Tanzania hatuna tabia ya kujichukia, tuache upotoshaji, bado tuko nyuma sana ukilinganisha na uwezo wetu(potential)

Tanzania hatuna tabia ya kujichukia, tuache upotoshaji, bado tuko nyuma sana ukilinganisha na uwezo wetu(potential)

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Kuna kijana kwenye mtandao wa kijami ameibua mjadala ambao nimeusikia na Clouds kwamba Tanzania kuna tabia iliyoota mizizi ya ya raia kujichukia sana(self-hate mentallity). Mifano yake aliyotoa sasa kwamba tuko vizuri ndio imenichekesha anazungumzia SGR, movie ya Idriss Sultan huko Netflix, miziki ya Diamond na mambo ya startups!

Hivi kweli sisi Tanzania ndio wa kujivunia hizi peanuts, yani Tanzania yenye rasilimali na jiografia tuliyo nayo leo baada ya miaka 60 ya uhuru ndio tujivunie hivi tuvitu?!

Tuache upotoshaji na uchawa usiotusaidia bali wenye kuzidi kutudumaza, bado tuko nyuma sana ukilinganisha na ukwasi wa rasilimali tulizo nazo, hali ya hewa na jiografia ya kikanda, tusifarijiane kwamba eti angalau tuna kidogo na wengine hawana, hiyo mitazamo ya Kiswahili itazidi kutudumaza.
 
Screenshot_20241105-082718_X.jpg
Screenshot_20241105-082732_X.jpg
 
mbona tunajipenda sana, labda anajichukia yeye, sisi tunachukia Madudu wanayofanya watanzania wenzetu kupitia nafasi tunazo wapa, kwa mfano Mchezaji yule yule ambaye ukiwakuta Yanga wanamsifia ndio huyo huyo anacheza Madudu kwenye mechi muhimu kwa taifa lake, Mchezaji huyo huyo ambaye akiwa simba ni kisiki, ndio huyo huyo anacheza fyongo kwenye timu yake ya taifa, huo uzembe tuupende?, wenzetu Africa hapa hapa na sio Ulaya wachezaji tunaowasifia kwenye ligi yetu wanafanya vizuri wakienda kwenye mataifa yao wanaonyesha kile ambacho wanakionyesha huku, tumekaa chini tukajua tatizo ni nini? ligi yetu inasifika kuwa bora, lakini timu ya taifa inastruggle hapo kulikoni???
 
Ni kweli hatuna mafanikio makubwa,

Lakini kujidharau tumezidi aisee

Watu wakiongelea kitu chochote cha wazungu lazima watasema 'huku bongo bado sana'
'huku tz labda miaka 100 ijayo'

Wanasema hivyo halafu hawafanyi chochote kubadilisha hali, wanajichimbia kaburi.

Wabongo wamekata tamaa.
 
Ni kweli hatuna mafanikio makubwa,

Lakini kujidharau tumezidi aisee

Watu wakiongelea kitu chochote cha wazungu lazima watasema 'huku bongo bado sana'
'huku tz labda miaka 100 ijayo'

Wanasema hivyo halafu hawafanyi chochote kubadilisha hali, wanajichimbia kaburi.

Wabongo wamekata tamaa.
Kuna kujidharau halafu kuna facts, ukweli ni kwamba kwa mwendo amabao tumekuwa tunaenda kwa muda mrefu itatuchukua hata miaka 100 kufikia walipo Ulaya ya leo, unaweza kuita hiyo ni kukutaa tamaa au kujichukia lakini huo ndio ukweli.
 
Kuna kujidharau halafu kuna facts, ukweli ni kwamba kwa mwendo amabao tumekuwa tunaenda kwa muda mrefu itatuchukua hata miaka 100 kufikia walipo Ulaya ya leo, unaweza kuita hiyo ni kukutaa tamaa au kujichukia lakini huo ndio ukweli.
Lakini mtu anayejichukia kila saa hayupo sawa

Tujichukie kistaarabu
 
Kuna shida ya exposure na ushamba kwa watu wetu wengi sana.
 
Back
Top Bottom