TANROADS yamjibu Khana Mbarouk, ubovu wa barabara na msongamano wa magari barabara kuu Mbagala - Kongowe

TANROADS yamjibu Khana Mbarouk, ubovu wa barabara na msongamano wa magari barabara kuu Mbagala - Kongowe

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Mohamed Besta amesema wameiona video clip iliyopostiwa na Mtangazaji wa Clouds media Khan Mbarouk siku mbili zilizopita inayoonesha ubovu wa barabara na msongamano wa magari katika barabara kuu iendayo mikoa ya kusini mwa Tanzania kipande cha Mbagala - Kongowe Jijini Dar es Salaam.

Kwenye mazungumzo na wanahabari jijini Dar es asalaam Mhandisi Besta amedokeza kuwa mpaka sasa mchakato wa manunuzi kwaajili ya ujenzi wa kipande cha barabara ya Mbagala Rangi tatu - Kongowe 3.8km kwa upanuzi wa njia 4 umeanza na utakamilika ndani ya wiki 4.

Aidha Mhandisi Besta ameongeza kuwa kwa kipindi cha miaka 4 cha Rais Samia hadi kufikia sasa karibu theluthi ya barabara zote nchini zimejengwa kwa kiwango cha lami na kuchochea uchumi kwa jamii zinazopitiwa miradi ya barabara hizo.


==========================​

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mhandisi Mohamed Besta, amesema Barabara zilizopo chini ya TANROADS zenye Kilometa 12,022 zipo kwenye Kiwango cha Lami.

Ameyasema hayo leo tarehe 07 Machi, 2025 wakati akiongea na Wanahabari kuhusu Miradi mbalimbali ambayo inaendelea Nchini ikiwemo ya barabara, Madaraja pamoja na Viwanja vya ndege.

Besta amesema theluthi ya Barabara zilizopo chini ya TANROADS ni za Lami.

"Mpaka sasa katika Nchi yetu tuna Kilometa 37,300 za urefu wa barabara ambazo zimekasimiwa na TANROADS na kati ya hizo Kilometa 12,022 zipo kwenye Kiwango cha Lami. Vilevile TANROADS inasimamia Madaraja 9,563 Nchi nzima ambayo yameshajengwa kwa awamu zote 6. Ndani ya Miaka minne ya Rais Samia Suluhu Hassan ameweza kukamilisha miradi 8 Mikubwa ya Madaraja Nchini na kuna Miradi 10 mingine ya Madaraja inaendelea kujengwa. Amesema Mhandisi Besta.

Mhandisi Besta amesema katika kindi cha miaka minne ya Rais Samia Suluhu Hassan TANROADS wameweza kujenga Kilometa 1366 za barabara ambazo ni Wastani wa Kilometa 400 kwa Mwaka.

Mhandisi Besta amesema TANROADS ina Kilometa 15,225 ya Miradi ambayo ipo kwenye hatua mbalimbali ya kujengwa na kufanyiwa Upembuzi yakinifu.

Mhandisi Besta ameongeza kuwa kuna Miradi ya Viwanja vya ndege inaendelea kujengwa na vipo kwenye hatua mbalimbali za utekelezani na vingine vimekamilika.

"Kiwanja kwa mfano cha Msalato kimefikia katika hatua nzuri na Vilevile na Viwanja vingine vya Mkoa kama vile Shinyanga, Sumbawanga, Musoma, Kigoma na Kwingineko. Na kuna miradi ambayo imekamilika kama Mtwara, Songea pamoja na Songwe". Amesema Mhandisi Besta.

Katika Mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Besta amesema Manunuzi ya Barabara ya Kilwa kutoka Mbagala rangi tatu mpaka Mbagala Kongowe Kilometa 3.8 yatakamilika Wiki ya nne ya Mwezi Machi 2025.

Mhandisi Besta amehitimisha kwa kisema kwamba hii barabara itajengwa kwa njia nne kama Rais Samia Suluhu Hassan alivyoagiza kwani hio barabara ina Msongamano sana. Tumeshafanya majadiliano na Mkandarasi ambaye amata mradi huu kuangaalia jinsi ya Kupunguza Msongamano.

=======================
Video ya Khan Mbarouk

Pia soma:
~
Barabara ya Mbagala hadi Kongowe ni nyembamba, ina mashimo na inasababisha foleni mara nyingi
~ Meneja TANROADS aelezea ulipofikia mchakato wa Ujenzi wa Barabara ya Mbagala Mzinga - Kongowe - Kisemvule
~ Barabara ya Mbagala hadi Kongowe inatesa wananchi Serikali itupie jicho
 
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Mohamed Besta amesema wameiona video clip iliyopostiwa na Mtangazaji wa Clouds media Khan Mbarouk siku mbili zilizopita inayoonesha ubovu wa barabara na msongamano wa magari katika barabara kuu iendayo mikoa ya kusini mwa Tanzania kipande cha Mbagala - Kongowe Jijini Dar es asalaam.

Kwenye mazungumzo na wanahabari jijini Dar es asalaam Mhandisi Besta amedokeza kuwa mpaka sasa mchakato wa manunuzi kwaajili ya ujenzi wa kipande cha barabara ya Mbagala Rangi tatu - Kongowe 3.8km kwa upanuzi wa njia 4 umeanza na utakamilika ndani ya wiki 4.

Aidha Mhandisi Besta ameongeza kuwa kwa kipindi cha miaka 4 cha Rais Samia hadi kufikia sasa karibu theluthi ya barabara zote nchini zimejengwa kwa kiwango cha lami na kuchochea uchumi kwa jamii zinazopitiwa miradi ya barabara hizo.
Video ya Khan Mbarouk
View attachment 3262621
Kwanini wasijenge njia sita au wanataka baada ya miaka miwili watu waanze kulalamika Kisha wabomoe waongeze nyingine Kisha wabomoe tena waongeze na mwendo Kasi?
 
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Mohamed Besta amesema wameiona video clip iliyopostiwa na Mtangazaji wa Clouds media Khan Mbarouk siku mbili zilizopita inayoonesha ubovu wa barabara na msongamano wa magari katika barabara kuu iendayo mikoa ya kusini mwa Tanzania kipande cha Mbagala - Kongowe Jijini Dar es asalaam.

Kwenye mazungumzo na wanahabari jijini Dar es asalaam Mhandisi Besta amedokeza kuwa mpaka sasa mchakato wa manunuzi kwaajili ya ujenzi wa kipande cha barabara ya Mbagala Rangi tatu - Kongowe 3.8km kwa upanuzi wa njia 4 umeanza na utakamilika ndani ya wiki 4.

Aidha Mhandisi Besta ameongeza kuwa kwa kipindi cha miaka 4 cha Rais Samia hadi kufikia sasa karibu theluthi ya barabara zote nchini zimejengwa kwa kiwango cha lami na kuchochea uchumi kwa jamii zinazopitiwa miradi ya barabara hizo.
Video ya Khan Mbarouk
View attachment 3262621


Kupinga Maelezo ya Besta kuhusu Maendeleo ya Barabara chini ya Rais Samia

Katika taarifa yake, Mhandisi Besta ametoa maelezo ya kupigiwa debe kuhusu maendeleo ya barabara nchini chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.

Anadai kwamba karibu theluthi ya barabara zote nchini zimejengwa kwa kiwango cha lami, na kwamba maendeleo haya yamechochea uchumi wa jamii zinazozunguka miradi hiyo.

Hata hivyo, ukweli ni kwamba taarifa hizi si za kweli na zinahitaji kupingwa vikali.

Kwanza, tunapaswa kujiuliza: Barabara hizi ziko wapi? Ni barabara zipi zilizojengwa kwa kiwango cha lami?

Katika maeneo mengi ya nchi, hali ya barabara ni mbaya.

Kwa mfano, barabara inayounganisha Arusha na Moshi imeshindwa kutengenezwa ipasavyo, na badala yake imejaa mashimo.

Hali hii inawakatisha tamaa wananchi wanaotegemea barabara hizi kwa ajili ya usafiri wa kawaida na biashara.

Pia, barabara ya Babati kuelekea Singida ina mashimo mengi, na hivyo kufanya safari kuwa ngumu na hatari.

Hali hii inakwamisha shughuli za kiuchumi na inawafanya wananchi kuishi katika mazingira magumu.

Hatuwezi kusahau barabara ya Tabora kuelekea Chunya, ambayo kwa sasa inakabiliwa na changamoto kubwa za vumbi na makongorozi, hali inayoathiri usafiri na biashara katika eneo hilo.

Aidha, barabara inayounganisha Mbeya na Makombako imejaa mashimo, na hali hii inawafanya abiria na bidhaa kuweza kusafiri kwa shida.

Ni wazi kwamba, ingawa Mhandisi Besta anajaribu kuonyesha picha chanya, ukweli ni kwamba barabara nyingi nchini bado hazijajengwa ipasavyo, na hivyo zinahitaji uangalizi wa haraka na wa kina.

Kwa hivyo, ni muhimu kwa wananchi wa Tanzania kuwa na ufahamu wa hali halisi ya barabara nchini. Wanapaswa kujua kwamba maelezo ya Mhandisi Besta ni ya kupotosha, na kwamba Rais Samia hana maendeleo makubwa ya kiuchumi yanayoonekana kupitia barabara hizo

Ni dhahiri kwamba, badala ya kuimarisha uchumi, hali hii inawafanya wananchi kuwa na changamoto zaidi katika maisha yao ya kila siku.

Katika uchaguzi ujao, ni muhimu kwa wapiga kura kufikiria kwa makini kabla ya kumchagua Rais Samia kwa kipindi kingine cha miaka mitano.

Hatuwezi kuendelea kuishi kwa matumaini yasiyo na msingi, wakati ukweli wa maisha yetu unazidi kuwa mgumu.

Wananchi wanahitaji viongozi ambao wataweza kuleta mabadiliko ya kweli na kuimarisha miundombinu, badala ya viongozi wanaotoa taarifa za uongo ili kujijenga kisiasa.

Kwa hiyo, ni wajibu wetu kuhamasisha wananchi wote wasimchague Rais Samia kwa kipindi Cha pili

Tunahitaji viongozi ambao watajitolea kwa dhati katika kuboresha hali ya maisha ya watu, sio wale wanaoshindwa kutimiza ahadi zao.

Kwa hivyo, tuungane katika kutafuta mabadiliko na kuleta maendeleo halisi nchini Tanzania.
 
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Mohamed Besta amesema wameiona video clip iliyopostiwa na Mtangazaji wa Clouds media Khan Mbarouk siku mbili zilizopita inayoonesha ubovu wa barabara na msongamano wa magari katika barabara kuu iendayo mikoa ya kusini mwa Tanzania kipande cha Mbagala - Kongowe Jijini Dar es asalaam.

Kwenye mazungumzo na wanahabari jijini Dar es asalaam Mhandisi Besta amedokeza kuwa mpaka sasa mchakato wa manunuzi kwaajili ya ujenzi wa kipande cha barabara ya Mbagala Rangi tatu - Kongowe 3.8km kwa upanuzi wa njia 4 umeanza na utakamilika ndani ya wiki 4.

Aidha Mhandisi Besta ameongeza kuwa kwa kipindi cha miaka 4 cha Rais Samia hadi kufikia sasa karibu theluthi ya barabara zote nchini zimejengwa kwa kiwango cha lami na kuchochea uchumi kwa jamii zinazopitiwa miradi ya barabara hizo.
Video ya Khan Mbarouk
View attachment 3262621
Aidha Mhandisi Besta ameongeza kuwa kwa kipindi cha miaka 4 cha Rais Samia hadi kufikia sasa karibu theluthi ya barabara zote nchini zimejengwa kwa kiwango cha lami na kuchochea uchumi kwa jamii zinazopitiwa miradi ya barabara hizo.

SASA HIYO INAHUSIANA NINI NA TATIZO HUSIKA?🥺🥺🥺
 
Aidha Mhandisi Besta ameongeza kuwa kwa kipindi cha miaka 4 cha Rais Samia hadi kufikia sasa karibu theluthi ya barabara zote nchini zimejengwa kwa kiwango cha lami na kuchochea uchumi kwa jamii zinazopitiwa miradi ya barabara hizo.

SASA HIYO INAHUSIANA NINI NA TATIZO HUSIKA?🥺🥺🥺
Tanroads imekufa siku alipokufa JPM
 
Aidha Mhandisi Besta ameongeza kuwa kwa kipindi cha miaka 4 cha Rais Samia hadi kufikia sasa karibu theluthi ya barabara zote nchini zimejengwa kwa kiwango cha lami na kuchochea uchumi kwa jamii zinazopitiwa miradi ya barabara hizo.

SASA HIYO INAHUSIANA NINI NA TATIZO HUSIKA?🥺🥺🥺
Shangaa na wewe Hakimu
 
Tunaviongozi wajinga na wapumbavu.kila changamoto inayotolewa watajidai kuwa ipo kwenye mchakato na mkandarasi yupo karibu kupatikana ndani ya mwezi fulani wakati tatizo ni la zaidi ya miaka sita.Mfano wilaya ya Ubungo kunasehemu hawana kabisa huduma ya maji hasa makabe,misumi na msakuzi lakini ukiwauliza Dawasa watasema tupo mbioni kupeleka hiyo huduma wakati ni tatizo la miaka mingi Toka tupate uhuru.Kazi ni kusifia tu rais lakini matokeo ni zero kabisa
 
Aidha Mhandisi Besta ameongeza kuwa kwa kipindi cha miaka 4 cha Rais Samia hadi kufikia sasa karibu theluthi ya barabara zote nchini zimejengwa kwa kiwango cha lami na kuchochea uchumi kwa jamii zinazopitiwa miradi ya barabara hizo.

SASA HIYO INAHUSIANA NINI NA TATIZO HUSIKA?🥺🥺🥺
Wanatafuta pakujishikilia😌😌
 
Aidha Mhandisi Besta ameongeza kuwa kwa kipindi cha miaka 4 cha Rais Samia hadi kufikia sasa karibu theluthi ya barabara zote nchini zimejengwa kwa kiwango cha lami na kuchochea uchumi kwa jamii zinazopitiwa miradi ya barabara hizo.

SASA HIYO INAHUSIANA NINI NA TATIZO HUSIKA?🥺🥺🥺
Siku hizi kusafisha nyota na kuondoa mabalaa sio kwa waganga tu! Lipo jina!
 
Sasa kulikuwa na ulazima gani wa kumtaja Samia.
Ukiona mtu anamtaja huyo mama, au Kuna picha yake,ujue Kuna wizi mkubwa au uzembe mkubwa sana.
Mfano hapa! Kuna wizi mkubwa sana
 

Attachments

  • IMG-20250307-WA0028.jpg
    IMG-20250307-WA0028.jpg
    113.7 KB · Views: 1
Back
Top Bottom