Tanzania Labour Law (Sheria ya Kazi Tanzania)

Tanzania Labour Law (Sheria ya Kazi Tanzania)

hapana,kuna mikataba yote ya miaka mitano na michango ya nssf ilivyokuwa ikiingia
mhh okay,lakini tusiende mbali sana maana ishu yako kubwa ni uhitaji wa michango yako ya NSSF tu,jitahidi kufuata utaratibu wa kufanya marekekebisho ya michango kama ilivyoelekezwa na wadau huko juu ,ila michango ya Mwaka na miezi 9 kwa sababu ulikuwa haukatwi chochote kwa ajili ya NSSF na mwajiri wako katika kipindi hiko ni ngumu kuidai,na hatujui ilikuwa mwaka gani pia. ila nakutakia kila kheri katika mchakato wako.
 
Sijui labour law mara katiba mambo ya sheria ni utapeli na ujinga mtupu ,kazi kuwapumbaza watu ila hayo mambo hayafuatwi...

Kuna watu wanapata uhamisho wa mbali mpaka wanapewa deadline ya kuripot wanafika hawapati stahiki zao ng'o eti tunafuata mchakato ,wanakaa vikao kupanga mtu apate stahiki zake.

Mtu kahamishwa tena ghafla alipotoka kaacha kodi ya miezi labda 3 mbele then apewi chake eti wanasubiria mchakato wa malipo na kuripot anatakiwa kufika ghafla ...

MaHR hawajielewi kutoa stahiki mpaka wakae vikao izo sheria zimebaki kweny makaratasi ni utapeli mtupu.

Nilihamishwa na taasisi mwaka fulani ,nimekaa nao miaka kibao ila kunilipa eti wanafanya uhakika washenzi kabisa msharaha wamenilipa mda sana ila kulipa kwa mkupuo stahiki hawataki mpaka nimeripot na kuanza kazi miezi miwili mbele ndio wamelipa.
Ujinga mtupu baadhi ya taasisi za serikali ndio zinafuata ila wengi ni hovyo kabisa
 
sikuwa nakatwa,nilikuwa nafanya kazi kama mwajiriwa lkn bila mkataba
Hapo utakuwa unataka kujikosesha haki zako kama mwajiriwa kwa kuwaza hivi, ipo hivi mfanyakazi yoyote atakaefanye kazi siku moja au zaidi awe skilled or unskilled anapaswa kuwa na mkataba kisheria kabisa na mfanyakazi huyo anatakiwa achangiwe kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii, NSSF Act inamtaka mwajiri kupeleka michango ya wafanyakazi nssf mwezi mmoja baada ya offisi hiyo kusajiliwa hizo ni sheria zipo hamjazipitia tu, na haijalishi wewe ni skilled au unskilled worker mkataba kwako ni lazima na lazima michango yako ipelekwe nssf ili kupata huduma mbalimbali , fanya kama ushauri wa awali niliokupatia waonyeshe nssf ulianza kibarua chako lini
 
ivi certificate of service anayotoa muhajiri inakazi gani
Inakusaidia kuonyesha una uzoefu wa majukumu fulani fulani ulipofanyia kazi awali, ukiwa nacho hicho cheti kinajaza sifa zaidi ya uzoefu hata huko mbeleni ukiomba kazi
 
Sijui labour law mara katiba mambo ya sheria ni utapeli na ujinga mtupu ,kazi kuwapumbaza watu ila hayo mambo hayafuatwi...

Kuna watu wanapata uhamisho wa mbali mpaka wanapewa deadline ya kuripot wanafika hawapati stahiki zao ng'o eti tunafuata mchakato ,wanakaa vikao kupanga mtu apate stahiki zake.

Mtu kahamishwa tena ghafla alipotoka kaacha kodi ya miezi labda 3 mbele then apewi chake eti wanasubiria mchakato wa malipo na kuripot anatakiwa kufika ghafla ...

MaHR hawajielewi kutoa stahiki mpaka wakae vikao izo sheria zimebaki kweny makaratasi ni utapeli mtupu.

Nilihamishwa na taasisi mwaka fulani ,nimekaa nao miaka kibao ila kunilipa eti wanafanya uhakika washenzi kabisa msharaha wamenilipa mda sana ila kulipa kwa mkupuo stahiki hawataki mpaka nimeripot na kuanza kazi miezi miwili mbele ndio wamelipa.
Ujinga mtupu baadhi ya taasisi za serikali ndio zinafuata ila wengi ni hovyo kabisa
pole sana ,ila naona serikalini kuna changamoto sana tofauti na sekta binafsi .
 
Huruma sana, mfanyakazi wa taasisi binafsi kafukuzwa kazi bila kulipwa kiinua mgongo, amefanya kazi miaka 22. Kosa eti kwa nini hajamripoti meneja wake kwenye kamati ya maadili kwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mfanyakazi wa chini yake. Jamaa anasema binti ndio aliyemwambia kuwa anatoka na boss wake. Inaonekana ni kama binti hakupewa kitu alichokubaliana na meneja, ndio akaamua kuripoti kwenye kamati ya maadili ya kampuni. Huko kwenye kamati wakati akieleza akamtaja yule mfanyakazi aliyemjurisha kwamba anatoka na boss wake. Huyu mfanyakazi aliyefukuzwa kazi ni msaidizi wa meneja aliyekuwa akitoka na huyo binti. Sasa kamati ya maadili ikawafukuza wote wawili yaani meneja na msaidizi wake. Sasa jamaa anaumia na ameamua kufungua shauri CMA kulalamika kwa nini afukuzwe kwa kosa alilolifanya meneja wake. Yeye sio mmoja wa watu waliopewa kazi ya kupokea kesi za kingono lakini binti alipomjulisha kwamba anatoka na boss wake alimshauri akaripoti kwa wahusika wanaopokea kesi za aina hio na binti akaenda kuripoti. Baada ya kikao cha nidhamu akaachishwa kazi kwa gross negligence. Hivi hapo haki ilitendeka kweli au ni mpango wa kudhurumu kiinua mgongo cha jamaa, maana alikuwa ndio anakaribia kustaafu.
 
Je!Ikitokea kuuzwa kwa kampuni unayofanyia kazi na mnunuzi akahitaji kukupa mktba wake baada ya kukamilisha taratibu za ununuzi ni ipi haki unayostahili km mfanyakazi kabla ya kusign mktba mpya?
Maelezo kwa mikataba yote 2 usiokuwa na kikomo na wa muda maalumu
 
Je!Ikitokea kuuzwa kwa kampuni unayofanyia kazi na mnunuzi akahitaji kukupa mktba wake baada ya kukamilisha taratibu za ununuzi ni ipi haki unayostahili km mfanyakazi kabla ya kusign mktba mpya?
Maelezo kwa mikataba yote 2 usiokuwa na kikomo na wa muda maalumu
Ninavyojua kuna vitu muhimu lazima uelezee kama muda wa mkataba, masaa ya kazi na taratibu zake, majukumu yako, haki zako, stahiki n.k sasa kama kuna kipengele hukubaliani nacho hapo ndio unaweza kataa au mkaangalia mnakiweka vipi kati yako na muajiri.
 
Ninavyojua kuna vitu muhimu lazima uelezee kama muda wa mkataba, masaa ya kazi na taratibu zake, majukumu yako, haki zako, stahiki n.k sasa kama kuna kipengele hukubaliani nacho hapo ndio unaweza kataa au mkaangalia mnakiweka vipi kati yako na muajiri.
Mktba uliopo sasa ambao ni wa muajiri wa zamani ni usio na kikomo na masaa ya kazi ni 8 pamoja na kutumia mktba huu wa zamani na kuendelea kupata stahiki zao km mktb ulivyokuwa unasema lkn wanasimamiwa na kampuni x ambayo ndio mnunuzi wa kampuni ya zamani.
Msaada unaohitajika hapa ni kujua ni ipi haki anayostahili muajiriwa kwa kuvunjiwa mktb wake wa zamani kabla ya kusign mktb mpya ambao ni wa mnunuzi wa kampuni ya zamani?
 
Mktba uliopo sasa ambao ni wa muajiri wa zamani ni usio na kikomo na masaa ya kazi ni 8 pamoja na kutumia mktba huu wa zamani na kuendelea kupata stahiki zao km mktb ulivyokuwa unasema lkn wanasimamiwa na kampuni x ambayo ndio mnunuzi wa kampuni ya zamani.
Msaada unaohitajika hapa ni kujua ni ipi haki anayostahili muajiriwa kwa kuvunjiwa mktb wake wa zamani kabla ya kusign mktb mpya ambao ni wa mnunuzi wa kampuni ya zamani?
Mkuu kama mmefikia hatua anawasainisha mkataba mwingine ni hatua nzuri. Kilichobaki hakuna haki nyingine za msingi zaidi ya kupata mkataba mwingine atakao saini muajiri mpya basi. Cha muhimu kuzingatia ni mambo ya msingi ya mkataba yanazingatiwa kabla hujasaini ambayo nimeyaeleza post ya juu.
 
Huruma sana, mfanyakazi wa taasisi binafsi kafukuzwa kazi bila kulipwa kiinua mgongo, amefanya kazi miaka 22. Kosa eti kwa nini hajamripoti meneja wake kwenye kamati ya maadili kwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mfanyakazi wa chini yake. Jamaa anasema binti ndio aliyemwambia kuwa anatoka na boss wake. Inaonekana ni kama binti hakupewa kitu alichokubaliana na meneja, ndio akaamua kuripoti kwenye kamati ya maadili ya kampuni. Huko kwenye kamati wakati akieleza akamtaja yule mfanyakazi aliyemjurisha kwamba anatoka na boss wake. Huyu mfanyakazi aliyefukuzwa kazi ni msaidizi wa meneja aliyekuwa akitoka na huyo binti. Sasa kamati ya maadili ikawafukuza wote wawili yaani meneja na msaidizi wake. Sasa jamaa anaumia na ameamua kufungua shauri CMA kulalamika kwa nini afukuzwe kwa kosa alilolifanya meneja wake. Yeye sio mmoja wa watu waliopewa kazi ya kupokea kesi za kingono lakini binti alipomjulisha kwamba anatoka na boss wake alimshauri akaripoti kwa wahusika wanaopokea kesi za aina hio na binti akaenda kuripoti. Baada ya kikao cha nidhamu akaachishwa kazi kwa gross negligence. Hivi hapo haki ilitendeka kweli au ni mpango wa kudhurumu kiinua mgongo cha jamaa, maana alikuwa ndio anakaribia kustaafu.
Pole sana kwa maelezo uliyotoa nafikiri hayana uhusiano na Gross Negligence,muhimu mwambie atafute wakili mzuri wa masuala ya kazi ili aweze kupata msaada zaidi na ikikupendeza basi karibuni tufanye kazi
 
Mktba uliopo sasa ambao ni wa muajiri wa zamani ni usio na kikomo na masaa ya kazi ni 8 pamoja na kutumia mktba huu wa zamani na kuendelea kupata stahiki zao km mktb ulivyokuwa unasema lkn wanasimamiwa na kampuni x ambayo ndio mnunuzi wa kampuni ya zamani.
Msaada unaohitajika hapa ni kujua ni ipi haki anayostahili muajiriwa kwa kuvunjiwa mktb wake wa zamani kabla ya kusign mktb mpya ambao ni wa mnunuzi wa kampuni ya zamani?
option ziko Mbili;
1: Mtabaki na mikataba yenu ile ile ambayo haina ukomo(Permanent contract)na itakuwa na taratibu zile zile za kazi kitakachobadilika ni kuwa mtasaini Makubaliano ya kubadilika kwa Mwajiri tu.
2. Mtafunga au kuvunja mikataba ya Zamani na mWajiri wa zamani na mtalipwa stahiki zenu kama kawaida(annual leave,Salary or renumeration,severance pay,notice(with limitation or caution),certificate of service)hizi ni baadi ya stahiki.

Pia karibu kwa maelezo zaidi maana kuna taarifa hazipo sawa katika maelezo yako
 
Back
Top Bottom