Tanzania inahitaji Rais anayejiamini na mwenye uhakika wa Jambo lake na Maamuzi yake

Tanzania inahitaji Rais anayejiamini na mwenye uhakika wa Jambo lake na Maamuzi yake

Mtaanza sasa Kutulazimisha kuamini kuwa Watu wa Jinsia fulani si ' Competent ' kwa nafasi ya ' Head of State ' na akina GENTAMYCINE tukiamini hivyo msituchukie au msianze ' Kutubatiza ' Jina lenu la SUKUMA GANG mkimaanisha ni Wapinzani ' Tukuka ' wa Utawala huu wa Rais ( Mama ) Samia Suluhu Hassan.

Tanzania ya sasa inahitaji Rais ambaye haishii tu kuwa Mchapakazi bali pia mwenye uwezo wa Kufuatilia Jambo, Kusoma sana, Kujiridhisha na kuwa na Timu ya Wasaidizi ( Washauri ) wenye Akili hasa na siyo Wapumbavu wenye ' Uchawa ' mwingi.

Kibinadamu Tukio moja linasameheka kwani hata Mimi GENTAMYCINE na hata Wewe ' Member ' pia huwa tunakosea ila Mtu huyo huyo akilirudia tena Tukio ( Kosa ) hilo hilo anaanza kututia Mashaka na kuanza kutupa Mtihani mzito wa Kumjibia kutoka kwa wale wasiomkubali.

Nina mengi Moyoni na Rohoni ila kabla tu Hasira zangu hazijanipanda zaidi kwa Upuuzi unaoanza Kuzoeleka natoa Ushauri wa bure kwa wale Watanzania ambao watagombea Urais miaka ijayo GENTAMYCINE nawaombeni teueni Makamu wa Rais Vijana ( Damu Changa ) na pia wawe ' very intelligent ' ili hata ikitokea Mmekufa ( Mmefariki ) watakaotwaa Madaraka ' Kikatiba ' wawe ni Watu ambao hawatotupa Mashaka Mashaka katika Kuwaamini kama ninavyoanza kupata Mashaka hayo sasa.

Najua kwa Uzi huu leo nami nitabatizwa kuwa natokea SUKUMA GANG hivyo nikiitwa hivyo kwa kusema huu Ukweli wangu nitalipokea hilo Jina ila pamoja na kwamba Hayati Rais Dkt. Magufuli alikuwa na ' Mapungufu ' yake ila nilikuwa nikimpenda zaidi katika tabia yake ya kupenda Kujiridhisha, Kudadisi, Kufuatilia Jambo na kufanya Maamuzi ya uhakika ambayo huenda yakachelewa ila hayatotupa Mashaka na kuanza Kutusababishia tuwe na Maswali mengi.

Mlio karibu na Mheshimiwa Rais nanyi pia ni sehemu ya tatizo kwani hamumsaidii hadi Mama kila mara anatoa ' Maboko ' yake tu ya ' Kuteua Kutengua ' au yawezekana pia mkawa katika Mpango ' Maalum ' wa Kumpigisha Shoti ( Kumuhujumu Mama ) ili aharibikiwe na achekwe Yeye na tuchekwe pia Sisi wana CCM wote.

Mwisho namalizia kwa Mama ( Mheshimiwa Rais ) hebu punguza sana kuwa karibu kwa 99% na Rais Mstaafu Kikwete ( hasa Kiushauri ) kwani Kitendo hiki ' Kinawakera ' baadhi ya Watendaji wako ( tena Waandamizi kabisa ) na usipokuwa nacho makini kitakuja Kukugharimu na utakuja Kunikumbuka GENTAMYCINE niliyenyimwa Utajiri na Nguvu ila niliyepewa Fikra na Maono na Mwenyezi Mungu.

Sisemi usimsikilize Mzee Kikwete bali acha Kumfanya ndiyo kila Kitu Kwako Kiushauri bali Shirikisho pia na Watu ( Wastaafu ) wengine lakini pia Waamini na hao Watendaji wako ulionao sasa Serikalini kwani huenda na Wao wakawa na Mawazo Cbanya Kwako Kimaendeleo na Kiuongozi hata kuliko hayo unayoyapata kwa Mzee Kikwete.

Hii ' Teua Tengua ' iwe mwisho Mama!!!!
najaribu kumfikiria M nakosa majibu anatuchezesha mfumo gani,kisera,utendaji,uteuzi. cjajua ni KIONGOZI WA AINA GANI?nabaki kusema Mambo yote yanaitaji maandalizi.RIP JPM
 
Angalau watu hawatekwi,watu wanapanda madaraja kazini na hajijengei uwanja wa ndege usio na tija kijijini kwake.....na angalau anawaondoa mapema na si kuwabakisha kwa jeuri kama Bashite ili tu kuwakomoa wanaompinga
Hayo mambo yashapita ndugu yangu mwendazake alishajiendea zake. Tujadili mambo ya nyakati hizi. Tanzania yupo Raisi mwingine lakini bado viatu alivyovaa ni vikubwa havimtoshi .
 
Samia akijisimamia tutapata Rais bora sana lakini ni hatari hii staili ya maelekezo kwa remote straight from Msoga. Mbaya zaidi ndio rumours zinazosambaa hadi kwa wananchi wa kawaida na hata "waandamizi" wanajipendekeza Msoga zaidi maana ni kama version ya 2010- 2014 imerejea.
 
..hapo inatakiwa WABUNGE wawe na nia na uwezo wa kumdhibiti.

..bahati mbaya yeye ni mwenyekiti wa chama, na amiri jeshi mkuu.

.
Uwezo wa kumdhibiti wanao kikatiba, labda nia ndio hawana ukichanganya na huo uenyekiti wake.

Kwa muono wangu, urais ni wadhifa ulio juu sana ya uwezo wake.
 
Samia akijisimamia tutapata Rais bora sana lakini ni hatari hii staili ya maelekezo kwa remote straight from Msoga. Mbaya zaidi ndio rumours zinazosambaa hadi kwa wananchi wa kawaida na hata "waandamizi" wanajipendekeza Msoga zaidi maana ni kama version ya 2010- 2014 imerejea.
Msoga mtambebesha lawama asizostahili. Tatizo ni uwezo mdogo wa rais mwenyewe.

Kuongoza taifa ni tofauti sana na kuongoza NGO. Kuna mtu kaniambia huyu mama alikuwa karani masjala huko nyuma.
 
Uwezo wa kumdhibiti wanao kikatiba, labda nia ndio hawana ukichanganya na huo uenyekiti wake.

Kwa muono wangu, urais ni wadhifa ulio juu sana ya uwezo wake.

..inawezekana kinadharia.

..lakini ukija kufanya kwa vitendo haiwezekani.

..mbunge wa ccm akileta fyoko-fyoko anaweza kufukuzwa toka kwenye chama na mwenyekiti.

..vilevile kwasababu mwenyekiti ni amiri jeshi mkuu anaweza kutumia vyombo vyake kumdhibiti mbunge / mwanachama mkorofi.

..nadhani unakumbuka tukio la Bashe na Musukuma kukamatwa wakati wa kikao cha CCM.

..ni vigumu sana kujinasua kutoka kwenye " utando " wa ccm, serikali, na vyombo vya dola. Kuna faida kwa CCM kwasababu inawahakikishia ushindi " tutake tusitake." Lakini hasara zake ni kwamba ni mfumo unaofuga uzembe, ufisadi, ukatili, etc etc.
 
Mleta mada nikuulize yule Mkuu wa wilaya aliyeteuliwa enzi za mwandazake akafika hadi ukumbini kwa ajili ya kula kiapo na muda mfupi akatolewa kwamba sio yeye je ulimwanzishia uzi? Au umeona kuwa sasa uko huru hata kutaja majina ya watu humu jukwaani tena kwa kijinasibu kuwa unajiamini? Leta hiyo thread humu nijue una msimamao tangu mwanzo.
Uyo mlete mada ni kahaba fulani asiejielewa
 
Msoga mtambebesha lawama asizostahili. Tatizo ni uwezo mdogo wa rais mwenyewe.

Kuongoza taifa ni tofauti sana na kuongoza NGO. Kuna mtu kaniambia huyu mama alikuwa karani masjala huko nyuma.
Mwambie basha wako basi aje tumpe nchi
 
Kwa muono wangu, urais ni wadhifa ulio juu sana ya uwezo wake.

..nadhani it is up to her kufanya vizuri au kufanya vibaya.

..anachotakiwa ni kutafuta wasaidizi very competent kwenye key ministries wamsaidie kuongoza nchi.

..aupukane na kishawishi cha kutaka kufanya mambo mengi makubwa kwa wakati mmoja.

..zaidi, asijaribu kujifanya anajua kila kitu.
 
...
Tanzania ya sasa inahitaji Rais ambaye haishii tu kuwa Mchapakazi bali pia mwenye uwezo wa Kufuatilia Jambo, Kusoma sana, Kujiridhisha na kuwa na Timu ya Wasaidizi ( Washauri ) wenye Akili hasa na siyo Wapumbavu wenye ' Uchawa ' mwingi.
...
Hii ' Teua Tengua ' iwe mwisho Mama!!!!
Mkuu GENTAMYCINE kinachoendelea kwa sasa, kiutawala, nchini kinafikirisha. Kuna wakati nilitakata kuweka bandiko kuhusu UTASHI WA KISIASA na MAAMUZI MAGUMU. Kwa nini sikufanya hivyo, bado najiuliza. Ila lililo kichwani mwangu bado naendelea kupokea na kuchambua yanayojiri katika utawala wa sasa, kama hilo la TEUZI nk.

Sifa/uwezo wa Mwanasiasa kuamua na kufanya mambo ambayo yataleta matokeo yatakayotakiwa, yamo katika misingi ifuatayo:
1. kuweka ‘utashi wa kisiasa’ ndani ya sehemu nyingine za mfumo fulani wa kisiasa.
2. Mwanasiasa lazima awe na angalau maono fulani – uwezo wa kufanya hivyo akitambua na kubainisha jinsi mambo yanavyoweza kuwa tofauti kutokana na maamuzi yake binafsi.
3. Sifa hizo ziwe ni za mwanasiasa binafsi si kwa pamoja - maamuzi magumu binafsi yenye maslahi mapana kitaifa.
 
Kwa maoni yangu nadhani ni kuwa rais ameanza kwa kupanga na kupangua kikosi kazi kwaajili ya kuendana na misimamo yake.

Yani ni kama kocha mpya akichukua team lazima kuna panga pangua huwa zinatokea kwenye kikosi ikiwamo na sajili mpya na kutemwa baadhi ya wachezaji ili kocha abaki na wale ambao wata fit kwenye mfumo wake.

Baada ya siku 100 madarakani kama hizi panga pangua hazijaisha basi nami nitakuunga mkono mleta mada.

Mada yako ina hoja nzito lakini.
Siku 100 zina uhusiano gani na umakini wa mtu? Mbona tunapenda kujiliwaza hata katika mambo yaliyo wazi? Tulishasema toka awali kuwa huyu hana uwezo! Anapenda kusoma kwenye Press kuwa Raisi wa JMT amefanya uteuzi wa fulani fulani kuwa fulani na kisha kukimbilia kwenye mitandao kuona comments. Ni Raisi mtaka misifa.
 
Mkuu naunga mkono hoja. Kwenye para ya 7 mimi nadhani mama amteue/kupata ushauri kutoka kwa Mzee Warioba kuhusu rasmu yetu (wanainchi) ya KATIBA ili mambo yaendelee.
 
Ndugu,
Rais wa sasa, angekuwa alibahatika kujua kabla hata kwa mwezi kuwa uhai wa Jiwe u karibu kukatika, angeweza kujipanga na kuja na orodha kamili za teuzi kwa ngazi zote kama alivyotamani.
Kwa hakika mpaka sasa anafanya vizuri na mabadiliko/marekebisho ayafanyayo BAADA ya muda mfupi ni kielelezo cha uangalifu mkubwa aliyonao, ili madosari ya uongozi aliyoyaona kwa mtangulizi wake, yaachwe hukohuko. Ni kweli kuwa, kuna baadhi ya mambo/vitu vizuri vinaweza hata kuja kuyumba, lakini hizo ndio gharama za mabadiliko ambazo yaweza kuwa sio rahisi sana kuziepuka.
Kutoka kwenye aina ya uongozi wa Mwendazake, ambako Mungu wa haki mwenye huruma ametuepusha na ili kukwepa kuendeleza kufanya makosa yaleyale dhidi ya binadamu wengine, hata kama itachukua siku zaidi ya hizo mia, nitaendelea kuunga mkono nia yake NJEMA ya kulitibu taifa letu, lililokuwa limekwishaacha mwenendo mwema wa kutoa UHURU NA HAKI kwa watz.
Ninaomba kwa Mungu azidi kuwaongoza wazalendo wa kweli, tusichoke kumuunga mkono kwenye HILI. Na pia tusije Tukakubali KUTAMANISHWA kwa lugha yoyote ile kurudi kwenye ule udhalimu.
AMEN
Kwa maoni yangu nadhani ni kuwa rais ameanza kwa kupanga na kupangua kikosi kazi kwaajili ya kuendana na misimamo yake.

Yani ni kama kocha mpya akichukua team lazima kuna panga pangua huwa zinatokea kwenye kikosi ikiwamo na sajili mpya na kutemwa baadhi ya wachezaji ili kocha abaki na wale ambao wata fit kwenye mfumo wake.

Baada ya siku 100 madarakani kama hizi panga pangua hazijaisha basi nami nitakuunga mkono mleta mada.

Mada yako ina hoja nzito lakini.
 
Back
Top Bottom