Tanzania hatuna shule inayovaa sare ya aina hii. Acheni kuichafua na kuipaka matope Serikali yetu iliyojenga madarasa bora mpaka vijijini huko

Tanzania hatuna shule inayovaa sare ya aina hii. Acheni kuichafua na kuipaka matope Serikali yetu iliyojenga madarasa bora mpaka vijijini huko

Nikikuwekea picha mnato na picha mjongeo na ukasikia sauti watoto (wanafunzi), walimu na wazazi wakilalamika kuhusu shule kukosa miundombinu na vitendea kazi utakubali kuwa serikali inakusanya kodi lakini hairudishi hiyo kodi kwa wananchi hasa wa vijijini!!???
Sio kweli.Hata wewe na mwingine mnajukumu la kuchangia.
 
Kwa hiyo wewe hujiamini kuwa ni Mwanaume? Au ni mpaka ujitangaze kuwa wewe ni mwanaume kama matangazo ya waganga wa kienyeji mitaani? Kwani watu hawafahamu kuwa wewe ni mwanaume? Au huwa wanakwambia wewe ni mwanamke?
Ding angepizi out tuuu hii shida isingekuwepo.
 
Sio kweli.Hata wewe na mwingine mnajukumu la kuchangia.
Jukumu la kulipa kodi.
Jukumu la kuchangia sungusungu.
Jukumu la kuchangia takataka.
Jukumu la kuchangia ujenzi wa barabara.
Jukumu la kuchangia ujenzi wa zahanati.
Jukumu la kuchangia madawati.

Ninapolipa kodi,tozo na makato mbalimbali kwenye mauzo,manunuzi na shughuli zangu, hiyo hela inaenda fanya nini mpaka nipewe majukumu mengine hayo niliyoyaorodhesha!!?

Kila sehemu penye shughuli yangu ya kiuchumi, huwa natoa CSR, pamoja na kulipa kodi na tozo mbalimbali kulingana na shughuli husika.
 
Unaposema wajibu unamaanisha nini? Kwani Nchi ngapi zimeshindwa kutimiza wajibu wao? Kwanini usipongeze kwa kazi nzuri iliyofanywa na serikali yetu?
Kodi, kodi, kodi, kodi, tax payers,tax payers,tax payers, ndio wenye kustahili pongezi
 
Kukosoa na kupongeza vyote viende sambamba

Shida ni wewe, kazi yako wewe ni kupongeza tu na hukosowi

Kwa nini unawakasirikia wanaokosoa?

Wewe sitiki kwenye eneo lako la kupongeza, waache wanaookosoa nao waendelee
Mjinga huyo analazimisha wote tuwe machawa
 
Kwani Nchi ambazo wanafunzi wao wanakaa chini na kukosa madarasa na huduma zingine.Je wao hawakusanyi kodi? Tujifunze kupongeza pale serikali inapofanya vizuri.
Kwani serikali ni nini? Na kuna aina ngapi za serikali?
Pia usisahau biashara inayofanya serikali hata kupata ili ajifunze kuisifia.
 
Mjinga mmoja wewe Kuna Mhadhiri msaidizi wa chuo x alitembelea shule x Kwa ajili ya asesment ya wanafunzi wa field akapiga picha mazingira kikichomkuta ni historia. Na waliomganyia hayo ni watu wa aina Yako bumunda wewe Karne ya 21 unajisifia matundu ya choo yalojengwa Kwa msaada
Wewe ndiye useme ni ya Nchi gani,mkoa gani,wilaya gani,kata gani,kijiji au mtaa upi na jina la shule ni lipi . Na siyo kuweka vipicha vya mitandaoni
 
Mjinga mmoja wewe Kuna Mhadhiri msaidizi wa chuo x alitembelea shule x Kwa ajili ya asesment ya wanafunzi wa field akapiga picha mazingira kikichomkuta ni historia. Na waliomganyia hayo ni watu wa aina Yako bumunda wewe Karne ya 21 unajisifia matundu ya choo yalojengwa Kwa msaada
Jibu swali hili kama una akili Timamu. Ni shule ipi ya msingi ya serikali wanaovaa sare aina hiyo hapa Nchini Tanzania?
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kumekuwa na utamaduni na tabia ya baadhi ya watanzania wachache wenye wivu na chuki binafsi za kuchukua picha mitandaoni kutoka Nchi za nje ya Tanzania na kuziweka mtandaoni na kusema ni Tanzania.

Picha hizo zimekuwa ni zile zenye kuchafua Taswira nzuri ya maendeleo na mafanikio tuliyoyapata na kufikia kama Taifa. Imekuwa ni kawaida kuona mtu anachukua picha ya wanafunzi au kipande cha barabara kibovu na kisicho pitika kutoka nchi fulani barani Afrika Na kusema ni Tanzania.

Lengo likiwa ni kuichafua na kuipaka Matope serikali yetu na kuonyesha kuwa haifanyi kazi. Jambo ambalo siyo la kweli hata kidogo. Kwa kuwa Watanzania wote wanafahamu namna serikali ilivyofanya kazi kubwa ya kusogeza huduma za kijamii karibu kabisa ya Mwananchi zenye ubora wa kiwango cha juu.


View attachment 3233233

Kuna picha hiyo hapo juu watu wameiweka mtandaoni ikionyesha wanafunzi waliovalia sare nyekundu kwa upande wa sketi na suruali pamoja na shati jeupe na kusema kuwa ni Tanzania wakiwa wamekaa kwenye matofali na darasa bovu la miti na lililokandikwa kwa udongo huku likiwa linapitisha Maji Matupu chini . Jambo hilo ni la uongo kwa sababu hakuna sare ya aina hiyo inayotumika na kuvaliwa na wanafunzi katika shule za serikali kwa upande wa shule za Msingi.

Rai yangu ni kuwaasa na kuwataka watanzania kuacha tabia hiyo mbaya na isiyokubalika ya kuichafua na kuipaka Matope serikali yetu kwa chuki binafsi. Tuache kueneza upotoshaji na habari za uongo kwa malengo Binafsi. Tuendelee kuiunga Mkono serikali yetu na kushiriki katika shughuli za maendeleo pamoja na kulinda Miundombinu na miradi ambayo imekuwa ikijengwa kila kona ya Nchi yetu pasipo kumchangisha hata mia Mwananchi.

Embu Tazama hapa kama Sample Namna serikali yetu ilivyojenga shule kwa ubora na kuvutia Utafikiri ulaya pasipo kuomba michango kutoka kwa watanzania.

View attachment 3233120View attachment 3233121

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Swala la shule inaitwaje , wilaya gani na mkoa gani haliendani na kichwa Cha habari Cha Uzi wako bwana Lukas.
Sasa je kwa hizi picha nilizoleta hapa kwa rangi za sare zilizopo kwenye picha ke, hizo shule ziko Tanzania au ni nchi za nje?!
 

Attachments

  • wanafunzi darasani.JPG
    wanafunzi darasani.JPG
    25.9 KB · Views: 2
  • images(198).jpg
    images(198).jpg
    12 KB · Views: 1
  • images(195).jpg
    images(195).jpg
    58.3 KB · Views: 2
  • images(190).jpg
    images(190).jpg
    32.8 KB · Views: 2
  • images(187).jpg
    images(187).jpg
    8.9 KB · Views: 1
  • images(191).jpg
    images(191).jpg
    40.5 KB · Views: 1
Back
Top Bottom