Uchaguzi 2020 Tangu Tanzania ipate Uhuru, kwa mara ya kwanza CCM inaenda kutumia nguvu nyingi kufanya kampeni

Uchaguzi 2020 Tangu Tanzania ipate Uhuru, kwa mara ya kwanza CCM inaenda kutumia nguvu nyingi kufanya kampeni

Mkuu ni kosa kubwa Sana kutoshiriki, maana ingekuwa hivyo magufuli asingeshiriki kuomba kugombea kipindi kile kupitia Ccm, hata wewe hapo ulipokaa unakumbuka na kufaham kuwa magufuli aliingia kwenye kinyanganyiro akihisi kuwa hawez fanikiwa yeye mwenyewe alihisi hivyo na wewe na Mimi na huyo uliekaaa nae hapo pembeni alijua hivyo, Hakuna aliejua kuwa magufuli angekuwa rais, asilimia Mia waligawanyika Kwa membe na lowasa Lakini hawakupita akaja kuwa magufuli, ninachotaka kukuambia kuwa ajue kesho yako ni MUNGU pekee, lolote linaweza kutokea hapo katikati, MUNGU ni Mkubwa kuliko binadam kwenye dhuluma iliyoko mbele, huwa anaiona mbele kabla Ya wewe, maisha Ya binadam na mfumo wa uongozi MUNGU huwa anaujua kabla na sisi huwa tunaangalia recorded iliyokwisha chezwa Akiwa anaangalia MUNGU

Kutokuwa na uhakika wa kushinda ni kitu kimoja na kujua haki haiwezi kutendeka ni kitu kingine. Kama Magufuli angekuwa na mashaka juu ya haki kutendeka bila shaka asingeshiriki hata kwenye hicho kinyang’anyiro!

Ni Tanzania pekee ambako utakuta mtu anashiriki uchaguzi akijua kwamba asiposhinda yeye, basi uchaguzi haukua huru na wa haki! Huo sio uchaguzi!
 
Kwa mujibu wa PolePole taarifa aliyoitoa juzi inaonesha kuwa Uchaguzi wa Mwaka huuu Ccm inaenda kufanya kampeni kubwa ambazo hazijawahi kushuhudiwa tangu nchi hii ipate uhuru.

Swali langu inamaana CCM Uchaguzi huuu inawasiwasi Mkubwa kushindwa? Au kuna mgombea wa upinzani ambae anaifanya CCM iwe na hofu?

Katika akiri tu Ya kawaida ukisikiliza maneno Ya Pole Pole yanaonesha pia kuwa Uchaguzi huuu utapelekea CCM kutumia hela nyingi kuliko chaguz zote zilizowahi kufanyika tangu Tanzania iiingie kwenye mfumo wa vyama vingi, hiii inanishangaza na kauli nyingi zilizokuwa zinatolewa huko Nyuma na baadhi ya wanaccm kuwa magufuli haitaji hata kufanya kampeni, wengi Walisema kuwa magufuli na CCM haviona sababu ya kufanya kampeni.

Unaweza kugundua kuwa CCM wenyewe wana hofu iliyopitiliza, maaana kukusanya tu wasanii zaid ya Mia moja pamoja watatumia pesa nyingi Sana na hiyo Yote ni hofu ya kushindwa, sasa kelele zooote za kutamba kuwa hakuna haja ya magufuli kufanya kampeni zimeenda wapi? Au kuna mgombea wa upinzani ambae hakudhaniwa kuwa atagombea sasa kajitokeza gafla wazee wakabadili gia angani?
Hapo wanatengeneza mazingira ya wizi wa kura. Itakapolalamikiwa kuwa wizi mkubwa wa kura umetokea, wao watadai wamepata kura nyingi kihalali ushahidi ikiwa ni kampeni ya nguvu waliyoifanya.
 
Usiseme chama Ndugu Mimi ni Ccm damu naomba nikueleze kuwa Kwa sasa Hakuna Ccm, huo ndio ukweli, Ccm ya zamani yenye democracy haipo, Ccm Kwa sasa ni mtu mmoja tu ndio mwenye maaamuz, magufuli ndio mwenye maaamuzi pekee yake ndio mwaaamuz wa kila Jambo hata wale unaowaona akina bashiru hana mamlaka yoyote Ccm imechukuliwa na magufuli Nani awe diwani, Nani awe Mbunge ni mtu mmoja tu ndio mwenye mamlaka na Kwa taarifa yako wale tu wanaokula Kwa kutokana na Ccm ndio wanaomuunga mkono Kwa asilimia Mia ila wale wanaoishi Kwa kutegema nguvu zao wanamuunga mkono kinafiki hawapo nae na wengi hawatampigia Kura Kama Mimi na ukoo wetu wote

Kwani mkuu wewe unaisha wapi? Inaonekana huijui vizuri hali ya democracy ndani ya vyama vya kisiasa vya Tanzania. Kwa ujumla iko chini ya kiwango. Na ndani ya vyama vya upinzani ndiyo kabisaaa (katiba ya chama, miongozo na kanuni zote ni formality ya kisheria na kwamba matakwa ya kiongozi mkuu wa chama ndiyo katiba, miongozo na kanuni zinazoendesha chama)!
 
Back
Top Bottom