Na akikodisha anatazama aliyekodi anafanyia nini akiona kinalipa mkataba ujao anapandisha dau la kodi ukikataa anakubalasa anasema hapangishi tena, rudi baada ya miezi kazaa unakuta anafanya shughuli ile ile ambayo alikuwa anafanya mtu aliyekodi shamba.Watu wamehama ardhi nyingi ipo tupu, sema mambo yale yale ya ukale yanawarudisha nyuma, mimi kijijini kwetu majirani karibu 4 kati ya 6 wamehama na mashamba hayatumiki ila kuuza hawauzi wala kukodisha
Siyo kweliMikoa mingine ambayo watu wanaongezeka, ukifanya utafiti wengi ni Wachaga.
Hahaha, Kilimanjaro banaKilimanjaro maisha ni magumu mnoooo. Ukitaka idadi kamili ya watu Kilimanjaro labda uwahesabu December au uhesabu NYUMBA. Maana NYUMBA zinajengwa halafu Hakuna watu.
Klm hakuna maisha?Watu wapo mikoani wanatafuta maisha
Ishu inayozungumziwa hapa ni wakazi, kama wenyeji mkiwa wengi ila hamkai huo mkoa ni shidaHapana, ukichukulia kiwango cha wakazi waliohesabiwa kutoka mikoa mingine, hilo ongezeko ni very sustainable as wengi sana tumehesabiwa kutoka mikoa mingine kama Dar na Mwanza
Wakazi kama wakazi wanaweza kuwa wachache lakini wenyeji tutakuwa tumeongezeka sana.
Ishu ni watu kupungua, ujue hata wangekuwa laki 5 ila wakawa hawapungui na nyumba kubaki tupu hapo haina shida, ila population inayopungua ina athari kiuchumi na kijamiiMkuu mbona Zanzibar ina watu 1.8 na uchumi upo vizuri mzunguko wa pesa ni mkubwa tu
Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Sawa issue mmepaacha ukiwa mkakimbilia mjini.Mkoa wa Kilimanjaro ndio wenye vijiji vilivyo endelea zaidi, nyumba bora, umeme, maji hata kipato, sio maneno yangu bali ni takwimu za serikali
YapoKlm hakuna maisha?
Kila kitu kizuri kinawekezwa Dar Es Salaam.Ukienda mkoa wa Kilimanjaro utashangaa mambo yafuatayo haya matatizo hayako tu uchagani bali hata upareni yapo
Idadi ndogo ya wanafunzi wanaoandikishwa darasa la kwanza, huku mikoa mingine wanafunzi wakiwa wengi na wengine wanakaa chini Hali ni tofauti mkoa wa Kilimanjaro idadi ya wanafunzi inazidi kushuka kila miaka inavyozidi kwenda Kuna shule inaandikisha darasa la kwanza wanafunzi 10, Kuna nyingine iliandikisha wa-nne sio tu vijijini hata mjini Kuna shule moja ipo manispaa ya Moshi mwalimu aliniambia wanastruggle sana kuandikisha wanafunzi wa darasa la kwanza
Nyumba nyingi kuwa empty hili ni tatizo lingine kubwa Kuna idadi kubwa sana ya nyumba hazina watu na ukienda vijijini Hali ndo mbaya Zaid nyumba nzuri nyingine gorofa Ila hazina watu na Hali inakua mbaya pale bibi na babu wakifariki sanasana utamkuta kijana mmoja tu ambaye Yuko kwa ajili ya kuziangalia, vijana kutoka Tanga hasa wasambaa, kutoka singida na manyara wambulu ndo utawakuta wanaangalia zile nyumba nyingi na kulimia migomba
Mfano ukienda upareni ni kawaida sana kuona nyumba imeachwa na kugeuka kuwa kichaka huku manyasi yakiwa yameota ndani huku nyumba ikiwa imebomoka bomoka
Vijiji mkoa wa Kilimanjaro havina watu kama umepanga kwenda kukaa week kwa Ile Hali ya vile vijiji vyao utajikuta umehairisha hakuna watu kabisa yaani in-short mkoa wa Kilimanjaro una ukiwa sio sawa na kipindi tunakua
Changamoto nyingine hakuna vijana Kuna kijiji nilienda kijiji kizima kijana ni mmoja ambaye ni bodaboda wengine waliobaki ni watu wa miaka 40 na kuendelea ni nadra sana kumuona kijana wa miaka 20's
Ishu inayozungumziwa hapa ni wakazi, kama wenyeji mkiwa wengi ila hamkai huo mkoa ni shida
Na ndicho nilichojibu lakini kwa mapana:Ishu inayozungumziwa hapa ni wakazi, kama wenyeji mkiwa wengi ila hamkai huo mkoa ni shida
Huu utaratibu inabid uachwe hakuna haja ya kujenga nyumba nyingi huku ambazo zipo watu hawakaiNitazungumzia Wachaga tu.
Ukweli utabaki palepale sisi Wachaga ni miongoni mwa makabila machache yaliyo starabika na kujali asili yetu, mila zetu, wazee wetu vilevile ardhi ya nyumbani ni mali na urithi wa kizazi kilichopo na kijacho.
Ni kweli kabisa kuna nyumba hamna watu zaidi ya wazee na mashambaboy tu mfano mzuri ni nyumbani kwetu na hii ni kutokana na kila mtu kuajiriwa/kujiajiri sasa abaki nyumbani kufanya nini..?
Hizo nyumba ulizoona zimefungwa hazikai watu hebu rudi tena kuanzia tarehe 10 December ukakutane na wamiliki wake.
Maana kila mtoto wa kiume aliyeoa atapambana ajenge hata room mbili kwenye shamba lake ili akienda nyumbani kusalimia au kwenye shughuli ya ukoo/familia afikizie kwake na sio kwenye nyumba ya mzee.