Tanzania inahitaji Rais anayejiamini na mwenye uhakika wa Jambo lake na Maamuzi yake

Tanzania inahitaji Rais anayejiamini na mwenye uhakika wa Jambo lake na Maamuzi yake

Mtaanza sasa Kutulazimisha kuamini kuwa Watu wa Jinsia fulani si ' Competent ' kwa nafasi ya ' Head of State ' na akina GENTAMYCINE tukiamini hivyo msituchukie au msianze ' Kutubatiza ' Jina lenu la SUKUMA GANG mkimaanisha ni Wapinzani ' Tukuka ' wa Utawala huu wa Rais ( Mama ) Samia Suluhu Hassan.

Tanzania ya sasa inahitaji Rais ambaye haishii tu kuwa Mchapakazi bali pia mwenye uwezo wa Kufuatilia Jambo, Kusoma sana, Kujiridhisha na kuwa na Timu ya Wasaidizi ( Washauri ) wenye Akili hasa na siyo Wapumbavu wenye ' Uchawa ' mwingi.

Kibinadamu Tukio moja linasameheka kwani hata Mimi GENTAMYCINE na hata Wewe ' Member ' pia huwa tunakosea ila Mtu huyo huyo akilirudia tena Tukio ( Kosa ) hilo hilo anaanza kututia Mashaka na kuanza kutupa Mtihani mzito wa Kumjibia kutoka kwa wale wasiomkubali.

Nina mengi Moyoni na Rohoni ila kabla tu Hasira zangu hazijanipanda zaidi kwa Upuuzi unaoanza Kuzoeleka natoa Ushauri wa bure kwa wale Watanzania ambao watagombea Urais miaka ijayo GENTAMYCINE nawaombeni teueni Makamu wa Rais Vijana ( Damu Changa ) na pia wawe ' very intelligent ' ili hata ikitokea Mmekufa ( Mmefariki ) watakaotwaa Madaraka ' Kikatiba ' wawe ni Watu ambao hawatotupa Mashaka Mashaka katika Kuwaamini kama ninavyoanza kupata Mashaka hayo sasa.

Najua kwa Uzi huu leo nami nitabatizwa kuwa natokea SUKUMA GANG hivyo nikiitwa hivyo kwa kusema huu Ukweli wangu nitalipokea hilo Jina ila pamoja na kwamba Hayati Rais Dkt. Magufuli alikuwa na ' Mapungufu ' yake ila nilikuwa nikimpenda zaidi katika tabia yake ya kupenda Kujiridhisha, Kudadisi, Kufuatilia Jambo na kufanya Maamuzi ya uhakika ambayo huenda yakachelewa ila hayatotupa Mashaka na kuanza Kutusababishia tuwe na Maswali mengi.

Mlio karibu na Mheshimiwa Rais nanyi pia ni sehemu ya tatizo kwani hamumsaidii hadi Mama kila mara anatoa ' Maboko ' yake tu ya ' Kuteua Kutengua ' au yawezekana pia mkawa katika Mpango ' Maalum ' wa Kumpigisha Shoti ( Kumuhujumu Mama ) ili aharibikiwe na achekwe Yeye na tuchekwe pia Sisi wana CCM wote.

Mwisho namalizia kwa Mama ( Mheshimiwa Rais ) hebu punguza sana kuwa karibu kwa 99% na Rais Mstaafu Kikwete ( hasa Kiushauri ) kwani Kitendo hiki ' Kinawakera ' baadhi ya Watendaji wako ( tena Waandamizi kabisa ) na usipokuwa nacho makini kitakuja Kukugharimu na utakuja Kunikumbuka GENTAMYCINE niliyenyimwa Utajiri na Nguvu ila niliyepewa Fikra na Maono na Mwenyezi Mungu.

Sisemi usimsikilize Mzee Kikwete bali acha Kumfanya ndiyo kila Kitu Kwako Kiushauri bali Shirikisho pia na Watu ( Wastaafu ) wengine lakini pia Waamini na hao Watendaji wako ulionao sasa Serikalini kwani huenda na Wao wakawa na Mawazo Cbanya Kwako Kimaendeleo na Kiuongozi hata kuliko hayo unayoyapata kwa Mzee Kikwete.

Hii ' Teua Tengua ' iwe mwisho Mama!!!!
Maoni murua ila umeharibu unapotoa shutma pasi ya kutoa ushahidi usio na shaka kuwa Mama 'anategemea zaidi' ushauri kutoka kwa JK!!!, kwanini hutaki apewe ushauri kutoka kwake, ambaye ndiye immediate past president kabla ya Magu?
Kama una bifu na JK hilo ni lako na ufe nalo mwenyewe usiwakanganye wengine kwa kupandikiza fikra potofu.
 
dawa gani tena mambo yanaonekana utelebwe kabisa.

Mama ni binadamu. Kila binadamu ana mapungufu yake kama alivyokuwa mwendazake.

Linganisha wawili hao. Ole, bashiri, chaku, katelefoni bila ya kulisahau genge lile pendwa la kikabia wanayo habari ya dawa unayoiulizia.

Mama? Hakuna cha mtelebwe wala mterembwe. Mambo mdundo.

Wenye nchi tunasubiri ripoti ya CAG BOT na TPA kwa kuanzia.

Watakoma raia wa Sengerema
 
naona tunazidi kuongezeka kwa kasi tuliposema hakuna rais hpo ...mimi siku ya kwanza tu baada ya jiwe kufariki niliamini hatuna rais sema sheria zetu tu ndizo zilizotupelekea kufika hpa tulipo
Kwanza mama ni mvivu sidhani kama ana muda wa kusoma na kufuatilia, sioni tukipiga hatua za maana kutoka hapa tulipo, mimi niligundua kuna udhaifu mahali siku nyingi .
 
Uzi gani sasa akaze? Anahangaika tu na maisha

Waliokaziwa uzi wakisikia swali lako watajua unawacheza shere.

List yao hii hapa: "Ole, bashiri, chaku, nk na kundi lote la vibaraka wao." Kina Malyamungu wenyewe kwenye utawala wa Nduli Amini.

Mama kaweka wazi hataki kodi za dhuluma, anataka maridhiano, anataka ukaguzi wa wazi Jan - March 2021 BOT na TPA, anataka haki, na mengi kama hayo.

Hiyo ndiyo dawa yenyewe yakhe. Dawa hiyo ni chungu mno kwa vibaraka wote wakiwamo wasiojulikana na timu nzima ya lile genge letu pendwa la kikabila.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Ule usemi wa kutesa kwa zamu ndiyo huu sasa!! waliolia majuzi leo wanacheka, hakuna kusikitika haka ka mchezo huwa hakatakagi hasira ndugu zangu, Mama endelea ku Over-whole Engine yote - hiyo crankshaft inatakiwa kuchongwa size 25 ndiyo tuirudishie...

View attachment 1803566

Mbona sasa ndo anazidi kuharibu, ujambazi umeshamiri kila kona, nchi haieleweki, Mama mwenyewe haeleweki yupo yupo tu kama maiti
 
mbaya zaidi tunaambiwa kazi iendelea...[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]...bandugu kazi gani mnayoiona inaendelea...kinachoendelea ni upigaji na ujambazi ...kodi imeenda chini sana sijui tutasomeshaje tutegemee bakuli kuanza kutembeza

Ndo nashindwa eti kazi iendelee mxieew, to be honest nchi imeoza hata magufuli hana miez sita kaburini, tuseme yote ila magu alijua kuiweka Tanzania kwenye mstari, nchi ilikua na adabu, wachawi, majambazi wote walikua wanamuogopa, alikua tishia hadi kwa wazungu unadhan huyo ni mtu wa kawaida
 
Mbona sasa ndo anazidi kuharibu, ujambazi umeshamiri kila kona, nchi haieleweki, Mama mwenyewe haeleweki yupo yupo tu kama maiti
CCM ipo madarakani, kumsema mama ni sawa na kuisema CCM kwamba ni dhaifu.
 
Kwa hili ngoja nichangie leo;

Rais Samia anaonekana anasikiliza sana Ushauri wa Kikwete kwakua Kikwete ndiye Rais Mstaafu pakee aliyebakia na mshauri mwenye uzoefu wa nafasi hiyo.

Mzee Mwinyi Kwa umri wake sidhani kama yupo katika hali ya kuweza kumshauri lolote Rais Samia.

Ila Sasa pamoja na hayo inampasa kuchukua ushauri na kuchanganya na maamuzi yake mwenyewe ili huku mtaani iwe vigumu sisi raia kujua hayo maamuzi yake source yake ni wapi.

Ila kwa sasa ni rahisi kutrace the source kwani mambo yanaonekana na Kila mtu.

Ajitahidi sana kurekebisha hilo.

All the best kwake na team yake.
 
Kwanza mama ni mvivu sidhani kama ana muda wa kusoma na kufuatilia, sioni tukipiga hatua za maana kutoka hapa tulipo, mimi niligundua kuna udhaifu mahali siku nyingi .
La kuwa Mvivu nakubaliana nawe 100%.
 
Mama ni binadamu. Kila binadamu ana mapungufu yake kama alivyokuwa mwendazake.

Linganisha wawili hao. Ole, bashiri, chaku, katelefoni bila ya kulisahau genge lile pendwa la kikabia wanayo habari ya dawa unayoiulizia.

Mama? Hakuna cha mtelebwe wala mterembwe. Mambo mdundo.

Wenye nchi tunasubiri ripoti ya CAG BOT na TPA kwa kuanzia.

Watakoma raia wa Sengerema
Ok, vizuri ila hao raia wa sengerema imekuwaje?
 
Mtaanza sasa Kutulazimisha kuamini kuwa Watu wa Jinsia fulani si ' Competent ' kwa nafasi ya ' Head of State ' na akina GENTAMYCINE tukiamini hivyo msituchukie au msianze ' Kutubatiza ' Jina lenu la SUKUMA GANG mkimaanisha ni Wapinzani ' Tukuka ' wa Utawala huu wa Rais ( Mama ) Samia Suluhu Hassan.

Tanzania ya sasa inahitaji Rais ambaye haishii tu kuwa Mchapakazi bali pia mwenye uwezo wa Kufuatilia Jambo, Kusoma sana, Kujiridhisha na kuwa na Timu ya Wasaidizi ( Washauri ) wenye Akili hasa na siyo Wapumbavu wenye ' Uchawa ' mwingi.

Kibinadamu Tukio moja linasameheka kwani hata Mimi GENTAMYCINE na hata Wewe ' Member ' pia huwa tunakosea ila Mtu huyo huyo akilirudia tena Tukio ( Kosa ) hilo hilo anaanza kututia Mashaka na kuanza kutupa Mtihani mzito wa Kumjibia kutoka kwa wale wasiomkubali.

Nina mengi Moyoni na Rohoni ila kabla tu Hasira zangu hazijanipanda zaidi kwa Upuuzi unaoanza Kuzoeleka natoa Ushauri wa bure kwa wale Watanzania ambao watagombea Urais miaka ijayo GENTAMYCINE nawaombeni teueni Makamu wa Rais Vijana ( Damu Changa ) na pia wawe ' very intelligent ' ili hata ikitokea Mmekufa ( Mmefariki ) watakaotwaa Madaraka ' Kikatiba ' wawe ni Watu ambao hawatotupa Mashaka Mashaka katika Kuwaamini kama ninavyoanza kupata Mashaka hayo sasa.

Najua kwa Uzi huu leo nami nitabatizwa kuwa natokea SUKUMA GANG hivyo nikiitwa hivyo kwa kusema huu Ukweli wangu nitalipokea hilo Jina ila pamoja na kwamba Hayati Rais Dkt. Magufuli alikuwa na ' Mapungufu ' yake ila nilikuwa nikimpenda zaidi katika tabia yake ya kupenda Kujiridhisha, Kudadisi, Kufuatilia Jambo na kufanya Maamuzi ya uhakika ambayo huenda yakachelewa ila hayatotupa Mashaka na kuanza Kutusababishia tuwe na Maswali mengi.

Mlio karibu na Mheshimiwa Rais nanyi pia ni sehemu ya tatizo kwani hamumsaidii hadi Mama kila mara anatoa ' Maboko ' yake tu ya ' Kuteua Kutengua ' au yawezekana pia mkawa katika Mpango ' Maalum ' wa Kumpigisha Shoti ( Kumuhujumu Mama ) ili aharibikiwe na achekwe Yeye na tuchekwe pia Sisi wana CCM wote.

Mwisho namalizia kwa Mama ( Mheshimiwa Rais ) hebu punguza sana kuwa karibu kwa 99% na Rais Mstaafu Kikwete ( hasa Kiushauri ) kwani Kitendo hiki ' Kinawakera ' baadhi ya Watendaji wako ( tena Waandamizi kabisa ) na usipokuwa nacho makini kitakuja Kukugharimu na utakuja Kunikumbuka GENTAMYCINE niliyenyimwa Utajiri na Nguvu ila niliyepewa Fikra na Maono na Mwenyezi Mungu.

Sisemi usimsikilize Mzee Kikwete bali acha Kumfanya ndiyo kila Kitu Kwako Kiushauri bali Shirikisho pia na Watu ( Wastaafu ) wengine lakini pia Waamini na hao Watendaji wako ulionao sasa Serikalini kwani huenda na Wao wakawa na Mawazo Cbanya Kwako Kimaendeleo na Kiuongozi hata kuliko hayo unayoyapata kwa Mzee Kikwete.

Hii ' Teua Tengua ' iwe mwisho Mama!!!!
Ni hatari kwa nchi kumruhusu Kikwete kujaza hilo ombwe la uongozi kwani historia yake huko nyuma haikutukuka!
 
Back
Top Bottom