Tangu kufariki Askofu Kulola, Kanisa la EAGT uongozi wake wa juu umeshindwa kuliunganisha kanisa bali kusababisha matabaka

Tangu kufariki Askofu Kulola, Kanisa la EAGT uongozi wake wa juu umeshindwa kuliunganisha kanisa bali kusababisha matabaka

Mjuba og

New Member
Joined
Apr 27, 2024
Posts
3
Reaction score
3
Tangu alipofariki aliyekuwa muasisi wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania, Dr. Moses Kulola, uongozi uliopewa dhamana kuliongoza kanisa hilo umeshindwa kuliunganisha kanisa hilo badala yake wamekuwa ni viongozi wanaolisambaratisha kanisa kwa mpasuko, matabaka, ukabila na kwa kuendekeza matumizi mabaya ya madaraka, rushwa, ubinafsi na uzandiki.

Mbali na hivyo kwa sasa watu wengi hawajui kuwa viongozi hawa wanadaiwa kutumia pesa kuwahonga viongozi wa kiserikali ili watumike kuwafukuza wachungaji wenye makanisa yenye hali nzuri kiuchumi ambao uongozi wa juu wa kanisa hauwataki kutokana na misimamo yao kiroho na kiufahamu, na unataka kuweka vibaraka wao wa ndio mzee ili wazidi kujiimarisha kiuchumi kutokana na mapato. Hali ni mbaya
 
Yule Mzee Kulola kuondoka kwake TAG na kanisa la Kristo lote hawajapata replacement ya mwinjisti mleta matokeo makubwa kama Kulola ya watu wengi kuokoka Hadi wenye ajira zao na mabosi maofisini wasio na shida yeyote

TAG haikulitendea haki kanisa la Kristo Kwa kuto m handle vizuri Mzee wa Watu .Hekima ya kiMungu haikutimika .Kanisa la EAGT lilisajiliwa hata Bila katiba na Raisi Mwinyi muislamu baada ya kuona ule mgogoro aibu watu hawasuluhishiki na mahakama Wala serikali wakati wote wanasema watu wa Mungu.Raisi Mwinyi akaamua kuwapa hati Kanisa la EAGT na jina liliamriwa serikali ili kuvunja mgogoro Kila mmoja aende kivyake serikali ipumue kuhangaika na mgogoro wao

TAG waombe Toba Kwa Mungu kwa kushindwa kutunza huruma kuwa ya uinjilisti ya Mzee Kulola

Mzee Kulola alijitambua kama Mwinjisti tu na alijulikana hivyo Kwa matokeo ya kazi zake.Sasa hivi Kuna shida mtu mchungaji anakomaa kujiita mwinjisti matokeo ya kazi yanakuwa madogo mno .Gharama za hata mikutano hazilingani na matokeo kama ya Mzee Kulola
TAG na EAGT wote losers hakuna hata mmoja katoa Mwinjisti wa kiwango Cha Moses Kulola wamebaki tu kugombea Mali tu majengo Nk lakini kwenye kutoa mwinjilisti hadhi na viwango vya Kulola hamna wanahangaika na non issues immaterial ambayo sio core business ya kanisa
 
Tangu alipofariki aliyekuwa muasisi wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania, Dr. Moses Kulola, uongozi uliopewa dhamana kuliongoza kanisa hilo umeshindwa kuliunganisha kanisa hilo badala yake wamekuwa ni viongozi wanaolisambaratisha kanisa kwa mpasuko, matabaka, ukabila na kwa kuendekeza matumizi mabaya ya madaraka, rushwa, ubinafsi na uzandiki.

Mbali na hivyo kwa sasa watu wengi hawajui kuwa viongozi hawa wanadaiwa kutumia pesa kuwahonga viongozi wa kiserikali ili watumike kuwafukuza wachungaji wenye makanisa yenye hali nzuri kiuchumi ambao uongozi wa juu wa kanisa hauwataki kutokana na misimamo yao kiroho na kiufahamu, na unataka kuweka vibaraka wao wa ndio mzee ili wazidi kujiimarisha kiuchumi kutokana na mapato. Hali ni mbaya
Hizi Pentecostal churches hakuna kanisa wala kuabudu. Wanachojuwa ni kelele na kukusanya sadaka baada ya kuwatapeli waumini wao wenye FRUSTRATION. Hakuna mtu mwenye maisha yaliyonyooka anaabudu huko

Anapokufa mwenyewe nalo linakufa. Soma thread hii hapa

TAKUKURU: Askofu na Viongozi Wakuu wa Kanisa la Avengelical assembless of God (EAGT) wachungunzwa kwa rushwa
 
Toka lini Kanisa lenye Demokrasia likatulia?
Ulaya kutokana na wimbi la demokrasia makanisa yaliyogoma kuwa na demokrasia ndani ya kanisa kama Katoliki, Anglican na Lutheran hayana watu wengi wa kusali yanafungwa Kila siku waumini hawataki kusali sababu kanisa halitaki demokrasia
 
Hizi Pentecostal churches hakuna kanisa wala kuabudu. Wanachojuwa ni kelele na kukusanya sadaka baada ya kuwatapeli waumini wao wenye FRUSTRATION. Hakuna mtu mwenye maisha yaliyonyooka anaabudu huko

Anapokufa mwenyewe nalo linakufa. Soma thread hii hapa

TAKUKURU: Askofu na Viongozi Wakuu wa Kanisa la Avengelical assembless of God (EAGT) wachungunzwa kwa rushwa
Na kiongozi wa juu wa hilo kanisa kwa sasa amekuwa anatumia sana hela kujiimarisha madarakani na umafia juu dhidi ya wapinzani wake, kanisani kwake kafukuza karibia robo ya waumini anasema ni wachawi
 
Na kiongozi wa juu wa hilo kanisa kwa sasa amekuwa anatumia sana hela kujiimarisha madarakani na umafia juu dhidi ya wapinzani wake, kanisani kwake kafukuza karibia robo ya waumini anasema ni wachawi
huyo aliyefukuza karibia robo ya waumini wake akidai ni wachawi ni kiongozi wa kanda mojawapo ya kanisa lao sio kiongozi wa juu.
 
Na kiongozi wa juu wa hilo kanisa kwa sasa amekuwa anatumia sana hela kujiimarisha madarakani na umafia juu dhidi ya wapinzani wake, kanisani kwake kafukuza karibia robo ya waumini anasema ni wachawi
Viongozi wa juu wa kanisa wanatakiwa kuheshimiwa sana na wachungaji wa Chini Tatizo lililoko makanisa ya kiroho baadhi hawana adabu Kwa viongozi wao wa juu akiona Kuna kitu anamzidi bosi wake wa juu anaota mapembe kuwa yeye ndie ana upako sana kuliko kiongozi wa juu yake au askofu anasahau maombi Yesu aliomba kuwa wanaomwamini wafanye mambo makubwa kuliko yeye

Yesu alihubiri Israel tu Billy Graham alihubiri kupitia TV wakaokoka mabilioni wengi.kuliko Yesu lakini yote yaliwezekana sababu Yesu aliomba wafuasi wafanye makubwa kuliko yeye

Matatizo mengi ya makanisa ya kipentecoste viongozi wa Chini Wana roho ya kora Mpinga Musa na Absalom Mpinga Daudi hawaheshimu viongozi wa juu yao akiwa na kakipawa ka kumzidi askofu au kiongozi wa juu yake au kanisa kubwa au upako anaota mapembe anaona yeye ndio yeye walio juu yake wajinga tu hawana wito Wala upako ni yeye tu kumbe wanaomba watu wa Chini Yao wafanye makubwa kuliko wao kama Yesu alivyoomba

Shida ndio huanzia hapo kwenye baadhi ya makanisa ya kipentecoste
 
Ulaya kutokana na wimbi la demokrasia makanisa yaliyogoma kuwa na demokrasia ndani ya kanisa kama Katoliki, Anglican na Lutheran hayana watu wengi wa kusali yanafungwa Kila siku waumini hawataki kusali sababu kanisa halitaki demokrasia
Siyo kweli. Umeandika uwongo kuhalalisha unachoamini. Katika kila watu 10 duniani, wawili ni wakatoliki. (. As of 2020, Catholicism is the second-largest religious body in the world after Sunni Islam. Church membership, defined as baptized Catholics, was 1.378 billion at the end of 2021, which is 17.67% of the world population)
Screenshot_20240428_082228_Google.jpg
 
Siyo kweli. Umeandika uwongo kuhalalisha unachoamini. Katika kila watu 10 duniani, wawili ni wakatoliki. (. As of 2020, Catholicism is the second-largest religious body in the world after Sunni Islam. Church membership, defined as baptized Catholics, was 1.378 billion at the end of 2021, which is 17.67% of the world population)View attachment 2975781
Wakatoliki wengi eanapatikana Afrika na Amerika ya kusini

Ulaya kumedoda Sasa hivi Kuna wakatoliki wachache
 
Tangu alipofariki aliyekuwa muasisi wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania, Dr. Moses Kulola, uongozi uliopewa dhamana kuliongoza kanisa hilo umeshindwa kuliunganisha kanisa hilo badala yake wamekuwa ni viongozi wanaolisambaratisha kanisa kwa mpasuko, matabaka, ukabila na kwa kuendekeza matumizi mabaya ya madaraka, rushwa, ubinafsi na uzandiki.

Mbali na hivyo kwa sasa watu wengi hawajui kuwa viongozi hawa wanadaiwa kutumia pesa kuwahonga viongozi wa kiserikali ili watumike kuwafukuza wachungaji wenye makanisa yenye hali nzuri kiuchumi ambao uongozi wa juu wa kanisa hauwataki kutokana na misimamo yao kiroho na kiufahamu, na unataka kuweka vibaraka wao wa ndio mzee ili wazidi kujiimarisha kiuchumi kutokana na mapato. Hali ni mbaya
Hili ni funzo sio EAGT tu hata hizi ministry unakuta ni one man show siku akidondoka kanisa linaparaganyika. Mfano kanisa kama la Kakobe au Gwajima maaskofu ni wao tu miaka na miaka utadhani ni mali binafsi siku wakidondoka unatarajia itakuaje? Kanisa lazima lipasuke

Solution ni kwamba umri ukienda sana anza kuandaa succession plan ili viongozi wapya watambulike na wapewe nafasi mapema kabla hujafariki. Ikiwezekana anateuliwa askofu mpya ukiwa wewe bado upo hai. Hapa hata ukidondoka hakuna risk
 
Back
Top Bottom