TANESCO: Sasa usambazaji wa umeme nchini kufanywa na sekta binafsi. Tayari Wawekezaji wameonesha nia ya kuwekeza TZS 3.3T kwa sharti la Ubia

TANESCO: Sasa usambazaji wa umeme nchini kufanywa na sekta binafsi. Tayari Wawekezaji wameonesha nia ya kuwekeza TZS 3.3T kwa sharti la Ubia

Upo kizamani sana.
Mmeshakula mlungula. Hamna sababu yeyote kwa sasa. Hebu niambie anakuja kufanya nini kwa sasa. Miundo.binu iliyopo ni kuibadili tu. Na inahitaji wakandarasi sio strategic ya ofisini. Hata siku moja serikali haiwezi fanya jambo ili ipate faida. Hiyo ni fallacy..
 
Nani alikudanganya?

Serikali inatakiwa iwe wasimamizi tu. Kazi zinafanywa na raia, kama hawawezi na wamewzidi wizi, uvivu, uzembe na ujinga. wanapewa Raia wa kigeni wanaoweza.
Sio kwenye kila kitu. Maji yako nyumbani huko Canada unalipa kwa city au kampuni?
 
Sio kwenye kila kitu. Maji yako nyumbani huko Canada unalipa kwa city au kampuni?
Usilinganishe Canada na Tanzania wu nchi nyingine yoyote duniani.

Canada serikali haiendeshi kitu chochote. Vyote vinaendeshwa na mashirika binafsi. Hata umeme unafuliwa na kusambazwana mashirika binafsi.

Bili zote huku unalipa bank. Bank zote ni binafsi.

Kwani uliambiwa hizo kampuni zitapokea bili zako za umeme huko Tanzania?

Kwanini mnapenda ku complicate mambo kwa kufikiri yasiyokuwepo?
 
Mkuu hebu nipe mradi mmoja tu ambao ulifanywa na Serikali ya Awamu ya nne ulio na manufaa kwa watz. Gesi imechukuliwa na wazungu kupitia mradi wa BOT (Build, Operate & Transfer) yaani wata-operate kwa miaka 50 then ndio wa-transfer kwenda serikalini kibaya zaidi hakuna watz walioandaliwa ku-takeover huo mradi hiyo inatokana na ubovu wa mikataba iliyoingiwa kati ya serikali na huyo mwekezaji.
Ukisikia ubia kwa tanzania ni kwamba sekta binafsi anakula uwekezaji wa umma wala hawekezi cha maana. Yeye anakula faida mbia serikali ndio anapata hasara na kubaki na madeni. usifikiri kina Adani hawa wahindi wanakua matajiri wakubwa duniani bure. Wanakuibieni kushirikiana na vigogo walafi.
 
Kuna zile bilioni nyingi tulilipa kwa kampuni ya huko huko India wakati ule Makamba ameingia tu wizara ya nishati kwa lengo la kuboresha upatikanaji wa umeme, bado biashara ile ipo?.
 
Ukisikia ubia kwa tanzania ni kwamba sekta binafsi anakula uwekezaji wa umma wala hawekezi cha maana. Yeye anakula faida mbia serikali ndio anapata hasara na kubaki na madeni. usifikiri kina Adani hawa wahindi wanakua matajiri wakubwa duniani bure. Wanakuibieni kushirikiana na vigogo walafi.
Ucha kupotosha ndg yangu
 
Usilinganishe Canada na Tanzania wu nchi nyingine yoyote duniani.

Canada serikali haiendeshi kitu chochote. Vyote vinaendeshwa na mashirika binafsi. Hata umeme unafuliwa na kusambazwana mashirika binafsi.

Bili zote huku unalipa bank. Bank zote ni binafsi.

Kwani uliambiwa hizo kampuni zitapokea bili zako za umeme huko Tanzania?

Kwanini mnapenda ku complicate mambo kwa kufikiri yasiyokuwepo?

Kuna tofauti ya uendeshaji na umiliki. Nakubaliana na uendeshaji binafsi lakini umiliki wa pipe za maji ya nyumbani, umeme wa manyumbani yaani ile path ni muhimu kumilikiwa na serikali au manispaa wengi hawafahamu hilo hata US na Canada ni hivyo
 
Kuna tofauti ya uendeshaji na umiliki. Nakubaliana na uendeshaji binafsi lakini umiliki wa pipe za maji ya nyumbani, umeme wa manyumbani yaani ile path ni muhimu kumilikiwa na serikali au manispaa wengi hawafahamu hilo hata US na Canada ni hivyo
Watanzania hawafahamu mambo mengi
 
Hii Nchi wasitufanye Wajinga.gharama ya umeme itapanda sana.

Tanesco auze kwa Msambazaji,ili apate faida atapandisha bei.
Atakaeumia ni Mlaji wa mwisho ambae ni mwana nchi.
 
Hii Nchi wasitufanye Wajinga.gharama ya umeme itapanda sana.

Tanesco auze kwa Msambazaji,ili apate faida atapandisha bei.
Atakaeumia ni Mlaji wa mwisho ambae ni mwana nchi.
Gharama ya umeme itaamuliwa na mamlaka za ndani
 
Back
Top Bottom