Tanzania Labour Law (Sheria ya Kazi Tanzania)


Kama amekupa barua ya increment ya mshahara, then anataka kukushusha kwamba alifanya makosa sheria inasemaje!
 
je? muajiri anapovunja mkataba wa zamani na kukupa mpya unaoonesha ongezeko la mshahara kwa madhumuni ya kuhamisha kitengo kimoja kwenda kingine kisha ukakaa mwezi mzima bila kufanya kazi kitengo hicho kipya atatakiwa kukulipa mshara wa mkataba mpya au wa zamani msaada tafadhali.
 

Why would only Acting Allowance be a taxable income?
What about other allowances? are there any regulations on this?
Please assist.
 
jamani mm nina acting nafasi kwa muda mrefu lkn napata mshahara wangu uleule, je kuna allowance yoyote na inalipwaje???
 
wandugu, msihangaike kutafuta sheria. sheria zote za tz kuanzia mpya hadi za zamani, zipo kwenye website ya parliament of tz. nenda kule utaipata kwenye pdf. nashangaa wengine wanasema walikuwa wanatafuta sheria hizi, wakati ziko wazi sana, tena mno.

Kule kwenye website ya Bunge unapata Pricipla Act lakini hupati Subsidiary zake yaani Regulations zake.
 
Habari,

Naomba mtu anielekeze jinsi ya kukokotoa acting allowance

Calculate the difference bwteen your salary and the salary of your superior acting post. Msingi mkuu ni katiba yetu isemayo {Every person is entitled to just remuneration (Katiba ya Tanzania, section. 23)}.

Hivyo, unapo-act unakuwa unafanya kazi ya post ya juu na hivyo mapato unatakiwa upate kama yake maana unafanya uzalishaji kama wake.
 
LUSAJO L.M.,

Kuhusu mahudhurio nenda kasome Code of Good Practice ilitoka mwaka 2007. Kuhusu kuukuzwa kazi hazuiwi na sheria kuwatangazia lakini huyo mfanyakazi akishinda kesi itakuwa taabu kwa mwajiri maana hilo tangazo litakuwa limemdharirisha na itabidi kumlipa fidia kubwa.
 
mkuu nisadieni sheria ya kwenda leave ni siku ngapi na mfanyakazi anawajibika kufanya kazi msaa mangapi kwa siku

Leave ni siku 28 mfululizo bila kukatakata.

31.-(1) An employer shall grant an employee at least 28 conse-cutive days' leave in respect of each leave cycle, and such leave shall
 
mimi sielewi vizuri kipengele cha severance allowance,,,mtu akiomba kuacha kazi, haupewi malipo ya severance allowance? na kama ndio hivyo, malipo haya yanatolewa mpaka mwajiri ukuachishe kazi...hebu dadavua kidogo

42.-(1) For the purposes of this section, ''severance pay'' means an
amount at least equal to 7 days' basic wage for each completed year of
continuous service with that employer up to a maximum of ten years.

(2) An employer shall pay severance pay on termination of emploment
if-
(a) the employee has completed 12 months continuous service
with an employer; and
(b) subject to the provisions of subsection (3), the employer terminates
the employment.
 

Je, wanaozifuatilia kinawatokea nini huko makazini?
 
Hivi ni section gani inazungumzia malipo baada ya mkataba kuisha? Sec 42 ya ELRC 2004 inasema severance pay ni hadi uwe terminated sasa mimi mkataba umeisha na sikuwa terminated, natambua section 42.1 inasema malipo yapo ila section 42 iko chini ya heading "other incidents of termination" naomba msaada jamank
 
Severance pay ni haki anayoipata mfanyakazi mara tu ajira inapokoma. Sifa ya kupata hiyo severance pay ni mpaka uwe umefanya kazi kwa muda wa mwaka au zaidi, na unalipwa si zaidi ya miaka kumi ktk utumishi wako. Kwa mshahala wa siku 7 kwa kila mwaka.

Kuna marekebisho yalifanyika. Kama uko pensionable, severance hailipwi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…