Tangazo la kifo cha Benjamin Mkapa, Kurungenzi ya Mawasiliano Ikulu lawamani. Inahitaji kusaidiwa kumsaidia Rais - Jicho Letu Ndani ya Habari

Tangazo la kifo cha Benjamin Mkapa, Kurungenzi ya Mawasiliano Ikulu lawamani. Inahitaji kusaidiwa kumsaidia Rais - Jicho Letu Ndani ya Habari

Wanabodi,
Naangalia Kipindi cha Jicho Letu Ndani ya Habari, kipindi kinajadili Msiba wa Benjamin Mkapa.

Tangazo la Msiba lililotolewa na Rais Magufuli, Kurungenzi ya Mawasiliano Ikulu imelaumiwa kwa kutokumsaidia rais kikamilifu kutoa tangazo hili, hali inayotafsiriwa kuwa katika baadhi ya matukio, Kurengenzi hiyo inahitaji kusaidiwa na manguli wazoefu ili waweze kumsaidia rais Magufuli katika baadhi ya matukio.

Manguli wa Mwanza, Dotto Bulendu, Edwin Soko na Moses Mathews, wamesema kwa vile hii ni shocking news, kulipaswa kuwepo kwa muda kidogo wa kumuandaa rais Magufuli kutoa tangazo hilo kulitangazia kuanzia, timing, dress code na content za tangazo lenyewe.


Timing
Kwa vile msiba umetokea usiku, kutoa tangazo saa 6:30 usiku was not the right timing kwa Watanzania, news ya msiba ingekuwa held, halafu Wahariri wakaitwa Ikulu usiku ule, halafu Tangazo litolewe live saa 12:00 asubuhi, rais akiwa na VP na PM.
TCRA kutoa taarifa vyombo vyote vya habari vya k electronic kujiunga na TBC ili hiyo live itangazwe Tanzania nzima.

Dress Code.
Kuna mavazi ya kawaida mtu anaweza kuvaa katika tukio lolote, yaani kuvaa casual, lakini kuna matukio lazima uvae, formal dress code, kutangaza msiba wa taifa, dress code should have been formal.

Wabobezi hao wanasema rais Magufuli alipaswa kushauriwa kutoa tangazo hilo akiwa amevaa a proper dress code ya tangazo hilo.

Contents za Tangazo
Tangazo la msiba wa kiongozi wa kitaifa linaongozwa na sheria ya Vifo vya viongozi, sheria imeweka contents za kisheria ambazo lazima liwe na vitu 6, likianza na National Anthem na kumalizika na National Anthem.
  1. Jina la Kiongozi ni nani
  2. Kifo kimetokea lini
  3. Kifo kimetokea wapi nchini, mkoani, safarini, nje ya nchi
  4. Mahali mahsus, kimetokea nyumba, hospitalini, safarini,
  5. Kama ni hospitalini, hospitali gani
  6. Sababu za kifo, kimesababishwa na nini, maradhi, ajali, usingizini, etc
Tangazo la rais Magufuli kutangaza kifo cha Mkapa, lilikosa, baadhi ya taratibu za tangazo muhimu kama hilo ikiwemo wimbo wa taifa, na taarifa muhimu za kisheria, hivyo kuleta sintofahamu kwa jamii.

Hajawahi kusikika kuwa Benjamin Mkapa anasumbuliwa na maradhi yoyote, hivyo taarifa kuwa amefariki hospitali ni shocking, hospitali gani na ameumwa nini, ni maswali ambayo taarifa ya rais ilikosa.

My Take
Kwa vile taarifa ya msiba ni shocking news, flaws ndogo ndogo katika tangazo la msiba huo, zinavumilika.

Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu inafanya kazi nzuri katika upashanaji habari wa shughuli za rais, lakini lazima itenganishe matangazo ya kawaida ya rais kwa shughuli za kila siku za kazi za rais na tangazo la taifa, Watu wa Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali, Dr. Hassan Abbas walipaswa kuhusishwa, na kwa vile mimi sio mserikali kujua nani alihusika, kama Dr. Abbas alihusika na bado tangazo la rais ndio lile, hii inamaanisha Dr. Abbas anaelemewa naye anahitaji kuwekewa wasaidizi.

Kwa maoni yangu, japo sheria inatamka tatangazo litolewe immediately kunapotokea msiba, kama msiba umetokea usiku wa baada ya saa 6:00, then alfajiri ni immediately kulikuwa hakuna uharaka wa kukimbilia kutangaza usiku mkubwa huo huo ili kutoa nafasi kwa rais kutangaza in a proper way na kufanya mashauriano na watu wawili watatu ili kutoa tangazo kamilifu kisheria, kikanuni na kiutaratibu na sio kumuharakisha rais kutangaza huku he looks sleepy!.

Namalizia kwa kutoa pole kwa Rais wa JMT, Dr. John Pombe Magufuli, Familia ya Mkapa na Watanzania kwa ujumla, kwa msiba huu mkubwa wa rais Mstaafu, Benjamin Mkapa.

Paskali

Update
Kumbe sababu ya kifo cha Mkapa ni Cardiac Arrest. Asante sana mwanafamilia William Erio kumaliza sintofahamu hii
Kumbe Sababu ya Kifo cha Mkapa ni Cardiac Arrest. Asante Sana Mwanafamilia William Erio Kumaliza Sintofahamu Hii!.

Kama Tangazo la kifo lingezingatia sheria tangu pale mwanzo, wala kusingetokea sintofahamu yoyote!.

Hivyo japo haijasemwa ni JF, lakini amini usiamini, mabandiko kama haya

Tangazo la kifo cha Benjamin Mkapa, Kurungenzi ya Mawasiliano Ikulu lawamani. Inahitaji kusaidiwa kumsaidia Rais - Jicho Letu Ndani ya Habari

Japo yanalaumiwa kwa kuonekana watu wana mind vitu vidogo vidogo ambayo sio vya msingi, lakini yanasaidia.

Chanzo cha kifo cha ghafla cha any state leader ambaye hajawahi kutamkwa kusumbuliwa na maradhi yoyote, automatically kita send a shock wave kwenda viral.

Baada ya kauli hii, sasa minongo yote kuhusu chanzo cha kifo imemalizwa rasmi.

RIP, Mhe. Rais Mstaafu, Benjamin William Mkapa.

Paskali

Wasaidizi wa Rais, Please Msaidieni Rais Wetu Kwenye Public . Msimuachie Kila Kitu Peke Yake!

Mayala, wakati ukikosoa kurugenzi ya mawasiliano, kosoa vyombo vyote vya habari. Ninasikiliza vyombo vingi vya habari kwa siku mbili sasa. Wengi wanapiga miziki ya furaha tu, bila kujali tangazo la msiba huu. Mawasiliano ikulu ni sehemu ya waandishi wa habari wetu nchini ambao huenda mafunzo yao, hayatoshi kuleta hisia za msiba.
Wanapitia mafunzo duni. Hata ktk TV hawawezi kuonesha hisia za taarifa wanazosoma. Mtu anasoma mapigano kwa furaha ya michezo. Anasimulia mtoto aliyebakwa bila hata hisia usoni. Waandishi habari ni habari na hawaoni kama wana wajibu wa kuibadirisha jamii.
 
Hivi kama Hayari baba wa Taifa Mwl. J.K. Nyerere tulijulishwa amefariki hospitali ya Mt. Thomas Uingereza alikokuwa amelazwa, Mzee wetu Mkapa kulikoni hatuelezwi alilazwa hospitali ipi! Ni muhimu kuelewa kuwa viongozi ni mali ya Taifa hivyo mali ya Wananchi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna watu wamepewa jukumu la kumshauri Rais katika kitu lakin naona kama hawatekelezi majukumu yao sasa sijui wanamuogopa au ni nni.

Mkuu jibu la swali lako liko ndani ya swali lenyewe! [emoji3]

Anayetakiwa ashauriwe anashaurika? Hapo ndipo issue ilipo!
 
Mkuu Pascal Mayalla
Kwa jinsi taarifa ilivyokua hakuna shaka yoyote kua ilikosa vigezo vya msingi vya ku-qualify kua imepitia kwa wabobezi wa habari, either kwa maksudi au kwa kutokujua ila haikua SMART!
 
Watanzania watamsamehe BWM kwa mabaya yake aliyotenda wakati wa uhai wake. Mwenyezi Mungu mwenye rehema amewaleta waovu na wenye mema duniani ili kuangalia matendo yetu. Ni vyema kuwa na huruma kwa waovu wengi hapa duniani ambao hawafahamu yale wanayoyatenda, maovu hayana nafasi hapa duniani.

Watanzania tuchape kazi tuondokane na umasikini wetu, tusitegemee uncle kutoka nje ya Tanzania.
 
Nimelazimika kurudia uzi huu baada ya kuona ikulu ya Chamwino haikuomba radhi baada ya andiko zuri la lenye ujumbe wa maslahi mapana ya Taifa kutoka kwa niliyemtaja hapo juu baada ya Rais wetu kuutubia taifa letu paspo kuzingatia sheria za matangazo ya vifo ya viongozi wetu wa kitaifa.

Kiukweli, Mh. Rais alitangaza kifo cha raisi wetu wa Awamu ya Tatu tatu ndivyosivyo hata Wimbo Taifa tu haukupigwa, hakuvaa vazi rasmi na mengineyo mengi.

Kimsingi, tangazo la kifo lilikuwa kama tangazo la uapisho wa viongozi au kufungua majengo fulani jambo ambalo sio kabsa.

Ikulu ya Chamwino iombe radhi watanzania kukengeuka kwa namna hii ni ishara ya kuzalilisha tunu za Taifa, ikiwemo Wimbo wa Taifa.
 
Wasamehe! tumsamehe! tuwasamehe! Msiba uliowapata alioupata tuliopata ni mkubwa in short tulivurugwa alivurugwa walivurugwa imeondoka ni nguzo muhimu
 
Hajawahi kusikika kuwa Benjamin Mkapa anasumbuliwa na maradhi yoyote, hivyo taarifa kuwa amefariki hospitali ni shocking, hospitali gani na ameumwa nini, ni maswali ambayo taarifa ya rais ilikosa.

Hata mimi bado sijui nishike lipi

  • Msaidizi wa Marehemu alisema aliondoka nyumbani kwa Mkapa na alipofika nyumbani alipata habari kuwa Mkapa amefariki
  • Msemaji wa familia anasema Marehemu alitaka kusimama kwenye kiti baada ya kutazama taarifa ya habari lakini alishindwa akakaa na kuinama, alipopimwa alionekana ameshafariki.
  • Kiongozi Mkuu anasema aliongea na Marehemu akiwa hospitali na akamwambia Yohana usiwe na wasiwasi
 
Hata mimi bado sijui nishike lipi

  • Msaidizi wa Marehemu alisema aliondoka nyumbani kwa Mkapa na alipofika nyumbani alipata habari kuwa Mkapa amefariki
  • Msemaji wa familia anasema Marehemu alitaka kusimama kwenye kiti baada ya kutazama taarifa ya habari lakini alishindwa akakaa na kuinama, alipopimwa alionekana ameshafariki.
  • Kiongozi Mkuu anasema aliongea na Marehemu akiwa hospitali na akamwambia Yohana usiwe na wasiwasi
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] mambo ni vululu tyuuuuuuh.
 
Angalia hio mistake tena ni YouTube chanel ya ikulu badala ya Urais wameandika Uraiz
20200825_095006.jpeg
 
Back
Top Bottom