Tanzania haina Mapato ya kubeba ongezeko la Mishahara yote kwa asilimia 23.3%

Tanzania haina Mapato ya kubeba ongezeko la Mishahara yote kwa asilimia 23.3%

Punguza kuwa nabii wa majanga (prophet of doom). SSH ameamua kuongeza mishahara ni suala zuri kuliko kuumiza mamilioni ya watu wakaishi kwa vinyongo wakati maisha haya ni mafupi.

Unazilipiaje? Wewe na wenzako kwenye serikali hii? Mtuambie. Ni rahisi sana kumuita mtu majina ukikosa majibu.

Hakuna binadamu , Mtanzania ambaye hapendi Watanzania wote wawe na maisha mazuri.

Mapato yanapungua, matumizi yanaongezeka.

Tuonyeshe hizi pesa zitatoka wapi, mikopo? Kodi zingine zaidi?
 
Punguza kuwa nabii wa majanga (prophet of doom). SSH ameamua kuongeza mishahara ni suala zuri kuliko kuumiza mamilioni ya watu wakaishi kwa vinyongo wakati maisha haya ni mafupi.

Kwanini mmetoa ruzuku kwa wakulima ambao ndio wengi 70% ya Watanzania.

Mshaurini vizuri SSH kwenye vikao vyenu. Kukuza uchumi kwa kasi punguzeni kodi, ukiritimba, milolongo, biashara zitashamiri.
 
Ukisoma vizuri kitabu cha WHY NATIONS FAIL ( The Origins of Power,Prosperity & Poverty) cha DARON ACEMOGLU na JAMES A.ROBINSON utajua kwa uhakika ni kwa nini Tanzania yetu ni masikini hivi na itachukua muda mrefu kubadili hali hii.

Kwa ufupi ni kwamba tunacho kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya maendeleo katika Nchi yetu kasoro watu wenye maarifa na taasisi imara.

Hata watu wachache wenye maarifa tulionao pia wana maarifa yaliyopitwa na wakati (obsolete) au waliyo karirishwa tu! Tunaweza kusema maarifa yao hayo ni USELESS KNOWLEDGE tu.

Nchi bila uzalishaji na kuingiza Nguvu kazi kubwa katika uzalishaji ili kuongeza tija ni kazi bure tu.

Viongozi wetu na wachumi wetu waliwasoma akina Adam Smith kwenye THE WEALTH OF NATIONS kwa ajili ya kukariri kujibia mitihani tu!

Watu wetu hata wasomi wakubwa hawajui kutafsiri hata vitu basic kabisa!

Watu wanaambiwa kima cha chini la Mshahara kimeongezeka kwa asilimia 23.3% ,wao wanakimbilia Rais ameongeza Mishahara kwa asilimia 23.3% ( akili za Ki- Mwijaku Mwijaku)!

Jiulize kwanza kama Mishahara itaongezwa kwa asilimia 23.3% yote ,Wage Bill yetu itakuwa Shilingi ngapi?!

Wage Bill ikifika bilioni 900 kwa mwezi na madeni tunayolipa kwa mwezi ni bilioni 900 wakati Mapato yetu kwa mwezi Trilioni 1.5 ( bilioni 1500) Nchi itakwendaje?!

Ukitaka kujua Nchi hii ina tatizo kubwa katika Wealth Creation angalia utitiri wa tozo katika mafuta!

Kwahiyo ukifuatilia sasa mjadala ni asilimia 23.3% ya ongezeko la Mishahara ni kwa kima cha chini pekee au Mishahara yote!
Wewe ni mchawi!
 
Ukisoma vizuri kitabu cha WHY NATIONS FAIL ( The Origins of Power,Prosperity & Poverty) cha DARON ACEMOGLU na JAMES A.ROBINSON utajua kwa uhakika ni kwa nini Tanzania yetu ni masikini hivi na itachukua muda mrefu kubadili hali hii.

Kwa ufupi ni kwamba tunacho kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya maendeleo katika Nchi yetu kasoro watu wenye maarifa na taasisi imara.

Hata watu wachache wenye maarifa tulionao pia wana maarifa yaliyopitwa na wakati (obsolete) au waliyo karirishwa tu! Tunaweza kusema maarifa yao hayo ni USELESS KNOWLEDGE tu.

Nchi bila uzalishaji na kuingiza Nguvu kazi kubwa katika uzalishaji ili kuongeza tija ni kazi bure tu.

Viongozi wetu na wachumi wetu waliwasoma akina Adam Smith kwenye THE WEALTH OF NATIONS kwa ajili ya kukariri kujibia mitihani tu!

Watu wetu hata wasomi wakubwa hawajui kutafsiri hata vitu basic kabisa!

Watu wanaambiwa kima cha chini la Mshahara kimeongezeka kwa asilimia 23.3% ,wao wanakimbilia Rais ameongeza Mishahara kwa asilimia 23.3% ( akili za Ki- Mwijaku Mwijaku)!

Jiulize kwanza kama Mishahara itaongezwa kwa asilimia 23.3% yote ,Wage Bill yetu itakuwa Shilingi ngapi?!

Wage Bill ikifika bilioni 900 kwa mwezi na madeni tunayolipa kwa mwezi ni bilioni 900 wakati Mapato yetu kwa mwezi Trilioni 1.5 ( bilioni 1500) Nchi itakwendaje?!

Ukitaka kujua Nchi hii ina tatizo kubwa katika Wealth Creation angalia utitiri wa tozo katika mafuta!

Kwahiyo ukifuatilia sasa mjadala ni asilimia 23.3% ya ongezeko la Mishahara ni kwa kima cha chini pekee au Mishahara yote!
Kaka minimum wage ndio imepandishwa kwa hiyo asilimia 23.3. High earners watakuwa na asilimia ndogo sana. Kupandishwa mishahara ni haki ya mtumishi yeyote.
 
Ukisoma vizuri kitabu cha WHY NATIONS FAIL ( The Origins of Power,Prosperity & Poverty) cha DARON ACEMOGLU na JAMES A.ROBINSON utajua kwa uhakika ni kwa nini Tanzania yetu ni masikini hivi na itachukua muda mrefu kubadili hali hii.

Kwa ufupi ni kwamba tunacho kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya maendeleo katika Nchi yetu kasoro watu wenye maarifa na taasisi imara.

Hata watu wachache wenye maarifa tulionao pia wana maarifa yaliyopitwa na wakati (obsolete) au waliyo karirishwa tu! Tunaweza kusema maarifa yao hayo ni USELESS KNOWLEDGE tu.

Nchi bila uzalishaji na kuingiza Nguvu kazi kubwa katika uzalishaji ili kuongeza tija ni kazi bure tu.

Viongozi wetu na wachumi wetu waliwasoma akina Adam Smith kwenye THE WEALTH OF NATIONS kwa ajili ya kukariri kujibia mitihani tu!

Watu wetu hata wasomi wakubwa hawajui kutafsiri hata vitu basic kabisa!

Watu wanaambiwa kima cha chini la Mshahara kimeongezeka kwa asilimia 23.3% ,wao wanakimbilia Rais ameongeza Mishahara kwa asilimia 23.3% ( akili za Ki- Mwijaku Mwijaku)!

Jiulize kwanza kama Mishahara itaongezwa kwa asilimia 23.3% yote ,Wage Bill yetu itakuwa Shilingi ngapi?!

Wage Bill ikifika bilioni 900 kwa mwezi na madeni tunayolipa kwa mwezi ni bilioni 900 wakati Mapato yetu kwa mwezi Trilioni 1.5 ( bilioni 1500) Nchi itakwendaje?!

Ukitaka kujua Nchi hii ina tatizo kubwa katika Wealth Creation angalia utitiri wa tozo katika mafuta!

Kwahiyo ukifuatilia sasa mjadala ni asilimia 23.3% ya ongezeko la Mishahara ni kwa kima cha chini pekee au Mishahara yote!
We hamnazo kweli pia una chuki binafsi n watumishi, soma vzuri ile barua, wamesema mishahara imeongezwa kwa watumishi wa umma kwa 23.3% ikiwemo kima cha chini.Hapo anamaanisha ombi la tucta la milioni moja na elfu kumi limekataliwa kwahiyo Kila mtumishi basic yake atazidisha kwa 23.3 na kugawa kwa 100%.Pongezi kwa Rais wetu na sio yule Babu yenu.
 
Kwanini mmetoa ruzuku kwa wakulima ambao ndio wengi 70% ya Watanzania.

Mshaurini vizuri SSH kwenye vikao vyenu. Kukuza uchumi kwa kasi punguzeni kodi, ukiritimba, milolongo, biashara zitashamiri.
Mkuu yule aliyepita ambaye nafikiri ndio mnamuona alikuwa sahihi alishawahi kuwajali hao wakulima unakwasema hapa?

Lakini pia, unataka kuniambia kwa njia yoyote ile serikali inakosa/itakosa nyongeza ya Billion 130 kwa mwezi ya hii nyongeza ya mshahara? Kama bwana yule aliweza kilipa trillions ndani ya mwaka kwa ajili ya ndege tena Cash kwanini nyongeza ya mshahara kwa wafanyakazi inakuwa nongwa?

Au hii ni vita tu kwakuwa yule hakuongeza na mnaona kama legacy yake inachafuliwa??
 
Unazilipiaje? Wewe na wenzako kwenye serikali hii? Mtuambie. Ni rahisi sana kumuita mtu majina ukikosa majibu.

Hakuna binadamu , Mtanzania ambaye hapendi Watanzania wote wawe na maisha mazuri.

Mapato yanapungua, matumizi yanaongezeka.

Tuonyeshe hizi pesa zitatoka wapi, mikopo? Kodi zingine zaidi?
Zinalipwa kwa kuongeza ufanisi zaidi. Mshahara mkubwa ni motisha ya kazi, unapoongezwa muajiri anategemea ongezeko la tija kutoka kwa mwajiriwa.

Tunalalamika mno watanzania. JPM hakuongeza mshahara miaka yote sita na haiikumnyima usingizi hata kidogo. SSH ameamua kuongeza mshahara mnakuja na malalamiko mengine!.

Sio ajabu tutakwenda ndani ya makaburi tukiwa na malalamiko mengi tu.
 
Mkuu yule aliyepita ambaye nafikiri ndio mnamuona alikuwa sahihi alishawahi kuwajali hao wakulima unakwasema hapa?

Lakini pia, unataka kuniambia kwa njia yoyote ile serikali inakosa/itakosa nyongeza ya Billion 130 kwa mwezi ya hii nyongeza ya mshahara? Kama bwana yule aliweza kilipa trillions ndani ya mwaka kwa ajili ya ndege tena Cash kwanini nyongeza ya mshahara kwa wafanyakazi inakuwa nongwa?

Au hii ni vita tu kwakuwa yule hakuongeza na mnaona kama legacy yake inachafuliwa??

Vita gani tena. Vita iko Ukraine. Hapa tunachambua vitu kama watu huru.

Kuhusu wakulima hata JPM alikosea sana infact serikali zote toka awamu ya pili hazijawahi kumsaidia mkulima kwa dhati.

Nilimkosoa sana JPM kuhusu kilimo, kodi, mazingira ya biashara. Alikuwa vizuri sana kwenye miundombinu kama maji, umeme, barabara. Nidhamu serikalini, kuthibiti mfumuko wa bei, kwa hayo tulimpongeza.

130bn kwa mwezi kwa mwaka ni kiasi gani? 1.5Trillioni permanent imeongezwa ndani ya matumizi ya serikali. Kwanini usingeongeza kidogo kidogo, manageable sums of money say 5%, kila mwaka unaongeza uchumi ukikuwa unaongeza zaidi.

Kulikuwa na ulazima gani kuondoa ruzuku kwenye pembejeo, kuweka tozo mbalimbali?

Kwanini bwawa la umeme kasi imepungua ya kulimaliza,? Ingeleta tija, faida kubwa sana kwa taifa.

Faida hizo ni kama watu kujiajiri, viwanda kujengwa,unafuu mkubwa wa maisha kwa Watanzania wengi. SGR, maji,kodi,barabara, mazingira mazuri ya biashara elimu hivi vitu ndio vinaifungua nchi.
 
Kwanini mmetoa ruzuku kwa wakulima ambao ndio wengi 70% ya Watanzania.

Mshaurini vizuri SSH kwenye vikao vyenu. Kukuza uchumi kwa kasi punguzeni kodi, ukiritimba, milolongo, biashara zitashamiri.
Tukipunguza kodi hayo madaraja na shule hazitajengwa na mtakuja humu mkilalamika kwanini hazijengwi. Ruzuku ni suala la muda, linafanyiwa kazi.
 
Nibora hasinge ongeza mishaara mfumuko wabei utakuwa mkubwa Sana vitu vita panda bei mfano Kodi ya Nyumba chumba cha 50,000 kitapanda mpaka 60,000.
Wewe ni famba mno. Yaani wafanyakazi wa umma wasiongezwe. Watu wengine sijui mpo na akili na roho za namna gani. Haaaaaaaaaa....... wewe ni.mchawi haki ya Mungu
 
Msikilize na umtizame mmoja wa washiriki wa mchakato wa upandishwaji mishahara. Anaseme si kwa kila daraja watapata 23% japo mama samia amejitahidi sana kuanxia mwaka jana mambo ambayo ameyafanya kwenye vipato vya watumishi si madogo
Miaka yote benchmark ya mshahara ni kima cha chini. Then inakwenda kwa discending order hadi mshahara wa juu
 
Zinalipwa kwa kuongeza ufanisi zaidi. Mshahara mkubwa ni motisha ya kazi, unapoongezwa muajiri anategemea ongezeko la tija kutoka kwa mwajiriwa.

Tunalalamika mno watanzania. JPM hakuongeza mshahara miaka yote sita na haiikumnyima usingizi hata kidogo. SSH ameamua kuongeza mshahara mnakuja na malalamiko mengine!.

Sio ajabu tutakwenda ndani ya makaburi tukiwa na malalamiko mengi tu.

Unakosea kusema ni malalamiko. Ni vitu muhimu vinajadiliwa. Wananchi siku zote watajadili jinsi serikali yao inavyotumia pesa zao.

Utahoji hata wewe kama mke wako, mfanyakazi wako, mtoto wako anavyotumia pesa zako kama unaona vitu haviko sawa.

Tumewapa dhamana ya muda kutuangalia, kutujengea mazingira sahihi na sisi walalahoi tuinuke kusaidia familia zetu. Kama wewe na wenzako mnavyolamba asali. Mnasahau hata umeme, maji kwa kila familia ni haki yao, kama yako.

Tunawakumbusha
 
Tukipunguza kodi hayo madaraja na shule hazitajengwa na mtakuja humu mkilalamika kwanini hazijengwi. Ruzuku ni suala la muda, linafanyiwa kazi.
Steph Curry. Wakulima na watoto wao wanakufa sasa hivi hawawezi kumudu bei za pembejeo, kuzalisha mazao. kwanini uzitoe in the first place?

Kwanini msipunguze wizi huu CAG aliousema, kupunguza ufisadi, matumizi ya hovyo?

Mkifanya hivyo mtapata pesa nyingi kuweza kuwalipa wafanyakazi wote, kuondoa kodi zinazowaumizi watu wengi wa chini.

Mtapata pesa kulipia afya, elimu, miundombinu.

Kusema ni suala muda ni maneno ya kisiasa. Muda inaweza kuwa miaka 30. JPM alizipata hizi pesa kwa kuthibiti wahuni, mafisadi, rushwa ndani ya miezi michache. Alipambana nao. Fanyeni hivyo.
 
Unakosea kusema ni malalamiko. Ni vitu muhimu vinajadiliwa. Wananchi siku zote watajadili jinsi serikali yao inavyotumia pesa zao.

Utahoji hata wewe kama mke wako, mfanyakazi wako, mtoto wako anavyotumia pesa zako kama unaona vitu haviko sawa.

Tumewapa dhamana ya muda kutuangalia, kutujengea mazingira sahihi na sisi walalahoi tuinuke kusaidia familia zetu. Kama wewe na wenzako mnavyolamba asali. Mnasahau hata umeme, maji kwa kila familia ni haki yao, kama yako.

Tunawakumbusha
Mshahara ndio umeshaongezwa kwa wafanyakazi wa kima cha chini kama ilivyokuwa ikiombwa na wafanyakazi kwa serikali kwa kipindi cha miaka sita, haya mengine ni maongezi ya kufurahisha baraza.
 
Steph Curry. Wakulima na watoto wao wanakufa sasa hivi hawawezi kumudu bei za pembejeo, kuzalisha mazao. kwanini uzitoe in the first place?

Kwanini msipunguze wizi huu CAG aliousema, kupunguza ufisadi, matumizi ya hovyo?

Mkifanya hivyo mtapata pesa nyingi kuweza kuwalipa wafanyakazi wote, kuondoa kodi zinazowaumizi watu wengi wa chini.

Mtapata pesa kulipia afya, elimu, miundombinu.

Kusema ni suala muda ni maneno ya kisiasa. Muda inaweza kuwa miaka 30. JPM alizipata pesa kuthibiti wahuni, mafisadi, rushwa. Fanyeni hivyo.
Chochote kitakachofanywa na serikali wa kulalamika mtakuwepo na wa kupongezwa na kufurahia maamuzi watakuwepo pia. Hakuna wa kumfurahisha kila mtu.
 
Kwa ivyo unapambana na inflation ambayo chanzo chake mafuta kwa kuongeza mishahara.

Wakati wakandarasi washaanza kulalamika gharama za kutekeleza miradi zimeongeka kwa sababu ya kupanda kwa mafuta, hiyo inakwenda kuongeza gharama za serikali kwenye kulipia miradi.

Mishahara inaenda kuongeza gharama za admin costs za serikali.

Bei za bidhaa zimepanda maradufu kwenye kila kitu ongezeko la mishahara italeta unafuu kiasi lakini fall in government collection zitakuwepo tu ambazo unategemea kulipia hiyo nyongeza ya mishahara.

Kutokana na hiyo vicious circle ndio maana kila nchi duniani inapambana na bei ya mafuta kwa sababu ndio tatizo la msingi.

Hili sakata la kupambana na inflation mtu ambae kalitolea majibu mazuri ni Zitto nadhani ile ndio direction sahihi.

Hili la kuongeza mishahara ni kujichimbia shimo zaidi na kuacha agenda muhimu. Ufungui nchi kwa kuzurura bali unafungua nchi kwa kuweka easy access ya watu kuweza kuwekeza popote na accesss za kufikia masoko kirahisi au bandari kama ni for exportation.

Swala la uwekezaji wa miundombinu ni chungu lakini hakuna shortcut hakuna nchi duniani iliyokuwa bila ya kufungua access za sehemu mbalimbali nchini kwake; ukisoma historia ya US ni interconnection ya railway ndio iliyopaisha uchumi, ukienda UK canals na baadae railway na nchi nyingine nyingi ni mabarabara; hakuna uchumi unaokuwa bila ya interconnection ya kufikia masoko kirahisi.

Swala hapa kupanga ni kuchagua agenda yako ya kitaifa ya muda mrefu ni nini; sera za awamu ya tano zilikuwa za muda mrefu na maendeleo yanataka sacrifice.

Ni bora utumie tsh1 kupambana na inflation kwa ku stabilise bei ya mafuta which you know is a temporary measure kuliko ujiongezee full time commitments za tsh2 trillion kila mwaka wakati mapato yenyewe wasiwasi.
Unaongelea bei ya mafuta wakati yamepanda kama mwezi mmoja tu uliopita lakini kumbuka wafanyakazi wa se
We hamnazo kweli pia una chuki binafsi n watumishi, soma vzuri ile barua, wamesema mishahara imeongezwa kwa watumishi wa umma kwa 23.3% ikiwemo kima cha chini.Hapo anamaanisha ombi la tucta la milioni moja na elfu kumi limekataliwa kwahiyo Kila mtumishi basic yake atazidisha kwa 23.3 na kugawa kwa 100%.Pongezi kwa Rais wetu na sio yule Babu yenu.
You are wrong. Hiyo asilimia ni kwa mshahara wa kima cha chini. Asilimia itakuwa inapungua kadri mshahara unavyokuwa mkubwa.
 
Back
Top Bottom