Tanzania kwanini isitangaze rasmi lugha ya 3 ya taifa?

Tanzania kwanini isitangaze rasmi lugha ya 3 ya taifa?

Lugha yetu ya Taifa ni moja tu,hizi nyingine ruksa kuzungumza nyumbani
 
Wanajf hamjambo!
Kama swali hapo ambalo huwa najiuliza mara kwa mara , Leo nimeona niwaletee tujadili kidogo kama inafaa au haifai with ground reasons.
Ukifika South Africa wao wana lugha kama nane officially recognized baadhi ni kizulu, kisuthu, Xhosa, Afrikana, English, nk . Ukifika katika ile wanaozaliana kama sangara wao wana English, Yoruba, Hausa, IBO nk zote ni officially recognized national language huko kwenye mji MKUBWA wenye msongamano wa magari Na wengi wa madereva wasio Na nidhamu.
Huko DR Congo kuna Lingala, Kikongo, Manyema , kifaransa nk ni officially recognized Language.
Je hapa Tz kwanini Lugha ya tatu isitambuliwe kuwa lugha 3 ambayo ndiyo lugha ya kiasili inayotumiwa na watz wengi na pia Watanzania wasio wa kabila hiyo wanaifahamu asilimia kubwa Na hata humu jf mtu akisema ngosha unaelewa tu.
Kwanini kisukuma kisiongezwe kiwe lugha ya tatu ya taifa letu? Tafadhali MAENDELEO haya Vyama!

Sent using Jamii Forums mobile app
Hauna akili wewe Kisukuma cha wasukuma. Lugha ya taifa ziendelee kuwa mbili English + Kiswahili. Wewe unataka kuleta ukabila . Na ukiona nchi ina malugha Mengi ya taifa kama Kongo na South kuunite watu ni ngumu Sana. Nchi zilizoendelea zina lugha moja ya taifa mfano USA, China , Germany, N.k.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati wenzako tunahangaika kuondoa language barrier (and all other barriers of communication) we mwenzetu unataka kuturudisha nyuma kama enzi za kuanguka kwa mnara wa Babel!
1551159981166.png
1551159981166.png
 
Hicho kiingereza tu mtihani wangeanza kuboresha hicho kwanza lakini pia tuna kiswahili kama lugha mama kwanini tuingize lugha ya kikabila?? popote uendapo ukizungumza kiswahili watu wataelewa sasa kisukuma wakati Tz kuna makabila sijui 200, lol.

Nakataa hoja yako.
 
Bado kidogo tu utapendekeza kisukuma kitumike mashuleni kama lugha ya kifundishia kwa vile kinaeleweka na watu wengi!!!

kutoka: 22D Arnold st.
 
Dawa zinatakiwa zimezwe kwa umakini sana..
Tanzania ni nchi iliyo na makabila mengi sana hivyo ukifanya hivyo makabila mengine yatatutumka nayenyewe kutaka hivyo..haistahiri kuwa lugha ya taifa kwanza sidhani kama inajitosheleza kimsamiati niambie kompyuta inaitwaje kwa hiyo lugha,pia calculator,rimoti je.?
Mkuu italeta mtafaruku usio mantiki bora tuendelee na tz yetu maana ikitambuliwa mtataka pia iwe lugha ya kufundishia
Sisi wataalamu wa lugha, tunasemaga "Hakuna lugha iliyobora kuliko nyingine" ila yofauti iliyopo ni jinsi lugha hiyo inaeleweka kiasi gani na kiasi gani cha jamii kinaitumia hiyo lugha. Watu wengi wanakielewa kisukuma na pia kinazungumzwa na watu wengi pia. Tukizungumzia habari ya kujirosheleza kimsamiati ni...Kinaweza kutohoa majina au maneno hayo kutoka lugha zingine na kuyafanya kuwa misamiati ya lugha ya kisukuma. Mfano kiswahili kimetohoa misamiati mingi sana si ya kwetu tumeiba kutoka lugha za wenzetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Labda ungesema kinyakyusa.. Maana ndo angalau lugha ambayo ina misamiati inayojulikana nchi nzima.. Na watu wanajisikia proud kutamka maneno ya kinyakyusa!
 
Wanajf hamjambo!
Kama swali hapo ambalo huwa najiuliza mara kwa mara , Leo nimeona niwaletee tujadili kidogo kama inafaa au haifai with ground reasons.
Ukifika South Africa wao wana lugha kama nane officially recognized baadhi ni kizulu, kisuthu, Xhosa, Afrikana, English, nk . Ukifika katika ile wanaozaliana kama sangara wao wana English, Yoruba, Hausa, IBO nk zote ni officially recognized national language huko kwenye mji MKUBWA wenye msongamano wa magari Na wengi wa madereva wasio Na nidhamu.
Huko DR Congo kuna Lingala, Kikongo, Manyema , kifaransa nk ni officially recognized Language.
Je hapa Tz kwanini Lugha ya tatu isitambuliwe kuwa lugha 3 ambayo ndiyo lugha ya kiasili inayotumiwa na watz wengi na pia Watanzania wasio wa kabila hiyo wanaifahamu asilimia kubwa Na hata humu jf mtu akisema ngosha unaelewa tu.
Kwanini kisukuma kisiongezwe kiwe lugha ya tatu ya taifa letu? Tafadhali MAENDELEO haya Vyama!

Sent using Jamii Forums mobile app
The Applicant must be fluent in English, Kiswahili and Kisukuma!!!
 
Ukiondoa kiingereza na kiswahili lugha inayoongeleka zaidi jf ni kinyakyusa
 
... Kichagga kipi bro? Cha Machame? Uru? Kibosho? Old Moshi? Marangu? Mwika? Mamsera? Mkuu? Mashati? au Tarakea? Maana kila baada ya hatua chache ni lugha mbili tofauti! Kama taifa tulishaachana na ukabila lakini!


Kisukuma nacho hakina tofauti kama hizo?
 
Kisukuma nacho hakina tofauti kama hizo?
... sina hakika japo uwezekano huo upo ila haiwezekani ikawa kwa kiwango cha kutisha kama Kichaga! Kwa mfano Kimasai; Kimasai ni Kimasai - no matter ni mmasai wa Tanzania au Kenya; Kiteto au Mkuranga; Kilosa au Katavi!
 
Hauna akili wewe Kisukuma cha wasukuma. Lugha ya taifa ziendelee kuwa mbili English + Kiswahili. Wewe unataka kuleta ukabila . Na ukiona nchi ina malugha Mengi ya taifa kama Kongo na South kuunite watu ni ngumu Sana. Nchi zilizoendelea zina lugha moja ya taifa mfano USA, China , Germany, N.k.

Sent using Jamii Forums mobile app
... isipokuwa India - 12 official languages.
 
Wagonjwa wa akili tunao mitaani then milembe tumepeleka wenye afadhali duh! Knifeclit my foot! [emoji848][emoji848][emoji848]

ᴾᵘⁿⁱˢʰ ᵒⁿˡʸ ʰᵉ ʷʰᵒ ᶜᵒᵐᵐⁱᵗᵗᵉᵈ ᵗʰᵉ ᶜʳⁱᵐᵉ✓
 
... sina hakika japo uwezekano huo upo ila haiwezekani ikawa kwa kiwango cha kutisha kama Kichaga! Kwa mfano Kimasai; Kimasai ni Kimasai - no matter ni mmasai wa Tanzania au Kenya; Kiteto au Mkuranga; Kilosa au Katavi!


Safi sana . Pendekeza na Kimasai nacho kiwe lugha ya Taifa. Kama ulivyosema kinavuka hata mipaka.
 
Safi sana . Pendekeza na Kimasai nacho kiwe lugha ya Taifa. Kama ulivyosema kinavuka hata mipaka.
... post yangu ya kwanza uliniyo-quote awali niko against na ukabila. Siwezi kupendekeza kitu cha aina hiyo!
 
Tupo karibia robo tatu ya watanzania, kwenye kupiga kura sisi ndio tunaamua nani atuongoze. Kuna siku tutaizunguka bongo yote tutaiweka mtu kati yani tutakua remote ya Tanzania yetu, I'm lake zonian.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom