Tanganyika :Wakazi wa Mishamo walalamikia kukosa Uhuru kama Raia wengine

Tanganyika :Wakazi wa Mishamo walalamikia kukosa Uhuru kama Raia wengine

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Wananchi katika makazi ya Mishamo katika Mkoa wa Katavi, yenye vijiji kumi na sita (16)wamelalamikia uongozi wa mkuu wa makazi kuwakosesha uhuru wa kufanya chochote na kujiona bado ni wakimbizi ilhali walishapewa Uraia.

Baadhi ya viongozi wa vijiji hivo wameeleza kuwa hawana uhuru wa kutoka ndani ya makazi bila Kibali maalumu kutoka katika ofisi ya mkuu wa Makazi.

Ili kutoka au kusafiri nje ya makazi lazima wapewe kibali cha kutoka kisichozidi wiki 3na ndani ya huo muda wawe wamesharudi hata kama una mgonjwa amelazwa Hospitali inawalazimu kuomba kibali na hakizidi wiki tatu.

Pia wakazi hao hawaruhusiwi kuhama nje ya makazi yao kwenda kufanya shughuli nje hivyo basi kufanya vijana na baadhi ya watu wazima kutoroka nje ya Mkoa huo na kwenda mikoa mingine kutafuta maisha.

Taasisi za kijamii haziruhusiwi kuingia Na kutoa huduma mbalimbali za kijamii katika Makazi hayo ya Mishamo bila Kibali maalumu toka katika ofisi ya mkuu wa makazi.

Pamoja na Mambo mengine wakazi hao wamekuwa wakilalamika kuwa ijapo walishapewa uraia na kuwa. Watanzania lakini bado hawako huru kama ilivo kwa watanzania wengine.
 

Huwezi kumuelewa.
Lakini kuna watu, si tu wanamuelewa bali wana-feel alichokiandika.

Ni rout gani ya mabasi ya mkoani ambayo magari yanasimamishwa kisha afisa uhamiaji wanaingia kuanza kuhoji uraia wa kila abiria kama sio mikoa ya Kigoma na Katavi??
 
Huwezi kumuelewa.
Lakini kuna watu, si tu wanamuelewa bali wana-feel alichokiandika.

Ni rout gani ya mabasi ya mkoani ambayo magari yanasimamishwa kisha afisa uhamiaji wanaingia kuanza kuhoji uraia wa kila abiria kama sio mikoa ya Kigoma na Katavi??
Na mpaka kufanya hivyo basi lipo jambo!,panapokunwa ndipo panapowasha.
 
Hao ni Watanzania wenye asili ya Burundi waliokakimbia vita Mika ya nyuma kabla hata ya Uhuru. Rais JK aliwapa uraia kati ya 2008 au 2009 na kuwa kama Watanzania wengine na Wana haki sawa kama raia wengine, Serikali imewapa eneo kubwa sana la kulima,kufuga,kuvua na kuishi na huduma zote za kijamii wanapata kama Maji safi,elimu,balabala na huduma za afya zote zinapatikana.
Ila ni watu ambao walianza kutishia amani miaka ya karibuni Kwa matukio ya utekaji,uwindaji haramu,ujambazi na hata ugaidi kumbuka walikua wanamiliki silaha za vita kinyume na taratibu zetu za nchi.Ilifanyika operation kabambe maeneo hayo na kufanikiwa kuwadhibiti na kuwapora silaha hizo zoezi lilifanikiwa Kwa zaidi ya 100% naweza sema. Baada ya hapo nadhani ndio hicho wanachokilalamikia Serikali naona iliamua kuwaangalia Kwa jicho Kali kidogo.

YouTube tafuta operation safisha katumba Katavi na Kigoma utaiona.
 
Alichokiongea mleta mada ni sahihi kwa 10000%. Wale watu walishapewa uraia toka mwaka 2015 (japo swala hilo lilikuwa lishapitishwa miaka kadhaa nyuma ila walipewa vyeti rasmi 2015)

Pamoja na kupewa uraia, wale watu bado hawapati uhuru wote kama raia wengine.

a) Hawaruhusiwi kugombea nyadhifa za kisiasa kubwa kubwa kama vile kupata mwakilishi wa ubunge.

b) Kuna baadhi ya kazi hawaruhusiwi kufanya (kuhudumu/kuajiriwa) kama vile jeshini na polisi.

c) Maeneo ya watu wale bado yanatambulika kama MAKAZI (ya wakimbizi) na bado lipo chini ya mkuu wa makazi.

d) mbaya zaidi,wamekuwa wakitishiwa kunyang'anywa uraia linapotokea tukio (amablo ni kawaida kutokea kwa maneneo mengine nchini) maeneo yale linalo/lililofanywa na mtu mmoja au kikundi cha watu wachache; kama vile mtu kukutwa na silaha, kukutwa na nyara za serikali, kufanya uhalifu mwingine ambao unatokea maeneo mengine nchini.

Kama raia wengine wakitenda uhalifu wanachukuliwa sheria, na kwa watu wale iwe hivyo hivyo. KWA kuwa wameshakuwa raia, anaevunja sheria basi ashughulikiwe KWA mujibu wa sheria za nchi sio kujumuisha wote na kuanza kuwatishia TUTAWANYANG'ANYA URAIA!!

You know what?? Kutokana na changamoto hizo za kutopewa uhuru na huduma kama raia wengine, watu wanahama kule kwa speed ya 5G na kwenda kujichanganya mikoani.
 
Alichokiongea mleta mada ni sahihi kwa 10000%. Wale watu walishapewa uraia toka mwaka 2015 (japo swala hilo lilikuwa lishapitishwa miaka kadhaa nyuma ila walipewa vyeti rasmi 2015)

Pamoja na kupewa uraia, wale watu bado hawapati uhuru wote kama raia wengine.

a) Hawaruhusiwi kugombea nyadhifa za kisiasa kubwa kubwa kama vile kupata mwakilishi wa ubunge.

b) Kuna baadhi ya kazi hawaruhusiwi kufanya (kuhudumu/kuajiriwa) kama vile jeshini na polisi.

c) Maeneo ya watu wale bado yanatambulika kama MAKAZI (ya wakimbizi) na bado lipo chini ya mkuu wa makazi.

d) mbaya zaidi,wamekuwa wakitishiwa kunyang'anywa uraia linapotokea tukio (amablo ni kawaida kutokea kwa maneneo mengine nchini) maeneo yale linalo/lililofanywa na mtu mmoja au kikundi cha watu wachache; kama vile mtu kukutwa na silaha, kukutwa na nyara za serikali, kufanya uhalifu mwingine ambao unatokea maeneo mengine nchini.

Kama raia wengine wakitenda uhalifu wanachukuliwa sheria, na kwa watu wale iwe hivyo hivyo. KWA kuwa wameshakuwa raia, anaevunja sheria basi ashughulikiwe KWA mujibu wa sheria za nchi sio kujumuisha wote na kuanza kuwatishia TUTAWANYANG'ANYA URAIA!!

You know what?? Kutokana na changamoto hizo za kutopewa uhuru na huduma kama raia wengine, watu wanahama kule kwa speed ya 5G na kwenda kujichanganya mikoani.
Bushmamy you're doing a great job!! God bless you
 
Hata Rais Ndayishimiye wa burundi kwa sasa aliishi pale mishamo, na miaka ile walitengwa wakimbizi kutoka Burundi walipelekwa mishamo na wakimbizi kutoka Rwanda walipelekwa mwesi au muhesi huko katavi hawa watu walivuruga eneo lile kiusalama kwa uwindaji haramu na ujambazi ikabidi serikali iwaangile kwa jicho la tatu
 
Nashauri waangaliwe zaidi kwani wale wa mwesi na hao wa mishamo wanaporudi Rwanda au Burundi hutambuliwa na nchi zao za asili na hupewa incetives zote ikiwapo haki za kugombea uongozi, kwa ushahidi ninao ufahamu hao sio wa kuamini kabisa kwani kwenye makundi yao pia wapo askari waasi wa majeshi ya nchi zao za asili na serikali sio wajinga kuweka udhibiti kidogo namna hiyo
 
Back
Top Bottom