TANESCO yasaini mkataba wa kuzalisha Umeme Jua MW 150 Kwa Bilioni 275. Waziri Makamba apiga marufuku mauziano ya Umeme kwa Dola

Safi, hii ni good move.

Je huo umeme utakuwa bei nafuu?, Au ndo yaleyale ya Maharage Chande kutaka umeme uendekee kuwa ghali?
 
January hapa umepatia!
Ila sasa ifikie hatua sera iruhusu wenye uwezo wa kuzalisha umeme wa ziada wauze Tanesco kwa makatano kwenye units.
Hii itatengeneza energy mix nzuri badala ya kutegemea juhudi za serikali peke yake!
 
Hizo siasa bwana mdogo umeme wa Maji bado unatumika na ni tegemeo kwa nchi nyingi Duniani .
Umeme wa maji unatumika ndiyo lakini tunakoelekea na haya mabadiliko ya tabianchi tegemea msuguano mkubwa kwenye mahitaji na matumizi ya maji!
Hivi si unakumbuka harakati za kupambana na waliochepusha maji kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji??
Sasa hizo harakati zitaongezeka as we go!
 
But gharama ya kuzalisha Mwh 1 ni $20-40 hiyo pesa ni kama kubwa kidogo .ukichukulia solar ndio umeme wa bei rahisi duniani .

 
China wamemaliza kujenga largest hydropower source duniani ,Tanzania uwe umeme wa kizamani kwa sasa ?
 
Baada ya hiyo gharama je kuna malipo ya kila siku wikinau mwezi? Na kwa muda gani ukomo wake? Au unakuwa wa kwetu jumla?


Najaribu kuwaza mitambo tunalipia sisi na huduma tuje lipia sisi tena?

B215 ni nyingi sana


Kwa bilion 20 wangeweza kufanya instalatiin ya kila nyumba hapo umeme wa solar tena ile super kabisa
 
Tunamtengenezea afu anatuzia umeme

Hahahahah noma sana

Kwa hizo gharama ilipaswa mitambo iwe mali yetu chini ya shirika la umeme la nchi
 
bwawa la nyerere halijaisha tumehamia kwenye umeme wa jua.hzo hela si mngepeleka bwawa la nyerere.mbona mnachezea hela.miradi hamumalizi mnarukia mingine
 
Atutajie mikoa hiyo mikoa mitatu
 
Bilioni 275 nimpesa kidogo kwa tanesco kwa nini isiwe watafute mkandalasi wa kufunga mitambo ikawa mali yatu badala ya kuuziwa umeme
 
Energy mix, huwezi tegemea Maji tu ikitokea hitilafu nchi itaingia gizani tuanze kulalamika hujuma!!

Ila kuhusu wao kununua ni hoja nzito, ilipaswa huu uwe mradi wao sio Tena wanunue then watuuzie wateja wa mwisho.
Na nani kabisha kuhusu energy mix ? Tanzania tunategemea maji pekee ? Hakuna Solar at household level ? Hakuna Gesi ? tunatumia mpaka mafuta na generator kwa gharama kubwa sana inayopelekea wananchi na nchi kufanya uzalishaji kuwa wa gharama; anyway haya mambo ya energy mix na the only way ya kufanya solar feasible nilishayaongelea hapa....

 
Huku ndio kuhesabu vifaranga wakati hata kuku hauna let alone mayai....; haya mambo ya kutosha tutaendelea kuongezea cha maana ni kumaliza mradi mmoja baada ya mwingine sio kushika shika hapa na pale in the end hakuna kinachofanyika.....; Miradi Lukuki utafikiri kuna mashindano ya kuanzisha miradi badala ya kumaliza tunayoanza hatua kwa hatua
 
Hivi ni Kwa nini nguvu moja isielekezwe sehemu moja ili ikikamilika ianze sehemu nyingine? Hata uangalizi unakuwa makini kwa hao contractors. Bwawa la Nyerere na Umeme wake wa maji na size ya source ya Umeme tuliambiwa shida ya Umeme itakuwa ni history likikamilika percent % sasa hizi source nyingine mpya za nini wakati ili bado? Anyway labda uelewa wangu ni mdogo.
 
Kwani ule mradi wa upepo umeishia wapi??
 
Ivi huu umeme usiku inakuwaje?
Ndio maana unahitaji storage (battery) kitu ambacho mpaka sasa ndio bottleneck ya solar; tatizo la umeme ni efficient kama unazalisha na kutumia kwa wakati huo huo; generator unaweza kuzima mitambo Hydro unaweza ukapump maji juu kuyarudisha (ikiwa off-peak ili utumie peak time)....; solar you need a good storage au itumike kama mix ya nishati nyingine au uitumie directly unapozalisha
 
bwawa la nyerere halijaisha tumehamia kwenye umeme wa jua.hzo hela si mngepeleka bwawa la nyerere.mbona mnachezea hela.miradi hamumalizi mnarukia mingine
Kwani kabla ya bwawa kulikuwa hakuna miradi mingine ya uzalishaji umeme?
 
Hakuna Cha storage acha kukurupuka,utaingia kwenye matumizi Moja kwa Moja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…