Tanganyika iiombe radhi Zanzibar?

Tanganyika iiombe radhi Zanzibar?

Siku Zanzibar ikijitenga kutoka kwenye muungano GDP yake itapanda na kuweza kufanana na WA nchi kama Luxemburg au Liechtenstein.
 
Zanzibar iiombe radhi tanganyika kwa lipi kwani marehemu anaombeka radhi?
Tanganyika si marehemu, tafadhali! Marehemu anaweza kumtawala aliye hai? Si inasemekana Tanganyika inaitawala Zanzibar kimabavu?
 
Mioyo ya Wazanzibar ilishaukataa Muungano siku nyingi. Tuko nao kimwili lakini si kifikra.

Ughaibuni huwa wanajitambulishaje? Mtanzania? Dhubutu!!!

Wanaojiita Watanzania ni Watanganyika. Mzanzibar akiwa ng'ambo hajiiti Mtanzania, bali Mzanzibar!!!
Thubutuuuuuu kuomba radhi kwa lipi.
 
Tulichofundishwa shuleni kuhusu Muungano, ni tofauti na ninayoyasikia Sasa!

Inasemekana, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar haikuwa takwa la wananchi, bali la Karume na Nyerere, lakini zaidi, Nyerere.

Inasemekana, hata yale yanayoitwa Mapinduzi Tukufu ya Zanzibar, yalikuwa ni mauaji katili, na yaliratibiwa na kusaidiwa, kwa sehemu kubwa, na Tanganyika. Hata silaha zilizotumika kwenye mapinduzi zilitoka Tanganyika.

Inasemekana, mapinduzi hayakulenga kumwondoa Mwarabu, bali Serikali halali kwa lengo la kukiweka madarakani Chama kilichokuwa kikiungwa mkono na Tanganyika.

Inasemekana, tokea mfumo wa Vyama vingi uanze, chama kinachoungwa mkono na Tanganyika kimekuwa kikishinda uchaguzi bila ridhaa ya wapiga kura. Kwamba kishinde kisishinde, lazima kiingie madarakani, maadam tu kinaungwa mkono na Tanganyika.

Inasemekana, hata huu Muungano uliopo kwa sasa si Muungano bali ni Ukoloni. Kwamba Tanganyika inaitawala nchi nyingine kimabavu.

Inawezekana, kama Zanzibar ingekuwa na uwezo, ingeshajitoa kwenye Muungano. Kuenedelea kwake kuwepo kwenye Muungano ni kwa sababu tu inalazimishwa na Tanganyika.

Yameshasemwa mengi na kuandikwa mengi.

Uungwana ni vitendo. Ikiwa hayo yote yanayosemwa ni kweli, basi Zanzibar wana haki ya kuulakamikia Muungano.

Kama ni kweli, nini kifanyike?

Mosi, Tanganyika iiombe radhi Zanzibar kwa yote inayoamini imeitendea Zanzibar ndivyo isivyo, na kwa yale ambayo Zanzibar inailalamikia.

Pili, kura ya maoni iitishwe kwa wananchi wa nchi ya Tanganyika na Zanzibar kuamua juu ya mustakabali wa Muungano.

Tatu, maamuzi ya wananchi yaheshimiwe.
Leo, tumeona ndugu zetu wapalestina walivo jitoa muhanga dhidi ya utawala wa wazayuni. Nyerere alipofanya mapinduzi alitumia mkataba wa utawala wa uingereza dhidi ya Ieland kututawala. Wapalestina waliwerkewa Balfour declaration na waingereza pia. Sisi wazanzibari na ndugu zetu wapalestina hatuna tafauti ila kuwa wenzetu wanatumia nguvu kujitoa kwa mkoloni na sisi tumekuwa matabaka, hatuwezi kujitoa kwa njia nyengine ya amani. Tunategemea kuchoka kwa mtawala. na wenzetu wanategemea kujikomboa. Wenzetu wa Ireland wamejikomboa. wazenji nao waamke na tutafute njia ya kujikomboa. Ukoloni na udhalilishwaji basi tena.
 
Back
Top Bottom