Tanzania haitambui ushindi wa Mugabe - Membe

Unamaanisha yule mbwa ambae hata mkia unafichwa katikati ya miguu?

lol!

Anyway nimekuelewa, lakini tabia hii si nzuri hata kidogo kwani ina chembechembe za undumi la kuwili.

..nakuelewa. lakini,si ni ubinadamu kuwa ndumila kuwili?
 
Mimi niliangalia BBC wakati mkuu wa waanagalizi wa SADC anatangaza, sikujua watu kama wewe walioshika mkia wa mbuzi wataniuliza mk.. uko wapi.

http://news.bbc.co.uk/2/hi/africa/7480431.stm


Mkuu Nyangumi,
Ningekushauri tu kuwa BBC iwe sehemu yako ya mwisho kupatia habari za Zimbabwe hasa zinapokosekana mahali pengine popote.

Kisheria, kitu ambacho ndio pekeyake alichokitaka Mugabe, uchaguzi wa Zimbabwe umetimiza vipengele vyote vinavyotakiwa. Was it FREE, absolutely YES. Was it FAIR probably NOT. How was the elections in TZ, Uganda, Kenya, Ethiopia, Nigeria n.k.? FREE but not FAIR, and no one listened to the opositions. Why is Zim so special?. How on earth should Kikwete say Mugabe is not a president but Karume is?
 
..umenikumbusha enzi za mzee wa kiraracha,lyatonga.

..duniani wawili wawili.

Ni afadhali hata Mwalimu angemsikiliza Mzee wa Kiraracha na Si Mzee wa Kiraracha kumsikiliza Mwalimu!
Kitendo cha Mwalimu kumwita Mrema Mbwa na Kusema Mkapa ndiye binadamu kimetufikisha Utumwani!
 

Kwa maana hiyo unanambia niliyemuona anatangaza hakuwa mkuu wa usimamizi wa uchaguzi wa SADC bali alikuwa Tony Blair???

Mimi nina akili timamu za kutambua propaganda na ukweli, kilichotokea Zimbabwe ni ukweli tupui suala ni kuwa vilipewa kipaumbele saana katika TV yao.

Unaposema uchaguzi ulikuwa free unamaanisha nini? Mamilioni ya Wazimbabwe waliokimbilia SA na msituni na walichomwa moto matakoni na sehemu zingine za mwili hawakupata hiyo freedom unayoisema
 
..hivi uchaguzi ulio huru [mnauita free,eeh] ndio ukoje?

..kitila,mkjj,fmes,etc?
 
Duh! Tanzania tuna ubavu wa kutoitambua serikali iliyochaguliwa Zimbabwe, lakini tunawatambua watawala wa Zanzibar?

Yaani kweli tunayo hiyo moral authority ya kutotambua wengine? Halafu humu JF kuna wanaounga mkono haya? Mbona makubwa sana haya wakuu, ni kweli hatupendi sana yanayoendelea huko Zimbabwe, lakini sisi Tanzania tukae kimyaa kwanza tuachie wengine kama Botswana, Malwi au Zambia, maana ndio wenye ubavu na authority ya kusema haya, sisi tunyamaze tu as a nation.

Hatupendi huu unafiki wa hali ya juu sana tena ni aibuuu!kuanzia taifa letu mpaka sisi wote wananchi, Membe afute hiyo kauli mara moja!
 
Kama hili ni kweli basi wamrudishe nyumbani balozi wetu Zimbabwe na pia wamuombe wa Zimbabwe arudi kwao.
 
jukumu la wasimamizi wa uchaguzi ni kuangalia kama uchaguzi ni huru na wa haki kisha wanatoa tathmini yao kwa vyombo vilivyowatuma na/au dunia nzima. lakini tathmini hii yaweza kukubaliwa au kukataliwa na wale wanaopokea hiyo tathmini.

sasa kama wasimamizi wa uchaguzi wa sadc wangekuwa wametoa taarifa sadc na kuona uchaguzi haukuwa wa haki basi naamini sadc ingepata wakati mgumu kukataa tathmini ya watu waliowatuma. lakini hapa tunazungumzia au na nchi wanachama wa au wanaweza kutokukubaliana na tathmini ya wasimamizi wa sadc bila shida yoyote. na naamini hali hii ndio iliyotokea huko misri na kama ilivyosemwa huko juu au haikuwa na msimamo wa pamoja.

ni vyema kama hapo ukumbi wa maelezo ingeelezwa kwamba kutomtambua jongwe ni uamuzi wa tanzania pekee lakini hili la kuashiria kwamba huo ni uamuzi wa au! naamini hapo serikali imeteleza na ninaomba iwe waandishi ndio wamekosea kuandika kilichoelezwa.
 
Botswana troops mass on Zimbabwe border


Nakumbuka Robert Mugabe alilalamika kwenye mkutano wa SADC mwanzoni mwa 1990's kwa nini Botswana at that time walinunua vifaa vingi sana vya kijeshi pamoja na silaha nzito. 'Aliuliza wanataka kupigana na nani?... ... Naona amepata jibu down the line 18 yrs after.

Kama Bubu alivyosema kukata mzizi wa fitina Balozi arejeshwe mara moja na wamtimue balozi wa Zimbabwe hapo Dar sivyo waache longo longo.
 
Hivi Tanzania inawezaje kuona umuhimu wa serikali ya mpito na umoja wa kitaifa kwa Zimbabwe, bila kwanza kupractise ushauri huo kwenye mgogoro wa CUF na CCM Zanzibar?

Nyani haoni kundule.
 
Tanzania ikiingilia huu mgogoro kwa namna MAFISADI wanavyotaka sisi tufanye...Basi usishangae AFRIKA KUSINI WAKIJA HAPA KWA MBWEMBWE KAMA TULIVYOENDA UGANDA!
Wale waliofukuzwa kutoka huko ambao ni WAZIMBABWE ni wale ambao hawamtaki MUGABE na MBEKI hataki wengine waitumie SA kama staging ground for guerilla attacks!
On the other hand..Raia wengine wageni waliotolewa baruti huko Afrika Kusini ni WATANZANIA ambao kutokana na msimamo wao wa kumsapoti TSIVANGIRAI DHIDI YA MSIMAMO WA MBEKI KUMSAPOTI MUGABE..Umepelekea IMANI yao kuwatoka dhidi ya watanzania hao ambao sasa wanajulikana kama vibaraka wa mkoloni AFRIKA..MBAYA ZAIDI...HATA WANANCHI WENYEWE HAWAWATAKI TENA!
 
Kama hili ni kweli basi wamrudishe nyumbani balozi wetu Zimbabwe na pia wamuombe wa Zimbabwe arudi kwao.


sijui kama wakuu wamelitazama hili. unapokuwa humtambui rais wa nchi na serikali yake inamaana hatua ambayo inafuata ni kuvunja uhusiano wa kibalozi au "kumuita balozi wenu nyumbani kwa mashauriano." sasa kama ndio mmeishaitiana mabalozi wenu kwa mashauriano sijui huko sadc kutakaaje.
 

..we propaganda ulifundishwa na nani?
 

..haswaaa, tusubiri tuone!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…