Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Mhandisi Kasekenya, ametoa agizo hilo Mkoani Kigoma leo tarehe 11 Januari, 2025 wakati akikagua miradi ya ujenzi inayoendelea kutekelezwa kwenye Sekta ya Elimu, Afya, Maji na Masoko kwa ushirikiano baina ya Halmashauri za Buhingwe, Manyovu, Kibondo na TANROADS.
Miradi hiyo inayotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa Shule ya Bweni Buhingwe, Kituo cha mabasi na uzio wa soko Manyovu, Ujenzi wa visima vya maji Buhingwe na Manyovu, Ukarabati wa Hospitali ya Kasulu pamoja na ujenzi wa Hospital Makere na Kibondo.
Amefafanua kuwa miradi ya CSR, ni miradi ambayo inajengwa kwa fedha za uwajibikaji wa kampuni kwa jamii kama vile ujenzi wa visima vya maji, shule, hospitali ambavyo vimetekelezwa kwenye Ujenzi wa barabara ambazo zinaendelea kujengwa Mkoani humo.
Kwa upande wake, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kigoma, Mhandisi Narcis Choma, ameahidi kuwa kupitia TANROADS na Wilaya za Buhingwe, Kibondo na Manyovu watashirikiana kuhakikisha Miradi hiyo yote ya CSR inakamilika kwa muda uliopangwa.