Tanzania kinara wa Utalii Afrika 2022

And Yet tunakabana mitaani na Tozo za Miamala na watu kukosa Mikopo ya Elimu ?

Kweli something is not right somewhere....
 



Nawashauri kwenye matangazo ya utalii msiweke siasa. Mfano The Bahamas ambayo ina watu 393,248 tu wanapata watalii Milion 5 kwa mwaka. Hii ina maana Zanzibar peke yake wangeweza kupata watalii wengi hivi. Nilimuuliza mfanyabiashara mmoja wa kule akasema wenyewe kinachowasaidia wanatangaza vivutio na sio siasa wa viongozi. Ukienda kwenye maonyesho yetu sisi tumejaza picha za wanasiasa ambao watalii hata hawajali na wanafikiri ni zile nchi kama North Korea. Badala ya propoganda pekee tunawapa mawazo halisi ya kufanyia kazi


Msikilize huyu mchungaji wa The Bahamas late Dr Munroe



Sisi badala ya kuweka vyakula, utamaduni, .... tunaweka picha za watu

 
Nakubaliana na wewe 100% lazima tuwe serious Utalii unatuvusha,
 
..Ni jambo zuri sana kupata tuzo hii.

..sasa tujiulize ni Watz wangapi wanaweza kutembelea vivutio vya utalii hapa nchini?

..Watz wangapi wanatembelea mbuga ya Serengeti kila mwaka?

..Au tunafikiri wanaostahili kufanya utalii ni watu wa nje peke yao?

..Tuchukulie mfano wa Disney World huko Florida, Marekani. Eneo hilo la utalii inapokea watalii zaidi ya 10 million kila mwaka.

..Na wengi wanaotembelea Disney World no raia wa Marekani. Mimi sijamsikia balozi wa Marekani hapa Tz akitushawishi tutembelee Disney World.

..Disney World inapata mamilioni ya watalii kwasababu wamejitangaza na kuji-brand kwa namna ambayo karibia kila mtoto wa Kimarekani ana NDOTO ya kwenda Disney kumuona Mickey Mouse.

..Turudi hapa Tanzania, Je, ni familia ngapi zina ndoto ya kwenda ktk mbuga za Serengeti, Udzungwa, Ruaha, etc? Watz wangapi wana ndoto ya kupanda mlima Kilimanjaro? Wana ndoa wangapi wanatamani kusherehekea honeymoon Zanzibar, Bagamoyo, au ktk fukwe zetu?

..Nadhani tunatakiwa tubadilike na kuangalia watalii wa ndani. Jinsi gani tunajenga utamaduni wa Watz kutembelea vivutio vya utalii hapa nchini.

..Mwisho, Tanzania ni nchi kubwa na yenye watu wengi. Hatuwezi kutoka kwa kutegemea utalii. Ili tufike kule tunakotaka ni lazima tumuinue MKULIMA.

CC Nguruvi3, Chige, Kamundu
 
Haya madini sitii neno ila natamani kila mmoja apite hapa,
 
Mkuu JokaKuu,

Yaani wakati naanza kusoma hoja zako, nami nilitaka kutumia mfano sawa na huo lakini reference yangu ilitaka kuwa Universal Orlando, huko huko Florida!!

Na hata hiyo Disney World uliyoitumia kama reference, tukisema zaidi ya 10 Million, watu wanaweza kuweka approx ya labda 12M, 15M or anything like that lakini pale ni sahihi kabisa tukisema zaidi ya 30M, na kama ulivyosema, asilimia kubwa ya wanaotembelea huko ni Wamarekani wenyewe!!

Linapokuja suala la Domestic Tourism Africa tunafeli sana lakini kwa bahati, tatizo la corona limeonesha ni kwanini kwa miaka kadhaa sasa watu wamekuwa wakisisitiza sana suala la domestic tourism kwa sababu huu ndio utalii pekee unaoweza kuwa stable!

Lakini usishangae kukuta majority ya Wakazi wa wilaya ya Serengeti hawajawahi kutembelea Hifadhi ya Serengeti kwa maana ya kufanya utalii!
 
Haya madini sitii neno ila natamani kila mmoja apite hapa,



..asante. Niliamua kuwa modest kwenye hizo data kwasababu sikuwa nimefanya research ya uhakika.

..hiki tunachojaribu kushauri nj kazi nzito ambayo inatakiwa kufanywa kwa muda mrefu.

..ugumu unakuja kwamba Watz tunapenda matokeo ya chap-chap. Tunapenda kujenga choo miezi miwili wananchi wanakuwa wanaona matokeo. Mipango yetu sio ya muda mrefu.

..Nashukuru umeniunga mkono ktk hoja hii. Kwamba inabidi tubadilike KIUTAMADUNI ili Watz wenyewe tuanze kufanya utalii.

..Kwa mfano, wasichana wangapi wa kizungu wanatamanj kuvishwa pete ya uchumba Eiffel Tower?

..Sasa rudi hapa Tanzania, ktk mwaka mmoja ndoa ngapi zinajengwa? Wasichana wangapi wa Kitanzania wanatamani kivikwa pete ya uchumba ktk fukwe za bahari mfano Zanzibar, Bagamoyo, Tanga?

..Again, asante kwa mchango wako,na kunipa " sapota " ktk hoja hii.
 
Yaani tunahitaji Mabadiliko Makubwa sana ya kifikra! Kuna wakati nilimuona Kigwangwala akivalia njuga hili suala, and I was very pleased lakini kama ilivyo kawaida yetu, nasikia ile kampeni ikageuka kuwa kichaka cha ufisadi.

Na upo sawa kabisa... hili ni suala linalojitaji kuwekewa mikakati ya muda mrefu ili hatimae watu wafahamu kwamba Utalii isn't just for Wazungu lakini wenyewe ndo soko la awali kwa sababu hata hao Wazungu wana misimu yao ya kutalii.

Yaani huwezi amini... moja ya tukio ambalo hadi kesho najilaumu ilitokea Zanzibar ambako nilikutana na rafiki yangu ambae by the time alikuwa kwenye hospitality industry! Basi weekend moja akanifuata nilikofikia kunipa offer tukafe sea tour na zile zinaitwa Glass Bottom Boat Tour.

Binafsi, sio mwoga wa bahari hata kidogo lakini cha ajabu nikakataa, halafu jamaa aliumia sana!! Na hakuna adventture mzuri unayoweza kukutana na sea tours zaidi ya hii ya kutumia hizi glass bottom boats!

Now imagine! People pay money kufanya tour na zile boat, mimi nimepewa free offer lakini bado nikakataa!! Hadi akili zinanirudia kwamba hivi naanzaje kukataa kitu kama hiki, ilishakuwa too late!

Hapo ndipo utakapogundua ni namna gani tusipolipa kipaumbele suala la utalii kwetu wenyewe!
 
..sasa tujiulize ni Watz wangapi wanaweza kutembelea vivutio vya utalii hapa nchini?
..Watz wangapi wanatembelea mbuga ya Serengeti kila mwaka?
..Au tunafikiri wanaostahili kufanya utalii ni watu wa nje peke yao?
Mkuu wew ni mkongwe hapa, utakumbuka tulishauri Waziri wa Utalii wakati huo Kigwangala kuhusu 'domestic tourism'. Tulikumbusha, baada ya uhuru kulikuwa na program za wanafunzi wa vyuo na shule kutembelea mbuga na vivutio mbali mbali vya ndani ili kujenga utamaduni wa utalii.
Jambo hilo lilifanywa kwa kutoa upendeleo kwa 'watalii wa ndani'' katika gharama

Utalii wa ndani unasaidia nyakati utalii wa kutoka nje unakuwa mdogo '' off peak season'.
Pili, unaongezaufahamu kwa wananchi kuitangaza nchi kwasababu wanakutana na kuzungumza na watu wengine

Mombasa ni destination kubwa ya watalii wa East and Central Africa kwanini kusiwe Tanzania!
Hata South Africa utalii wa ndani ni mkubwa zaidi kutuzidi

Kuna njia nyingi na siyo zile za ajabu ajabu za kuwekeza milioni 600 kwa matanganzo katika mabasi ya East London. Wekeza ndani ili wananchi washiriki 'kuinadi nchi yao'

1. Punguza gharama za watalii wa ndani
2. Tengeneza program za kuvutia kama vile za ' fungate'' katika kutangaza utalii
3. Toa tax incentives kwa watakao safarisha au ku-rent watalii katika Hotel zenye vivutio
4. Tengeneza vitu zaidi ya mbuga za Wanyama na Beach. Hivi Dar kuna kitu gani ukiachilia Bar?
Kule Coast Mombasa kuna Hoteli ndani ya majahazi kwenda ndani ya bahari kubarizi
5. Tazama miji yote duniani ina alama '' landmark' tujiulize Tanzania ni mikoa mingapi ina kitu kama London Bridge, Eifel Tower , Opera House, CN Tower , Collessum, Disney, n.k.
Maeneo hayo hutembelewa na kuongeza utalii wa ndani

White House au 10 Downing street ni maeneo ya utalii. Watu kutoka mbali wanakwenda kuangalia ''changing of guard '' ambayo ni gwaride tu pale Downing street

Sisi Tumeweka uzio na kuziba barabara za Ikulu! Yaani hofu imetawala kuliko huko kwingine

Ikulu ni sehemu ya utalii wa ndani! kwanini kuna uzio mkubwaaaa ! ulinzi ni Technology tu

Tuna matatizo ya kufikiri, walioko katika bodi za utalii ''wanakula urefu wa kamba''
Exactly! Yaani hapo honeymoon palikuwa pazuri sana. Kwa mfano ''ofa' kwa wanandoa ya fungate siku 2 au 3 ni investment kwasababu wanandoa hao wakijaliwa familia watarudi na itakuwa ni mzunguko wa kudumu katika Familia. Nani anaona vitu vidogo kama hivi?

Tunashindwa kubuni vitu rahisi sana vyenye maana. Treni zipo kwanini hatuna za utalii hadi tusubiri ile ya ''Vos' kutoka South Africa?

Treni ni sehemu ya utalii wa kwenda Serngeti, Mikumi , Tarangire n.k.

Kuna program moja niliona India wana Treni inayokwenda siku 7 ikisimama katika miji na watu kuangalia vivutio ikiwemo ''Temple lenye panya' na watu wanashangaa na kufurahia

Australia kuna India-Pacific Train si kwa wageni bali watu wa ndani.

Leo mtu akitoka Dar utamuuliza alifika eneo gani? Hakuna!
Arusha japo mtu atasema Mnara wa Azimio. Mwanza je?

Juzi balozi wa US alikuwa Arusha kwa Mrombo anakula nyama choma! hivi hata ku promote vitu vidogo kama hivi hatuwezi. Mikumi na Selous zipo karibu hatuwezi kuwa na ''Carnivore' kama Nairobi.

Tunashindwa kufikiri vitu vidogo sana tunasubiri ' Documentary ya Rais''
Hata jengo moja tu la kuvutia hakuna!


..Nadhani tunatakiwa tubadilike na kuangalia watalii wa ndani. Jinsi gani tunajenga utamaduni wa Watz kutembelea vivutio vya utalii hapa nchini.
Kila siku tunasikia teuzi za Wakurugenzi na Bodi, nadhani ni wakati sasa watu wapimwe kwa ubunifu. Hizi habari za kuteuana zina madhara sana.
..Mwisho, Tanzania ni nchi kubwa na yenye watu wengi. Hatuwezi kutoka kwa kutegemea utalii. Ili tufike kule tunakotaka ni lazima tumuinue MKULIMA.
Tunaposhindwa kuuza chakula ni aibu kubwa san. Sisi tulitakiwa tuwe power house ya kilimo EA
Tuwe na wakulima wakubwa na wadogo !

Utashangaa mkulima wa Mbeya ana magunia ''400,000' ya mahindi halafu serikali haiwezi kumsaidia kupata soko wakati UN kupitia FAO wanataka kwa ajili ya maeneo ya njaa.
Serikali haifanyi biashara lakini inaweka mazingira mazuri.

Kuna watu wana maswali kichwani na moja ni hili '' Watanzania wangapi wata afford utalii wa ndani''. Well jibu ni rahisi sana labda waulize Tanzania breweries wanapata wapi hela? Waulize kule TCRA wanakusanya bilioni ngapi na kutoka wapi?

 
Natamani watu wote wapite na kusoma hii
 
Tanzania tunakwenda vizuri sana,
 
Natamani Mhe Rais asome hii
 
nzuri sana hii taarifae
 
Safi Tanzania,
 
Natamani mamlaka zipitie huu uzi,
 
Hoja nzuri hii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…