Tanzania: Consumer Protection Ipo?

Tanzania: Consumer Protection Ipo?

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
17,048
Reaction score
22,790
Mwaka juzi (2007) nilikuwa nyumbani nikiwa namwuguza ndugu yangu wa karibu sana. Ikafika wakati wa sikukuu ya Krismas, na nikaamua nimnunulie mgonjwa huyo zawadi ya viatu, lakini nilitaka kum-surprise; hata hivyo sikuwa najua saizi ya miguu yake sawasawa. Nikabshiri kuwa huenda atakuwa anavaa namba 8, hivyo nikanunua pea nzuri sana ya bei nzuri pia. Kwa bahati mbaya, mgonjwa yule alikuwa anavaa namba 7 kwa hiyo namba nane ikampwaya. Nikasema hakuna tatizo ngoje niende nikabadilishe kule dukani nilikonunua nipewe namba 7. Dah!!, pamoja na kurudi nikiwa na sales receipt yangu, tena siku hiyo hiyo niliyokuwa nimenunua viatu hivyo, mwenye duka alinikatalia kata kata. Nikaamua kutoa viatu vile kwa mtu mwingine tu, na badala yake ninunue pea nyingine ya namba 7 kwa ajili ya mgonjwa wangu.

Huo ni mwaka mzima umepita tangu hayo yanipate. leo hii nikiwa pale kwa shigongo nikatutana na hii sales receipt inayoonyesha kiuwa ukishanunua kitu, basi huwezi kukirudisha, ndipo nikakumbuka ule mkasa wangu. je Tanzania tuna utaratibu wowote wa kumlinda mlaji iwapo atanunua kitu ambacho hakikidhi mahitaji yake ama kwa ubora au kwa sababu yeyote ile?

attachment.php
 

Attachments

  • 1231223412_1w.jpg
    1231223412_1w.jpg
    33.3 KB · Views: 153
Wafanya biashara wa bongo hawajiamini na wao wameweka mbele tamaa ya kupata tu, ndiyo kwa maana ukinunua bidhaa dukani ukishailipa tu umejifunga na hiyo bidhaa hata kama baada ya nusu saa utakuwa hukuipenda basi huwezi kirudisha tofauti na nchi nyengine unaweza kununua bidhaa na kuirudisha tena dukani hata baada ya siku saba ilimradi usiichafue au kuiharibu.
Maduka mengi ya bongo yanayouza vitu vya electronic hayatoi warrant kabisa, ikikutokea bahati mbaya bidhaa ikiharibika kwa fluctuations za umeme basi ndio imeisha hiyo hasara juu yako. Ipo haja ya serikali kuunda chombo cha kumsimamia mlaji na kukataza hizi risiti zinazokataza kurudisha bidhaa dukani hata kama umeuziwa ikiwa mbovu.
 
Back
Top Bottom