TANESCO lini mmeanza kutumia magari yenye namba binafsi?

Brother kunakitu unatakiwa uelewe. Sio kila anaedeal na miundombinu ya umeme ni Tanesco. kuna baadhi ni Wakandarasi wa REA
 
Sasa nchi rasmi imeingia utawala wa 'Kambale'. Baba sharubu, mama sharubu na mtoto sharubu. Namba binafsi inaweza kutumika kwenye kite go cha usalama tu kwenye shirika la umma. Na mara nyingi ni magari mdogo si malori.
 
Hizo ni gharama za mwenye gari hazihusu shirika. Kampuni nyingi zina outsource huduma kupunguza gharama kwao na kuzihamisha kwa anayetoa huduma.
Kwa hiyo Mwenye gari hatengenezi faida, baada ya shirika kuzikwepa hizo gharama.
 
Mbona yapo miaka yote. Kuna kazi maalumu kama ya REA na mengine. Umewahi kuona Serikali ikikodisha mabasi ya abiria kwa kazi fulani. Je Wanaosambaza umeme wa REA wanatumia magari yenye namba gani? , Fikiri kabla ya kuuliza
Juzi yamekodiwa ma bus kumi ya shabiby kuwatembeza wabunge kukagua miradi ya serikali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa uelewa wangu, nitakusaidia ufafanuzi kidogo, ila una haki ya kukubali ama kukataa, kwa sababu inategemea umeegemea wapi.
  1. TANESCO huwa wanakuwa na miradi ambayo inafadhiliwa na wafadhili, aidha msaada wa kiufundi (technical assistance) au wa kifedha na mali nyingine. Miradi hii huwa ya muda mfupi, na hao wafadhili huamua kutoa magari yao ili ktekelea kazi hizo. Magari haya sometimes yanabakishwa serikalini/TANESCO, lkn sometimes yanachukuliwa na mfadhili baada ya mradi kwisha! Mengine ndio hayo unayaona yana namba binafsi. Mengine yanakuwa na namba DFP lakini ni ya TANESCO, kutokana na masharti ya mfadhili kwamba ionekane gari ama mtambo umefadhiliwa na sio wa kodi za serikali. Hii DFP iko kwenye wizara almost zote.
  2. Serikali kupitia TANESCO na REA huwa wana mikataba na kampuni binafsi katika kufanya kazi za umeme (turn key) projects. Hawa hubandika nembo za REA/TANESCO kutegemea mkataba wameingia na nani, ili magari ama vifaa vingine vinapotumika kufanya kazi vitambulike kirahisi. Huenda hio gari uliyoiona na nembo ya TENESCO ikiwa na namba binafsi inafanya kazi hizo.
  3. Mwisho, serikali ia inatumia namba binafsi kwenye magari yake, kwa sababu maalum. Hii iko polisi, kwenye mashirika nk.
Nadhani utanielewa.
 
Sasa nchi rasmi imeingia utawala wa 'Kambale'. Baba sharubu, mama sharubu na mtoto sharubu. Namba binafsi inaweza kutumika kwenye kite go cha usalama tu kwenye shirika la umma. Na mara nyingi ni magari mdogo si malori.
Mkuu, serikali ina mambo mengi mno ambayo raia wa kawaida asiye mtumishi ni ngumu sana kuyaelewa. Acha Tutabaki kubwabwaja humu JF, lakini all in all serikali inaweza kutumia namba yoyote kwenye vyombo vya moto kwa makusudi fulani, au ikawa na chombo cha moto kisicho na namba ya usajili kabisa. Ibaki hivyo kwa sasa.
 

 
Mbona yapo miaka yote. Kuna kazi maalumu kama ya REA na mengine. Umewahi kuona Serikali ikikodisha mabasi ya abiria kwa kazi fulani. Je Wanaosambaza umeme wa REA wanatumia magari yenye namba gani? , Fikiri kabla ya kuuliza
Wewe unaeyajua hayo ndio uyaseme. REA na Tanesco ni taasisi moja?
 
Brother kunakitu unatakiwa uelewe. Sio kila anaedeal na miundombinu ya umeme ni Tanesco. kuna baadhi ni Wakandarasi wa REA
Wakandarasi wa REA ndio wana_respond to Emergency, tena hapa mjini kabisa! Hapa sizungumzii mikoani huko, hii ni hapa hapa "Dathlam" tena Kimara_Baruti.
 
Juzi yamekodiwa ma bus kumi ya shabiby kuwatembeza wabunge kukagua miradi ya serikali

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani wabunge wanafanya ziara kila siku.!? Ila shughuli za maintenace au emergency kwa Tanesco ni za kila siku, so wao kuwa na gari kwa ajili hiyo wala si ajabu. Labda uniambie mbona wabunge kila siku wanafanya ziara kukagua miradi na magari wanakodi.
 
waakodisha pick ups kwa ajili ya kazi. Kama una Pick up waone waikodishe
 
Je TANESCO ya kweli haya?! Ngoja tuisogeze @takukuru au @pccb wachunguze…
 
Gharama za service, kuajiri dereva kumlipa mshahara, paye, nssf, posho za
likizo, kununua matairi, insurance
Acha ujinga wewe unajua mnaingia mkataba wa malipo uwe unefanya au hujafanya kazi analipwa mtu
Sijui una akili zipi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…