jkipaji
JF-Expert Member
- Sep 22, 2019
- 6,963
- 9,401
Aje huko wapi!?Kama una ushahidi na hayo nakushauri uende nao kwenye ofisi iliyo juu yake yaani mkoani...bila kuacha kumpa taarifa OCD wa wilaya ya Kilindi.....ikishindikana huko ndio uje huku
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Aje huko wapi!?Kama una ushahidi na hayo nakushauri uende nao kwenye ofisi iliyo juu yake yaani mkoani...bila kuacha kumpa taarifa OCD wa wilaya ya Kilindi.....ikishindikana huko ndio uje huku
Ni nafuu angekuwa tu mpigaji lakini amevuka mipaka kwa kulewa madaraka amekuwa mnyanyasaji sana , vitendo anavyofanya kwa wakulima wa huku ni vya kiuonevu , huyu bwana tunajipanga kufanya maandamano kwenda ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Tanga na mabangoKilacmtu akipata upenyo ni kutandika tu
Ova
JF kuomba ushauri mwingine kama atakwama hukoAje huko wapi!?
Sio fitna huyu jamaa kila mtu anamlalamikia huku , uliza mtu yeyote wa wilaya ya Kilindi atakwambia habari zake ni mtu wa hovyo sanaWatu wa Maramba kwa kufitiniana?!
Aje huko wapi ?
Sahihi kabisa maana JF ni jukwaa muhimu la watu kupaza sauti zaoJF kuomba ushauri mwingine kama atakwama huko
Ni sahihi kabisa nakubaliana na unalolisema Sisi huku kilindi tunateseka Sana na huyu bwana ambaye kwa sifa zake hata ujumbe WA nyumba kumi hawezi kuongozaHii nchi laana tuliyopewa ni hio ya kuteua wakuu wa mikoa na wilaya wakati ilitakiwa waombe kazi kama taaluma nyengine wanavofanya/ wapigiwe kura,
Usingesikia huo upuuzi. Wanavimba.
Katiba mpya muhimu.
Halafu mshikaji design tejaBado Yupo Ofisini
Mkuu niko nje ya mada kidogo naomba nisaidie maelekezo kuhusu io wilaya hivi maisha ya huko yakoje hasa hasa kwenye suala la upatikanaji wa maji majumbani pamoja na umeme na uwepo wa Hospitali karibu je.? ivyo ni vitu vya uhakika au ni changamotoRais wangu nakusalim kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni mimi raia wako Rashidi Jumaa kutokea Tanga wilaya ya Kilindi ni mzawa wa huku
Sauti ya mnyonge huwa haisikiki kwa urahisi, nimeona nilitoe dukuduku langu humu kwenye mitandao ya kijamii kutokana na kero tuliyokuwa nayo na huyu mkuu wetu wa wilaya ya Kilindi mkoa wa Tanga, Hashim Mgandilwa Nina imani kubwa serikali yako ni sikivu itanipa sikio la kunisikiliza.
Mkuu wa wilaya ya Kilindi ni kichefuchefu
Amekuwa akiwakandamiza sana wakulima na kuonesha upendeleo wa wazi kwa wafugaji bila kusikiliza pande zote
Mfano katika kata ya Mafisa kuna kesi ya mkulima kupigwa risasi na mfugaji na kesi ilifika mezani kwake lakini hakuna maamuzi yeyote aliyoyatoa na kwa taarifa nilizokuwa nazo ana uswahiba na yule aliyefanya tukio hilo la kinyama wana mradi wao wa ufuagaji
Mashamba ya wakulima yanaharibiwa na wakulima wanatengenezewa makosa ya uongo wanawekwa ndani
Sio msikivu kabisa kwa raia wake ametawaliwa na ujeuri / kiburi cha madaraka anafanya ofisi kama ni mali yake hafwatishi kanuni na muongozo wa kazi ,
Ukimfuata ofisini huwa ana majibu ya ovyo sana ya kuonesha dharau kwa sisi wananchi wa hali ya chini
Huyu mkuu wa wilaya naona bado ni mwanafunzi hana uwezo wa kuongoza, hatufai wilaya ya Kilindi Tanga na wala hafai popote pale, maana hata akiamishwa ni sawa na kupeleka matatizo sehemu nyengine.
Ninayozungumza sio majungu ni hali halisi tunayokutana nayo huku. Nakuomba Rais tuma wapelelezi wako wafuatilie utendaji wake watayasikia mambo mengi sana juu yake.