Tanzania idadi ya watu imeongezeka lakini hali sio nzuri mkoa wa Kilimanjaro

Tanzania idadi ya watu imeongezeka lakini hali sio nzuri mkoa wa Kilimanjaro

Watu wamehama ardhi nyingi ipo tupu, sema mambo yale yale ya ukale yanawarudisha nyuma, mimi kijijini kwetu majirani karibu 4 kati ya 6 wamehama na mashamba hayatumiki ila kuuza hawauzi wala kukodisha
Na akikodisha anatazama aliyekodi anafanyia nini akiona kinalipa mkataba ujao anapandisha dau la kodi ukikataa anakubalasa anasema hapangishi tena, rudi baada ya miezi kazaa unakuta anafanya shughuli ile ile ambayo alikuwa anafanya mtu aliyekodi shamba.
 
Hapana, ukichukulia kiwango cha wakazi waliohesabiwa kutoka mikoa mingine, hilo ongezeko ni very sustainable as wengi sana tumehesabiwa kutoka mikoa mingine kama Dar na Mwanza

Wakazi kama wakazi wanaweza kuwa wachache lakini wenyeji tutakuwa tumeongezeka sana.
Ishu inayozungumziwa hapa ni wakazi, kama wenyeji mkiwa wengi ila hamkai huo mkoa ni shida
 
Mkuu mbona Zanzibar ina watu 1.8 na uchumi upo vizuri mzunguko wa pesa ni mkubwa tu

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Ishu ni watu kupungua, ujue hata wangekuwa laki 5 ila wakawa hawapungui na nyumba kubaki tupu hapo haina shida, ila population inayopungua ina athari kiuchumi na kijamii
Mkoa mzima overall unaonyesha watu kuongezeka kwa laki 2 (hii imebebwa na Moshi mjini) ila ukichunguza wilaya moja moja watu wanapungua
 
Ukienda mkoa wa Kilimanjaro utashangaa mambo yafuatayo haya matatizo hayako tu uchagani bali hata upareni yapo

Idadi ndogo ya wanafunzi wanaoandikishwa darasa la kwanza, huku mikoa mingine wanafunzi wakiwa wengi na wengine wanakaa chini Hali ni tofauti mkoa wa Kilimanjaro idadi ya wanafunzi inazidi kushuka kila miaka inavyozidi kwenda Kuna shule inaandikisha darasa la kwanza wanafunzi 10, Kuna nyingine iliandikisha wa-nne sio tu vijijini hata mjini Kuna shule moja ipo manispaa ya Moshi mwalimu aliniambia wanastruggle sana kuandikisha wanafunzi wa darasa la kwanza

Nyumba nyingi kuwa empty hili ni tatizo lingine kubwa Kuna idadi kubwa sana ya nyumba hazina watu na ukienda vijijini Hali ndo mbaya Zaid nyumba nzuri nyingine gorofa Ila hazina watu na Hali inakua mbaya pale bibi na babu wakifariki sanasana utamkuta kijana mmoja tu ambaye Yuko kwa ajili ya kuziangalia, vijana kutoka Tanga hasa wasambaa, kutoka singida na manyara wambulu ndo utawakuta wanaangalia zile nyumba nyingi na kulimia migomba

Mfano ukienda upareni ni kawaida sana kuona nyumba imeachwa na kugeuka kuwa kichaka huku manyasi yakiwa yameota ndani huku nyumba ikiwa imebomoka bomoka

Vijiji mkoa wa Kilimanjaro havina watu kama umepanga kwenda kukaa week kwa Ile Hali ya vile vijiji vyao utajikuta umehairisha hakuna watu kabisa yaani in-short mkoa wa Kilimanjaro una ukiwa sio sawa na kipindi tunakua

Changamoto nyingine hakuna vijana Kuna kijiji nilienda kijiji kizima kijana ni mmoja ambaye ni bodaboda wengine waliobaki ni watu wa miaka 40 na kuendelea ni nadra sana kumuona kijana wa miaka 20's
Kila kitu kizuri kinawekezwa Dar Es Salaam.
Kazi, biashara, huduma za afya, elimu n.k.
Matokeo yake ndio hayo, mtu mwenye elimu yake kama haishi Dar, basi ni ughaibuni, na huko ndiko familia yake ilipo.
Wachaga walijenga shule nyingi, na walielimika wengi hata huko migombani, tatizo huko hakuna pa kuzitumia elimu yao, hivyo we go kama sio wote waliondoka. Sijui kama watarudi watakapostaafu au la.
 
Ishu inayozungumziwa hapa ni wakazi, kama wenyeji mkiwa wengi ila hamkai huo mkoa ni shida

Ishu inayozungumziwa hapa ni wakazi, kama wenyeji mkiwa wengi ila hamkai huo mkoa ni shida
Na ndicho nilichojibu lakini kwa mapana:

Wakazi - Kwa mujibu wa sensa 2022 bado wanaongezeka ingawa kwa kasi inayopungua tofauti na mtoa mada anayesema wakazi wamepungua sana kama si kwisha kabisa.

Ukijumlisha na sisi tunaoenda holiday season tu idadi inakuwa kubwa zaidi kuendelea ku sustain lively hood.
 
Nitazungumzia Wachaga tu.
Ukweli utabaki palepale sisi Wachaga ni miongoni mwa makabila machache yaliyo starabika na kujali asili yetu, mila zetu, wazee wetu vilevile ardhi ya nyumbani ni mali na urithi wa kizazi kilichopo na kijacho.

Ni kweli kabisa kuna nyumba hamna watu zaidi ya wazee na mashambaboy tu mfano mzuri ni nyumbani kwetu na hii ni kutokana na kila mtu kuajiriwa/kujiajiri sasa abaki nyumbani kufanya nini..?

Hizo nyumba ulizoona zimefungwa hazikai watu hebu rudi tena kuanzia tarehe 10 December ukakutane na wamiliki wake.
Maana kila mtoto wa kiume aliyeoa atapambana ajenge hata room mbili kwenye shamba lake ili akienda nyumbani kusalimia au kwenye shughuli ya ukoo/familia afikizie kwake na sio kwenye nyumba ya mzee.
 
Nitazungumzia Wachaga tu.
Ukweli utabaki palepale sisi Wachaga ni miongoni mwa makabila machache yaliyo starabika na kujali asili yetu, mila zetu, wazee wetu vilevile ardhi ya nyumbani ni mali na urithi wa kizazi kilichopo na kijacho.

Ni kweli kabisa kuna nyumba hamna watu zaidi ya wazee na mashambaboy tu mfano mzuri ni nyumbani kwetu na hii ni kutokana na kila mtu kuajiriwa/kujiajiri sasa abaki nyumbani kufanya nini..?

Hizo nyumba ulizoona zimefungwa hazikai watu hebu rudi tena kuanzia tarehe 10 December ukakutane na wamiliki wake.
Maana kila mtoto wa kiume aliyeoa atapambana ajenge hata room mbili kwenye shamba lake ili akienda nyumbani kusalimia au kwenye shughuli ya ukoo/familia afikizie kwake na sio kwenye nyumba ya mzee.
Huu utaratibu inabid uachwe hakuna haja ya kujenga nyumba nyingi huku ambazo zipo watu hawakai
 
Back
Top Bottom