Wacha akutane na waandishi maana inaonyesha wameshajipanga kumjambisha Mengi ,ila WaTanzania msiwe na pupa hivi ni vita vya wenyewe kwa wenyewe ,hawa ni wafadhili wakuu wa Serikali ya Sultani CCM ,hawa ndio wanaochangia mfuko wa Sultani CCM ,hawa ndio wanaowahonga wasimamiaji wa Uchaguzi ,hawa ndio wanaowanunua mawakala wa upinzani ,hawa ndio wanaotumika katika kuchangia ili Sultani CCM afanikiwe katika kufanya hujuma za kukwiba kura na kugeuza matokeo ,hawa ndio wanaoiua Tanzania kwa kuwatumia wafuasi wa Sultani CCM kupitisha mikataba mibovu isiyona faida kwa Taifa hili la Tanzania ,hawa hawana rangi kuwa ni weupe au ni weusi ,hawa ni watu ambao sura zao utaziona zina uchungu na Taifa hili wakati wanapofanya mikutano na vyombo vya habari ,lakini ndani ya mioyo yao ni maadui wakubwa wao na chama chao wanachokisapoti. CCM imewalea kwa kuwatunza na kuwapa uhuru wa kufanya lolote walitakalo leo ni matajiri wakubwa kutokana na hila na ulaghai ,kiasi cha kuifanya serikali ya Sultani CCM isiweze kuwachukulia hatua yeyote ile na kubaki viongozi wake wakisema ,sheria ifuatwe ,sheria iheshimiwe ,haifai hiki na hakifai kile ,uwongo mtupu kuanzia juu mpaka chini ,hivi ikiwa serikali haiheshimu sheria nani atakaejali kama kuna sheria inayofaa kufuatwa ,zaidi tutaonewa mimi na wewe masikini za Mungu tusio nakitu,ndio maana wakikuona umepanga mafungu ya muhogo na malimau wanakuja na kukubomolea na wakikukamata wanakusweka hata jela wala hawafanyi kesi au kukupeleka mahakamani ,sheria wanazileta na kuziona zina maana ikiwa tu wahusika ndani ya serikali wanahusika na ubadhirifu ,hapo sheria zote zitawekwa hadharani ,wakipita na majalada ya kesi kwenda nayo kulia na kushoto ,ukiwauliza kuna kubwa lipi mbona kesi haziendi zimekwama ,wanakwambia uchunguzi haujakamilika au utawasikia wakisema hali ni ngumu kupambana na watu hawa !
Majina ya wanaoingiza unga ( Cocaine wanayajua)
Majina ya mafisadi bandarini wanayajua.
Majina ya mafisadi wa BOT wanayajua.
Majina ya mafisadi EPA wanayajua.
Majina ya Mafisadi Radar wanayajua.
Majina ya ya ya ya ya yote wanayajua ,hivyo kila kitu wanakijua ,sasa lipi liwashindalo kuwachukulia hatua za haraka watu hawa ? Serikali kama imeshindwa kuwachukulia hatua itangaze hadharani ili isiwasumbue wananchi na maneno ya kila siku ,kuwa tunawajua ,majina tunayo na hiki na kile ?
jamani uopngozi na utawala wa Nchi hii kama umewashinda basi isiwe mbinde ondokeni madarakani ili muwapishe wanaoweza ,Kikwete hujaharibu kitu ikiwa utaamua kutangaza kuwa umeshindwa kazi ,na sio umeshindwa bali kutokana na maswahiba wako kuwa wahusika wakuu na hivyo inakuwia vigumu kuweka sheria ya msumeno ,hakuna kubwa tangaza rasmi na hakutakuwa na shida wala kelele kutoka kwa wananchi ,naamini kabisa watakuelewa na pengine kuzidi kuheshimika .maana jitihada zako za kupanga na kupangua zimegonga mwamba na watu hao unaowapanga wamekuwa sugu na hawafuati amri zako tena ,wanajifanyia wanavyotaka wao ,hivyo ni bora uwatupe mkono na kutangaza kuivunja serikali na kila mmoja atajijua namna ya kujipapatua ,itakapokuja serikali ya kweli isiyo na uswahiba ,Kikwete tunakusikia unaposema sheria zifuatwe kwa kuwa na utawala bora unaofuata sheria na kila Mtanzania ana haki ya kuhukumiwa na kufunguliwa mashtaka kwa mujibu wa sheria ,lakini leo ni mwaka wa tatu tokea malalamiko yatokee ,waliojiuzulu wamejiuzulu ,uliowapangua umewapangua ,lakini kumekuwa na ucheleweshaji wa makusudi unaofanywa nawatendaji walio chini yako ,wakidai wanafuata sheria kuyafikisha na kuzisikiliza kesi lakini hao wote ni waongo na hawana moja wanalolifanya zaidi ya kunua muda kwa kutumia upole wako,hivyo mpishe mwengine ambae atapimwa kwa kuharakisha kuwapatia WaTz hatima ya kukabiliana na mafisadi kwa haraka. NCHI INADIDIMIA KATIKA DIMBWI LILILOHATARI SANA.