Tangazo la kifo cha Benjamin Mkapa, Kurungenzi ya Mawasiliano Ikulu lawamani. Inahitaji kusaidiwa kumsaidia Rais - Jicho Letu Ndani ya Habari

Magufuli is a country bumpkin.

Katangaza msiba kama kafurumushwa kutoka usingizini akalazinishwa atangaze mara moja bila ya kujiandaa.

Mengine uliyoyaandika na mimi niliyaona, nikafikiri ndiyo kibongobongo watu hawaoni hayo.
 
sababu za vifo vya viongozi zinazotolewa nyingi huwa ni za uongo kwahiyo ni bora wasiwe wanatoa sababu ya kifo!!
 
Braza hongera sana kwa kuweza kutupa hii elimu kuhusiana na hili jambo. Nakupa Good critical na like za kutosha siku ya leo.........
 
Ikulu imechemsha, Watanzania tuna haki ya kujua chanzo Cha kifo, tangazo limekaa kizuzumagic sana.
Unataka tutangaze ugojwa( changamoto ya kupumua) halafu watalii wasije? Ni marufuku kupima wala kutangaza death arising from covid19,maana virus wapo Kenya na Uganda,Rwanda na Burundi tuuu,wameogopa ku cross border kuingia Tanzania sababu ya maombi. ASANTE WAJUMBE ASANTE NDUNGULILE KWA UKOMBOZI WA TAIFA
 
Mkuu P nadhani walilinda hiyo habari isisambae mana siku hizi wajuzi tupo wengi just imagine ingetangazwa na kigogo2014 na auongezee kwa kusema jiwe amemuuwa Bwm. Huu ni Ulinzi
Ni miezi sasa huyu Kigogo kapotea? What might have happened?
 
Hata mimi sio mwanahabari wala mwanahitifaki ila niliona mapungufu mengi kwenye hilo tangazo, asante kwa kuthubutu kulisemea
 
Sure! Nina assume kuanzia leo ambavyo angekuwa busy uwanja wa taifa, na suruali zake za kubana kuonyesha makalio na hips. Mungu fundi Sana...! Nakumbuka nilihudhuria msiba wa Samwel Sita maana nilikuwa Tabora( Urambo) kipindi hicho,huyu Bashite alikuwa na mbwembwe kwenye msiba balaaa aliku ana ki drone chake ana rekodi matukio kwa mbwembwe na vurugu, yaani mc yeye,mkuu wa itifaki yeye,chakula yeye. NINA HAKIKA HUYU KWA SASA HABEBEKI HASA BAADA YA UMMA KUONYESHA DHAHILI UMEFURAHIA MAAMUZI YA WAJUMBE WA TAIFA,NATABILI KUWA HUYU ATAKUFA KIFO KIBAYA CHA AJALI YA KUTENGENEZA AU SUMU INAYOUWA TARATIBU ILI KUFICHA ALIOSHIRIKI NAE UDHALIMU WAKE WOTE.
MWAMBA huyo, katukomeshea kweli.
Sipati picha, kama mtoto pendwa angekuwa hajaionja ile sumu, kwa matukio hayo mawili, (Ya Mkapa na Lissu) angekuwa ametoa maagizo ya aina gani kwenye MKOA WAKE!
 
Update
Kumbe sababu ya kifo cha Mkapa ni Cardiac Arrest. Asante sana mwanafamilia William Erio kumaliza sintofahamu hii
Kumbe Sababu ya Kifo cha Mkapa ni Cardiac Arrest. Asante Sana Mwanafamilia William Erio Kumaliza Sintofahamu Hii!.

Kama Tangazo la kifo lingezingatia sheria tangu pale mwanzo, wala kusingetokea sintofahamu yoyote!.

Hivyo japo haijasemwa ni JF, lakini amini usiamini, mabandiko kama haya

Tangazo la kifo cha Benjamin Mkapa, Kurungenzi ya Mawasiliano Ikulu lawamani. Inahitaji kusaidiwa kumsaidia Rais - Jicho Letu Ndani ya Habari

Japo yanalaumiwa kwa kuonekana watu wana mind vitu vidogo vidogo ambayo sio vya msingi, lakini yanasaidia.

Chanzo cha kifo cha ghafla cha any state leader ambaye hajawahi kutamkwa kusumbuliwa na maradhi yoyote, automatically kita send a shock wave kwenda viral.

Baada ya kauli hii, sasa minongo yote kuhusu chanzo cha kifo imemalizwa rasmi.

RIP, Mhe. Rais Mstaafu, Benjamin William Mkapa.

Paskali
 
Hata mimi niliona hilo, hakukuwa na haraka ya rais kutangaza msiba usiku na kutupa taarifa nusu nusu, Refer tangazo la Mkapa akitangaza msiba wa Mwalimu ilikuwa clear kabisa kila kitu kilisemwakea tangazo, kwenye dress code mmh, I reserve my comments
Kutangaza ilikuwa lazima iwe usiku ule ule kabla taarifa hazijavuja mitandaoni. Ila wangemsaidia raisi kuiandaa vizuri zaidi kabla raisi hajaisema.
 
Kwa mwili wa mzee ulivyokuwaga miaka yote, haikuwa ngumu kuhisi. Mie nilihisi itakuwa moyo au stroke akiwa amelala, akapitiliza.
Hata hivyo mwenyezi Mungu amemjaalia imekuwa chapchap bila mateso. Cardiac Arrest ni bora kuliko vyanzo vingine vingi tu. Maana ni papo hapo. Apumzike kwa amani kwa kweli. Alifanya kazi kubwa akiwa raisi.
 
Kaka "nasikia,narudia tena nasikia"ni kujihami?
 
Nami kama mwandishi wa habari kwa upande wa electronic media, kuna vitu vingine niliviona lakini nikamezea tu.

1] Lighting! Sijui walikuwa wanatumia karabai? Maana mwanga wake ni hafifu sana.

2] Shot nayo haikuwa nzuri. Ilipaswa iwe tight kidogo. Rais alipaswa kupigwa waist up. Na siyo kakaa kwenye kochi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…