Tetesi: Tanzania hatarini kuondolewa AFCON 2025 baada ya kukiuka kanuni za Shirikisho la Soka la Afrika (CAF)

Tetesi: Tanzania hatarini kuondolewa AFCON 2025 baada ya kukiuka kanuni za Shirikisho la Soka la Afrika (CAF)

Bila intelligence taifa huwangamia nakuwa kituko Rais kashatoa 700 mnafanyeje kufuta hili kituko uchawa unauwa Taifa
 
Ile million Mia saba iende kwa waliopata maafa na wananchi wanao hitaji misaada..

Haswaa kabisa basi ikalipie waliojifungua mahospitali ya serikali na kuzuiliwa kutoka hadi walipe bili.
 
Wakuu,

Mwandishi wa habari za michezo wa Ghana, Micky Jr ameripoti kuwa, Tanzania inaweza kuondolewa kushiriki michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 nchini Morocco licha ya kufuzu, baada ya kukiuka kanuni za Shirikisho la Soka la Afrika (CAF).

Pia, Soma:
Katika dakika ya 73 ya mechi yao ya kufuzu, Tanzania ilifanya mabadiliko na kumuingiza mchezaji aliyekuwa na jezi namba 26. Hata hivyo, kwenye orodha rasmi ya wachezaji iliyowasilishwa CAF kabla ya mechi, hakukuwa na mchezaji yeyote aliyekuwa ameambatanishwa na namba hiyo ya jezi.
Kwenye Media start list Ibrahim Mohamed Ame ambaye ndiye alivaa jezi namba 26 aliorodheshwa na namba 24, ambaye aliingia dakika ya 76 kuchukua nafasi ya Nahodha Mbwana Samatta.
yaani aliyefanya hii mistake ni mjinga sana
sasa huyu ni kit manager au?
 
hapo caf labda watumie ubinadamu tu wakienda kwenye sheria tunaliwa kichwa
 
Mtoa mada anavuja..., nikajua tumechezesha raia wa Ghana, au tumechezesha mcheza mieleka ambaye hakusajiliwa katika soka.. kumbe ni mchezaji wetu kabisa jezi namba tu ndo shida?
 
Wakuu,

Mwandishi wa habari za michezo wa Ghana, Micky Jr ameripoti kuwa, Tanzania inaweza kuondolewa kushiriki michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 nchini Morocco licha ya kufuzu, baada ya kukiuka kanuni za Shirikisho la Soka la Afrika (CAF).

Pia, Soma:
Katika dakika ya 73 ya mechi yao ya kufuzu, Tanzania ilifanya mabadiliko na kumuingiza mchezaji aliyekuwa na jezi namba 26. Hata hivyo, kwenye orodha rasmi ya wachezaji iliyowasilishwa CAF kabla ya mechi, hakukuwa na mchezaji yeyote aliyekuwa ameambatanishwa na namba hiyo ya jezi.
Kwenye Media start list Ibrahim Mohamed Ame ambaye ndiye alivaa jezi namba 26 aliorodheshwa na namba 24, ambaye aliingia dakika ya 76 kuchukua nafasi ya Nahodha Mbwana Samatta.
Hao wanataka kulalamika kwa vile Ghana imetolewa. Kanuni hiyo inakataza kutumia acheazji ambao ni "ineligible" yaani hawana sifa kwa maana ya kuwa siyo raia wa nchi husika au walizuiwa kucheza au wale ambao majina yao hayakupelekwa. Haisemi kuwa namba ya jezi atakayovaa itakuwa ni ipi. Wachezaji wote wanaoingia kama subs hukaguliwa uhalali wao na refa wa mezani ndipo anaruhusiwa kuingia uwanjani.
 
Taarifa hii ya TFF haijitoshelezi na haijibu hoja husika

Taarifa hiyo ilitakiwa ifafanunue huyo mchezaji aliyeingia sub alivaa jezi namba ngapi na ndiyo hiyo iliyowasilishwa kwa mamlaka husika kabla ya mechi?
Hawa TFF wajinga sana wanawaona wTZ hamnazo. Shida hapo ni jezi badala ya 24 aliyotakiwa kuvaa Ibrahim Ame amevalishwa jezi namba 26 ambayo haipo kabisa kwenye orodha siku hiyo.

Hii ina maana walichukua mtu toka jukwaani wakamwingiza kucheza uwanjani kwa jina la Ibra Ame.

Wasitufanye wajinga
 
Back
Top Bottom