Tanga: Wanafunzi 12 wakamatwa wakivuta Bangi vichakani

Tanga: Wanafunzi 12 wakamatwa wakivuta Bangi vichakani

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Wanafunzi 12 wa shule ya Sekondari Handeni iliyopo wilayani Handeni mkoani Tanga wamekamatwa vichakani wakivuta bangi na kucheza kamari muda wa masomo hali iliyopelekea uongozi wa shule hiyo kuwasimamisha masomo kwa muda wa siku 14.

Wanafunzi hao wamekamatwa kufuatia oparesheni maalumu ya kuwasaka wanafunzi watoro katika shule za sekondari Halmashauri ya Mji Handeni ikisimamiwa na Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Mussa Mkombati.

Mkombati amesema wanaendelea kuthibiti utoro katika halmashauri hiyo kwa lengo la kuona watoto wanaripoti shule na kupata elimu.

Baadhi ya wazazi wamepongeza hatua zilizochukuliwa viongozi pamoja na walimu katika kuthibiti utoro huo na kuomba ushirikiano zaidi kutoka kwa walimu.

Jumla ya wanafunzi 214 waliotakiwa kujiunga kidato cha kwanza 2023 bado hawajaripo shuleni mpaka sasa.

MWANANCHI
 
Wanafunzi 12 wa shule ya Sekondari Handeni iliyopo wilayani Handeni mkoani Tanga wamekamatwa vichakani wakivuta bangi na kucheza kamari muda wa masomo hali iliyopelekea uongozi wa shule hiyo kuwasimamisha masomo kwa muda wa siku 14.

Wanafunzi hao wamekamatwa kufuatia oparesheni maalumu ya kuwasaka wanafunzi watoro katika shule za sekondari Halmashauri ya Mji Handeni ikisimamiwa na Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Mussa Mkombati.

Mkombati amesema wanaendelea kuthibiti utoro katika halmashauri hiyo kwa lengo la kuona watoto wanaripoti shule na kupata elimu.

Baadhi ya wazazi wamepongeza hatua zilizochukuliwa viongozi pamoja na walimu katika kuthibiti utoro huo na kuomba ushirikiano zaidi kutoka kwa walimu.

Jumla ya wanafunzi 214 waliotakiwa kujiunga kidato cha kwanza 2023 bado hawajaripo shuleni mpaka sasa.

MWANANCHI
Walimu wakikaza Mnasema Wakatili Sana nawatakia kila la Kheri Walimu wote kwa kazi nzuri kutengeneza nidhamu ya jamii.Walimu Oyeeeeee
 
Mh hawa wanafunzi tatizo linaanzia nyumbani. Kuna siku nipo nyumbani jioni ya giza kabisa nilikuwa na mshikaji wangu wa kitambo tunakula mjani.

Basi nje ya fensi wakapita kikundi cha wanafunzi hawapungui sita na walipokaribia fensi yangu umeme ukakatika wakapiga kelele na kubweka kama mbwa ili mbwa wangu aanze naye kubweka kwakua tulikuwa nje pale hawakubweka basi madogo wakarusha mawe juu ya bati...... Dah kile kitendo kilinitia hasira alafu wao wakaanza kukimbia.

Nikachukua kirungu changu niliibaga kwa masai mlinzi muda sana basi nikatoka getini nikaanza kuelekea walipokimbia mshkaji wangu naye alitoka na kamkia ka taa sio kakubwa ila mkononi kanashikika vizuri.

Tumekimbia kidogo umeme ukarudi nikawaona wako sehemu ina watu wengiii nikasema pale pale wakipita tu wale watu nakuwa nimeshawafikia, nikaongeza speed na wao walishabweteka wakijua hakuna anaekuja.

Nilipofika karibu nikachomeka rungu kuinoni nikakamata mashati ya wawili nukaenda nao hadi chini nikawatuliza na goti mmoja nimemkunja shati mpka vifungo vinakatika.

Mshkaji wangu naye akafika tukaanza kirudi nao watu wanashangaa imekuje usiku na wanafunzi mnawapiga hakuna anaewapa jibu mpka tumefika nyumbani alafu umeme ukakatika tena hapo ndipo walipoumia maana zilitembea rungu na mikia ya taa mpka umeme unarudi tena madogo hawafai wakaanza kuomba msamaha wakilia sana mimi machale yakanicheza niwakague ebhana eehhh dogo mmoja ana puli la bhange kisu kali na paper za kutosha dah pale pale nikataifisha begi alafu kichapo kikaendelea mixer kuwaambia wawalete na wenzao waliopiga mawe. Ila ninachotaka kusema ni malezi toka nyumbani yamedorora hivyo lazima watoto wazingue tu.
 
Hawatayaona peke yao mkuu; wewe na mimi pia tutayaona kwa sababu ndiyo panda Road wenyewe hao wajao.
Ni kweli mkuu malezi mabovu ni chanzo cha haya yote, waswahili walisema samaki mkunje angali mbichi. Ni rahisi kumrekebisha kimalezi mtoto wa darasa la 3 ila wa form 3 tayari inakua too late japo inawezekana.
 
Wanafunzi 12 wa shule ya Sekondari Handeni iliyopo wilayani Handeni mkoani Tanga wamekamatwa vichakani wakivuta bangi na kucheza kamari muda wa masomo hali iliyopelekea uongozi wa shule hiyo kuwasimamisha masomo kwa muda wa siku 14.

Wanafunzi hao wamekamatwa kufuatia oparesheni maalumu ya kuwasaka wanafunzi watoro katika shule za sekondari Halmashauri ya Mji Handeni ikisimamiwa na Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Mussa Mkombati.

Mkombati amesema wanaendelea kuthibiti utoro katika halmashauri hiyo kwa lengo la kuona watoto wanaripoti shule na kupata elimu.

Baadhi ya wazazi wamepongeza hatua zilizochukuliwa viongozi pamoja na walimu katika kuthibiti utoro huo na kuomba ushirikiano zaidi kutoka kwa walimu.

Jumla ya wanafunzi 214 waliotakiwa kujiunga kidato cha kwanza 2023 bado hawajaripo shuleni mpaka sasa.

MWANANCHI
Bring back viboko
 
Back
Top Bottom