Tanzania ili uitwe milionea unatakiwa kuwa na pesa kuanzia kiasi gani?

Tanzania ili uitwe milionea unatakiwa kuwa na pesa kuanzia kiasi gani?

Bro world standard money ni dola, kwasababu kibongobongo ukiwa milionea basi ata ukivuka kenya/nigeria/sa na nchi nyingi tuu apo amna kitu. Though hakuna kiwango wacha tufanye measurements za kidola
 
Hata siwasalimii maana salamu zenyewe za kwenye nyuzi sijawahi kuona zikijibiwa (joking)

Twende moja kwa moja kwenye mada! Swali langu ni hivi kibongobongo ili aitwe milionea anatakiwa awe na pesa kuanzia kiasi gani kiujumla?

Ninaposema kibongobongo namaanisha kulingana na standard yetu kwa kuzingatia uchumi wetu na thamani ya pesa yetu. Siyo kwa kulinganisha na thamani ya pesa za nchi nyingine.

Maana kwa mfano kwa Marekani wenyewe wanasema kwao ili mtu aitwe milionea anatakiwa awe na pesa au mali zenye thamani ya kuanzia Dola Milioni 30. Hizo ukizileta kwenye pesa yetu ya madafu ni takriban Shilingi Bilioni 69 na pumba.

Kwahiyo tukisema na sisi twende na standard hiyo basi tutajikuta asilimia 90 ya wabongo ni kina 'lakionea' na 'wananionea' tu! Kwa hivyo ningependa kujua kwetu sisi milionea anatakiwa awe na kuanzia kiasi gani cha pesa!

Na vile vile ili mtu awe katika position nzuri ya kuuelekea umilionea, kama ni mfanyabiashara anatakiwa awe anaingiza faida kiasi gani na kama ni muajiriwa anatakiwa awe analipwa mshahara kiasi gani ili awe kwenye nafasi nzuri ya kuutafuta umilionea?

Nawasilisha
Angalau uwe na uwezo wa kumiliki bilioni mbili na nus za kitanzania au dollar million mojs
 
Back
Top Bottom