TANESCO yatangaza mgawo wa umeme

TANESCO yatangaza mgawo wa umeme

Hivi mnauelewa utaratibu wa manunuzi ya umma? Ni wapi katika kanuni hizo zinasema wanafunzi au wakazi wa kiTanzania walioko nje wanaweza kutumiwa kunua vifaa vya Serikali/Shirika kinyume na taratibu hizo?

Kama kweli mnuwezo huo leteni tenda!!
 
Mkuu Zitto,
Ur not serious!.. are You?
Mkuu tulikwambia toka siku zile kwamba mitambo ipo na sii GE peke yake mipya na kukukuu maadam wapeni kazi vijana wataifanya..Mimi binafsi nilikwambia pia kabla na baada ya mgogoro wa Dowans...nimeandika humu humu JF iweje leo somo tunarudia kule tulikotoka?..

Acha mbali kwamba Lowassa alipotembelea hapa (hatukuonana naye alikwenda Mexico badala ya kukutana na Watanzania)niliwajulisha baadhi ya viongozi walioandamana na msafara wake, lakini Richmond ilikuwa ndio somo na hakuna upinzani.
Sasa nenda kawaone hao Tanesco wambie vijana wapo tayari kisha rudisha kazi hiyo hapa JF utaona uwezo wa vijana mnapowapa kazi ya taifa...
Binafsi siwezi kwenda ovyo kutafuta mitambo kisha majibu yenu yawe yale yale tunaonekana wajinga na matapeli.. ongea na Tanesco watupe go ahead, contact zao hata iwe kupitia kwako tutaifanya kazi tena haraka kuliko mtakavyo fikiria.

Kisha gharama ya ujenzi haiwezi kuwa kubwa kwa sababu ile mitambo ya Richmond/Dowans tayari ilikwisha jengewa na kufanya kazi hivyo chochote mtakachonunua kitawekwa pale ilipokuwa mitambo ya Dowans au sio!.

Hivi kweli utaratibu wa manunuzi ya umma mnauelewa? Ni wapi katika taratibu hizo unawaruhusu Serikali/Tanesco kuwatumia wanafunzi au waTanzania waliopo nje kufanya manunuzi kinyume na taratibu? Utaratibu huo ulioelezwa hapo juu si tu utazua soo jingine?

Kama kweli mnauwezo huo kwanini hamleti tenda?
 
Dawa ni kuwa na mshindani mwingine wa kufua umeme ili tanesco na li-bichwa lake la kiburi likome
 
jamani hivi ile mitambo ya richond imebinafsishwa? Vinginevyo wanatafuta kisingizio cha kuinusuru richmond na lowasa......tulijua maana idrisa rashid alikuwa mbogo kuambiwa kuwa hii mitambo hainunuliwi ila inabidi itaifishwe......AJBU SIJAWAHI KUMSIKIA LOWASA AKIPENDEKEZA MITAMBO IBINAFSISHWE KAMA SIO YAKE NA ROSTAM...........................Hii ndio tanzania ya wadanganyika na tunadanganyika kiukweli....
 
tumewaajili ili waproject kila kitakacho tokea na wapendekeze hatua za kuchukua kudhibiti matatizo yasitokee na hata yakitokea basi isiwe kwa kiasi cha kutisha.....lakini muda unaenda mwisho tunaambiwa yaleyale tuliyo zoea kuyasikia kuwa maji yamepungua hivyo kutakuwa na mgao wa umeme..........haya yanachosha sana watz...TUWAFANYE NINI HAWA WATEULE WA RAIS?
 
Kikwete aliahidi alipofanya mkutano na watanzania London kwamba mgao wa umeme utakuwa na umeasha kuwa historia... sasa aulizwe ni historia gani hiyo alikuwa anazungumzia...
Namwomba anipe ukurugenzi wa Tanesco nimoneshe kazi inavyofanywa... umeme utakuwa 24/7 kila siku ya mwaka na hakuna kukatika hata kidogo...

Pia wanatoa sababu ya
kuharibika kwa mtambo wa Songas UGT1 (20 MW), kuharibika kwa mtambo wa Kihansi (60 MW) na kuharibika kwa mtambo wa Hale (8 MW).

Hivi hawa mafundi au ma-engeners ni ushwara ua ni kazi yao hawaijui? inachukua muda gani kutengeza mitambo... kama ni vipuri inachukua muda gani kuviagiza....Ndege za DHL and Fedex zinafanya kazi kila siku 24/7 sasa kwa nini wasinunue vipuru hivyo hata kutoa venezuela na kuvileta... Itachukua si chini ya masaa 24 vifaa hivyo kufika Tz..

Ni uzembe wa hali ya juu ambapo ingefaa wahusika wafikishwe mahakamani kwa kuzembea katika uwajibikaji wao wa kazi kama akina Mramba na Yona..
 
Hivi mnauelewa utaratibu wa manunuzi ya umma? Ni wapi katika kanuni hizo zinasema wanafunzi au wakazi wa kiTanzania walioko nje wanaweza kutumiwa kunua vifaa vya Serikali/Shirika kinyume na taratibu hizo?

Kama kweli mnuwezo huo leteni tenda!!
Tk,
Nadhani wewe ni mmoja wa watu waloshindwa jua maana. na hunipa shida sana kujieleza zaidi kwa sababu ni wewe unatakiwa kusoma na kuchambua yaliyomo baina ya kila mstari.
Uwezo wa kujua wapi mali inapatikana ndio tunasema sisi tunao, na sii uwezo wa kushiriki ktk tender za serikali ambazo zinahitaji mabillioni ya fedha. Kisha in reality najua siwezi kupata kutokana na ukiritimba..kifupi haiwezekani..
Hivyo mnapowataka vijana wawe preactive wakati mkijua hatu qualify ktk utaratibu wenu wa manunuzi, kisha mnakuja na kuuliza kwa nini hatushirki mnataka sisi tujibu vipi?..

Hizo taratibu kaziweka nani, sisi au ni serikali ktk kujenga bureaucracy na mwanya wa corruption. Tazama mfano mdogo wa Tazara wao wanaenda moja kwa moja GE wakati Tanesco wanapitia wizarani..now who finance Tazara kama sio serikali za nchi mbili iweje kule iwe rahisi lakini tunashindwa Tanesco na hata TRC..
Mkuu nitakwambia kitu kimoja huyo msomi mliye msomesha hadi chuo kikuu ni mtaji mkubwa ktk maendeleo ya Tanzania kuliko mwekezaji wa billioni moja..mkishindwa kuwatumia makosa sii yangu mimi ila yenu kwa tamaa ya fedha na ulimbukeni ndio maana mnaweza sheria na taratibu sizizokuwa na kichwa kabisa..We can help, lakini taratibu za serikali zinataka ati Mtanzania aje na dollar laki moja kuwekeza nchini ndio apewe kibali cha excemption lakini akija na degree yake hana thamani, yet rais huyo huyo anawataka Watanzania warudi nyumbani kuwekeza, kuwekeza katika kitu gani?.....Unafikiri huyu rais anafikiria kitu gani zaidi ya kuwekeza ni miradi ya fedha tu.. Wasomi vijana wake waliofuta madarsa wakahifadhi misahafu ya elimu dunia hawa qualify!..why?...hivi elimu za hawa vijana mnaona hazina impact kabisa ktk utaratibu wa maendeleo yenu...mnaichukulia elimu kama sii investment wala haipo ktk Rights za wananchi isipokuwa ni privilege fulani hivi...

Nitakupa mfano mwingine nimeona TRC wameweka tender ya kuwa supplied vyuma vya reli...Mimi najua wapi wanaweza kuvipata na hata shirika gani lionaweza kutandika reli na ukarabati wake kwani ndio kazi yao kubwa hata huku Nje.Wanaaminika na wanafanya kazi ya Uhakika.Lakini nitaweza vipi kuishauri serikali ambayo haina hata idea ya mashirika yanayotengeneza au ku supply vyuma hivyo acha mbali utendaji kazi wake... nitaanzia wapi?
Leo wanatoa tender ati washiriki wanashindana kuandika Bidding Documents kwa kiingereza wakati najua fika huyo Waziri na wakurugenzi wake watatoka watupu kama sii kuwategemea wataalam wa TRC.. Then kwa nini TRC wenyewe wasitafute mali hiyo na kuwakilisha mapendekezo yao wizarani.
Mkuu wangu tender inapendeza tu ikiwa unatafuta ku contract kazi nzima kwa shirika mwekezaji na sii kwa mali uhayotaka kununua kwa mahitaji yako..besides hata siku moja serikali zetu haijawahi kununua wala kufuata tender hahisi na Imara isipokuwa ghali na yenye ulaji iwe magari, rada, ndege U name it kila siku tunanunua vitu ghali kuliko thamani halisi ya vitu hivyo... Yoote ni NJAA tu mkuu wangu hatuna sababu, hizi siasa nyingi za utaratibu na kadhalika ni kujipa moyo wa U saint!
 
Last edited:
idrisa rashidi anasema kama unalalamika usimlalamiokie yeye isipokuwa mlalamikie aliye mteua...
 
More dark days ahead?....

Firstly we all must accept that there was a pre-warning by the one and only Tanseco regarding the looming darkness by september.
Secondly, our belove Govt., recently announced that Songas will/would generate more power into the grid..what happened thereafter?if so,than how come their present system has broken down?

Lastly, why does the Gvt., wait for the last and dying minutes before taking the necessary actions?

With this heat and recession spells,what more are we being cursed with?
 
Haya ni matokeo ya kulea uzembe katika uongozi. Ikiwa bosi wa GM ametolewa nje, sisi tunashindwa nini? Tunaogopa nini?

Amandla.......
 
Hivi kweli utaratibu wa manunuzi ya umma mnauelewa? Ni wapi katika taratibu hizo unawaruhusu Serikali/Tanesco kuwatumia wanafunzi au waTanzania waliopo nje kufanya manunuzi kinyume na taratibu? Utaratibu huo ulioelezwa hapo juu si tu utazua soo jingine?

Kama kweli mnauwezo huo kwanini hamleti tenda?

...halafu ndio mnajiita watetezi wa maslahi ya umma..........!
ulikuwa wapi wakati wa Zabuni ya Richmond......ndugu yangu........
 
du nchi zinazoendelea sijui zitakuwa developed lini?
 
Hivi ndugu zangu nikisema nchi hii kiuongozi ni mufilsi nitakuwa nimekosea? nasema hivi kwasababu tatizo la mgao wa umeme alikuanza leo au jana. Tangu awamu ya pili mpaka leo mambo ni yaleyale kila mwezi Oktoba unapofika. Mvua zikigoma kunyesha basi mambo yanakuwa ndivyo sivyo. Impact ya gesi ya Songosongo pamoja na IPTL haionekani. Sasa tufanyeje? Kwa ushauri wangu naona tuzungumze na Iran au Korea ya Kaskazini watusaidie kujenga kinu cha nuklia maana tuna Uranium kibao. Tahadhari: Siku hao wataalam wetu wa nuklia watakapobofia basi watu wote karibu na hicho kinu watakuwa kwishnei.
 
Hii serikali inamatambo sana kwa sababu ya ukimya na nidhamu ya kijinga tuliyonayo leo hii katika miaka 48 nchi nzima iwe inaachwa rehani kwenye giza halafu Idrisa anatoka huku akijitutumua anasema eti tumuulize aliyemteua manake anamdharau kwamba kumuweka pale kama pakacha atajivunia nini akitoka hapo kwamba alikifanya kizuri kuwakwamua wananchi kwenye shida kuu ya umeme
Mi si elewi ni kwa vipi watang,olewa hawa wamekula inatosha hakuna kitu uji uji tuu kwenye vichwa vyao
raisi waziri mwenyeki wa bodi katibu mkuu wa wizara za nishati na idrisa mwenye zaidi ya mara moja wameshatuahidi hakuatkuwa na mgao nchii hii
hawana lolote wochovu wasiofaa kabisa kuongoza nchi waende wakavimbiwe huko wanakozurura
 
...halafu ndio mnajiita watetezi wa maslahi ya umma..........!
ulikuwa wapi wakati wa Zabuni ya Richmond......ndugu yangu........

Una maana na wewe unataka kuanzisha Richmond yako au??
 
Una maana na wewe unataka kuanzisha Richmond yako au??

.......ndugu yangu.....hili suala la manunuzi ya umma tumetoka nalo mbali........hatujalianza just recently..............check mjadala wa Richmond.........na hatimaye Dowans..........halafu niambie kuhusu public procurement in relation to "manufaa ya umma"..............
 
Hii ni ishara nyingine kwamba hatuna uongozi makini katika level zote. iwapo Rashidi alijua kwamba kutakuwa na tatizo litakalosababisha mgawo wa umeme, alichukua hatua gani? Au alitaka tutambue kwamba tulifanya makosa kukataa kununua mitambo ya fisadi mwenzake, Rostam? Kuna wizara kamili inayoshughulikia nishati. Hivi wamefanya nini kuhakikisha nchi haingii kwenye matatizo ya umeme? Kwenye long term plans kuna kitu kweli kinafanyika? Kwa kweli haiingii akilini...
 
technical issues and political engineer are two differrents entity.
 
Nchi hii kila mmoja anataka kila akisemacho kifanyiwe kazi isipofanyiwa kazi basi adhabu inatupwa kwa wananchi walipa kodi! Kwanini Tanesco wameshindwa kujiwekea mikakati ya kuhakikisha kwamba umeme unapatikana bila tatizo? Umeme wenyewe unawafikia watu sio zaidi ya milioni 10 tu alafu wanashindwa sasa nchi mzima itapata umeme mwaka gani! Huu ni uzembe wa hali ya juu na hatuwezi kukubali! tanesco wafanye kazi sio siasa!

ndio maana naaamini hii nchi bila mapinduzi haitafika popote
 
Zitto,
Umejiingiza sana kwenye masuala ya TANESCO kuliko shirika jingine lolote la UMMA. Hii ni hatari kwako kwani wewe unaongea na MENEJIMENTI tu, undani hasa wa shirika lile hauujui. Iachie Bodi ya TANESCO ifanye kazi yake. Ufisadi uliomo ndani ya TANESCO hakuna siku litakaa litengeneze faida!

Kaka i would do the same with TPDC and STAMICO. These Parastatals have to be guided like nothing. They are potential champions of our economy - TANESCO; TPDC and STAMICO!
 
Back
Top Bottom