Tanzania iitake VOA kuomba Msamaha kwa habari yake ya Uzushi na Uongo

Tanzania iitake VOA kuomba Msamaha kwa habari yake ya Uzushi na Uongo

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Watanzania,

Haya ni maoni yangu mimi kama mimi kuiomba Serikali yetu kuiandikia barua VOA kupitia Ubalozi wa Marekani Nchini Tanzania kuiomba Msamaha nchi yetu, kwa habari yake ya kizushi, uongo, fitina, uchonganishi na yenye kuichafua serikali pamoja na Rais wetu.

Hii ni kwa kuwa kila mmoja anatambua kuwa habari iliyotolewa na VOA yaani Sauti ya Marekani ni ya uongo mkubwa sana, kwa kuwa mkataba uliosainiwa na Nchi yetu inahusisha mkopo wa masharti nafuu kabisa wa Dolla Billion 2.5. ambao utalipwa kwa muda wa miaka 40 na ambao riba yake ni 0.01% tu. Mkopo ambao utasaidia sana katika kuchochea kasi ya maendeleo na kuinua uchumi wetu kupitia miradi ambako pesa hizo zitawekezwa pamoja na kuzalisha fursa za maelfu ya ajira kwa vijana.

Ni Muhimu chombo hiki kiombe msamaha kwa propaganda zake chafu na zenye nia ovu ya kutaka kujenga taswira mbaya kwa serikali na Rais wetu. Ikumbukwe habari hii haijatolewa kwa bahati mbaya au kukosea, bali ni habari ambayo inalenga kuichonganisha serikali na wananchi pamoja na kutaka kumshushia heshima Rais wetu kwa watanzania ,hasa kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu na kutambua nguvu na Ushawishi mkubwa alionao Rais wetu kwa watanzania.

Hii ni baada ya kuona kuwa Marekani kwa sasa Inaendelea kupoteza nguvu na ushawishi wake iliokuwa nayo pamoja na kuendelea kubomoka kwa ule ufalme wake na U Mungu mtu wa kuabudiwa na mataifa mbalimbali.

Sasa mataifa mengi yanaikimbia Marekani ambayo mikopo yake wakati mwingine imekuwa na masharti Magumu ambayo yanakwenda kinyume na mila na utamaduni wetu. kwa wao kusema ni sehemu ya haki za binadamu na kwamba tuziheshimu haki hizo na kuzilinda na kuwalinda watu hao.

Napenda kuwakumbusheni tu watanzania wenzangu kuwa hakuna mkataba ambao serikali yetu imesaini unaoitoa sehemu au kipande chochote kile cha bahari yetu, wala hakuna mahali popote pale ambapo mkataba umesainiwa ambao Unayatoa madini yetu au Mgodi wetu na kuwakabidhi Korea kusini, hakuna mkataba huo na hakuna sehemu yoyote ile penye masharti ya aina hiyo wala makubaliano ya namna hiyo.

Hii ndio sababu hata hao wazushi na wachonganishi na wafitini wameshindwa kabisa kabisa kuweka na kuonyesha sehemu au mahali au kipengele chochote kile cha mkataba kinachozungumza habari hizo za Uzushi na ufitini wa kutoa bahari na madini yetu kama sehemu ya masharti ya kupata pesa hizo takribani Trilioni 6.5.

Tuendelee kuwa na Imani na serikali yetu pamoja na Rais wetu kipenzi. Tukumbuke ya kuwa mahasimu wetu pamoja na washirika wao wameumia sana kwa sisi kupata mkopo huo wa masharti nafuu kabisa na wenye tija kubwa sana kwa ustawi wa Taifa letu na maendeleo ya watanzania.

Kazi iendelee, Mama ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa. Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.

Soma:
- VoA: Tanzania imepokea mkopo kutoka kwa Korea Kusini na kutoa sehemu ya bahari na madini
 
Ukishashiba tu maparachichi, unaanzisha uzi kila baada ya dakika. Halafu maudhui yako unakuta ni yale yale. Kiufupi unazingua sana mdogo wangu ☹️
Wewe ni aina ya wale watu wasiojitambua na waliokosa uzalendo kwa Taifa letu na wanaopenda kushabikia na kushadadia habari za uongo,uzushi na uchonganisha.
 
Mwashambwa Katika ubora wako
Tuwe wazalendo na wakweli na tusikubali kamwe kushabikia uzushi na uongo wa mahasimu wetu na washirika wao wanaotaka kutuhujumu kwa maslahi yao binafsi na watu wao.
 
Sasa wewe upo huko kantalamba halafu unaandika utafikiri wewe ndiye ulikuwa mwandishi wa huo mkataba, kumbe wewe mwenyewe hata hiyo habari ya VOA umekuja kuishtukia hapa kijiweni, huo uchawa wako ni special edition.
Acha ujinga wako wa kushabikia uzushi na uongo.

Unaweza kuweka ushahidi wa uzushi na uongo uliotolewa na VOA? Au wewe unakaririshwa tu kama kasuku?

Au wewe unameza tu na kunyonya kila kitu unachosikia kama Dodoki?
 
Futa pale kwa maarekani, uzi wako uwe na mashiko, mbona huwa mnatumia mifano isiyo na uhalisia. Yaani unaandika thread kutamka hivi, ndani unaongeza ambiguity, hii ndio hupoteza maana ya thread. Maarekani lini kashuka kiutawala
 
Wewe LOFA usipende kushabikia UJINGA Kwa kitu ambacho hukijui.

Serikali yako hii ya kifala imekiri kuingia mikataba ya madini na Korea alafu wewe unakuja na upuuzi.
20240604_165740.jpg
 
Wewe LOFA usipende kushabikia UJINGA Kwa kitu ambacho hukijui...
Serikali yako hii ya kifala imekiri kuingia mikataba ya madini na Korea alafu wewe unakuja na upuuzi View attachment 3008346
Acha ujinga wako hapa.kwa hiyo hapo ni wapi waliposema na kuonyesha kuwa tunagawa madini yetu na migodi yetu kama karanga za kuonja. Unaelewa maana ya ushirikiano? Au umekurupuka tu huko.
 
Acha ujinga wako wa kushabikia uzushi na uongo . Unaweza kuweka ushahidi wa uzushi na uongo uliotolewa na VOA? Au wewe unakaririshwa tu kama kasuku? Au wewe unameza tu na kunyonya kila kitu unachosikia kama Dodoki?
Mimi si mjinga, mjinga ni wewe unayekariri kila kinachosemwa na mtawala, mwerevu huakiki kwanza, na mhakiki hana hakika, btw, nimekuwepo kipindi habari za kuuzwa kwa sehemu ya msitu wa loliondo zilipovuma, wahakiki tulisubiri, ila kama kawaida wakina Lucas Mwashambwa wa enzi hizo walikuwa mbogo!! Wakirusha maneno huko na huko kuwa mzee anasingiziwa,lakini mwisho historia ikatusha taji,, ulikuwa na miezi mingapi wakati wabunge walipokuwa wakibwatuka kama vichaa bungeni kuwa Wilbrod Slaa afunguliwe kesi ya uchochezi kwa kuibua madudu ya Richmond? Kama ulikuwa hujazaliwa(kiakili au kimwili) basi watafute waliokuwepo enzi hizo wakuelimishe kidogo, na uwaulize nani aliibuka mkweli kwenye sakata hilo, kwa hiyo nyie ma butt lickers mlikuwepo,na bado mpo tu,tumekuwa observers wa haya mambo long time back, NEVER say NEVER, kesho unaweza ukaaibika kama wengine ambao walilazimika kubadili ID zao hapa jf, time will tell.
 
Back
Top Bottom