TANESCO ndilo shirika linalochukiwa zaidi Tanzania kwa mwaka 2023, hadi wahubiri wawaomba waumini kuwasamehe

TANESCO ndilo shirika linalochukiwa zaidi Tanzania kwa mwaka 2023, hadi wahubiri wawaomba waumini kuwasamehe

Tatizo la umeme lilianza January Makamba aliitisha kongamano kubwa la matajiri na viongozi mbalimbali kwa fedha nyingi za serikali.

Tatizo la TANESCO lilipanuka pale ambapo wanasiasa akiwemo Naibu WAZIRI Mkuu Biteko alipoanza kufanya siasa na kuacha kusema kweli kuhusu undani wa tatizo

Tatizo lilizidi kukuwa pale Mwenyenzi Mungu alipoleta mvua ambayo ilifuta kauli za ulaghai za wanasiasa kwamba mgawo unatokana na ukame.

Changamoto ilizidi kupanuka pale watendaji wa TANESCO walipokosa wakuwakemea au kuwawajibisha.

Kwa ujumla wamewakwaza wengi hasa ikizingatiwa ni shirika linalolipwa fedha za maslahi makubwa nchini.

Viongozi wa dini wameliona tatizo laTANESCO na kutuomba tuwasamehe ili Mwenyenzi Mungu afungue njia tupate watu sahihi kwenye sekta hii. Tumelitangaza shirika linalochukiwa ila pia tuamue sasa kusamehe may be 2024 Mwenyenzi Mungu atamwonyesha Mh. Rais safu mpya itakayosaidia kuondoa hizi fedhea.
Tatizo linalofanya kuchukiwa ni mwenendo wake ambapo kuna mashaka mashaka. Leo hii unakatiwa umeme usiku kucha unarudi saa tatu asubuhi halafu saa nane wanakata tena mpaka usiku saa tatu mbaya zaidi ni public holiday. Hakuna taarifa yoyote na cha kushangaza sehemu nyingine wao wanao ukirudi kwenu wale nao wanakula off. Mwanzo walisema maji mara wakaja mitambo haikufanyiwa service unashindwa ukamate kipi. Je Mh Kalimani waziri aliyekuwepo enzi zake alifanyaje kukawa hakuna mgao wa hovyo? Juzi Mhe Raisi kasema kuwa ikifika Januari,2024 mtambo wa bwawa la mwalimu Nyerere utaanza majaribio kwa mtambo mmoja yaani ni kama Tanesco wameambiwa sasa kata kweli kweli umeme. Nilitegemea kuona unafuu kumbe ndiyo balaa.Sasa watu wanakula sikukuu giza na joto hili unategemea watapendwa na utadhani huduma yenyewe ni ya bure.
 
CCM na TANESCO ndio taasisi zinazochukiwa kuliko zot.
 
Tatizo la umeme lilianza January Makamba aliitisha kongamano kubwa la matajiri na viongozi mbalimbali kwa fedha nyingi za serikali.

Tatizo la TANESCO lilipanuka pale ambapo wanasiasa akiwemo Naibu WAZIRI Mkuu Biteko alipoanza kufanya siasa na kuacha kusema kweli kuhusu undani wa tatizo

Tatizo lilizidi kukuwa pale Mwenyenzi Mungu alipoleta mvua ambayo ilifuta kauli za ulaghai za wanasiasa kwamba mgawo unatokana na ukame.

Changamoto ilizidi kupanuka pale watendaji wa TANESCO walipokosa wakuwakemea au kuwawajibisha.

Kwa ujumla wamewakwaza wengi hasa ikizingatiwa ni shirika linalolipwa fedha za maslahi makubwa nchini.

Viongozi wa dini wameliona tatizo laTANESCO na kutuomba tuwasamehe ili Mwenyenzi Mungu afungue njia tupate watu sahihi kwenye sekta hii. Tumelitangaza shirika linalochukiwa ila pia tuamue sasa kusamehe may be 2024 Mwenyenzi Mungu atamwonyesha Mh. Rais safu mpya itakayosaidia kuondoa hizi fedhea.
TANESCO haina shida, shida ni Makamba na Chande ndiyo wamefilisi hili shirika
 
Back
Top Bottom