwani mwenye gari (wanayemkodi) hizo hesabu wanazozikimbia TANESCO za service, insurance nk anakuwa hana? Au magari wanayokodi ni mabovu??

Kama mwenye gari naye ananunua matairi, anafanya service nk na anakodisha gari na kupata faida, si ni wazi tanesco wanaingia hasara zaidi kwa kukodi magari kuliko ambavyo wangekuwa wanatumia magari yao!!
 
Hizo ni gharama za mwenye gari hazihusu shirika. Kampuni nyingi zina outsource huduma kupunguza gharama kwao na kuzihamisha kwa anayetoa huduma.
Kwa hiyo Mwenye gari hatengenezi faida, baada ya shirika kuzikwepa hizo gharama.
 
Wanakodisha gari binafsi siku hizi. Hii inaweza kuwa ni gharama nafuu kwao maana wamepunguza service ya gari, mshahara na marupurupu ya dereva etc etc
Aidha gharama nafuu ama upigaji. Kigogo mmoja hapo kaanzisha side business ya kuwakodisha magari kwa pesa za shirika hilo hilo halafu mwisho wa siku anawauzia.
 
Mbona yapo miaka yote. Kuna kazi maalumu kama ya REA na mengine. Umewahi kuona Serikali ikikodisha mabasi ya abiria kwa kazi fulani. Je Wanaosambaza umeme wa REA wanatumia magari yenye namba gani? , Fikiri kabla ya kuuliza
 
Back
Top Bottom