Tanzania mtu ana Kodi mkononi anahangaika kuilipa

Tanzania mtu ana Kodi mkononi anahangaika kuilipa

TRA TRA TRA TRA ,kitengo cha rushwa, wanakuzungusha ili muda upite wakupige penati kama za Mbape
 
Mtu anatakiwa alipe Kodi akiwa amelala sio kwenda kupanga foleni na ujinga wa control number
Yaani kama TRA Dodoma unaenda ofisini kwao kulipa kodi wanajizungusha wee hadi ugombane nao ndio wanaanza kushughulikia suala lako.
 
ukipewa control number si unalipa kupitia sim bank
 
Hata kuwe na mfumo gani bila kujituma na kuwajibika vema TRA itachukiwa siku zote. Watanzania tumezoea kufanya vitu siku ya deadline na hilo ndio linawagharimu watu sana
Hapana Mkuu, ukitaka kwenda kulipa kodi TRA au kupata leseni ya biashara Halmashauri, kama ni mfanyakazi omba kabisa ruhusa kazini. Maana inachukua Siku 1 au 2 kushughulikia masuala hayo.
 
Hapana Mkuu, ukitaka kwenda kulipa kodi TRA au kupata leseni ya biashara Halmashauri, kama ni mfanyakazi omba kabisa ruhusa kazini. Maana inachukua Siku 1 au 2 kushughulikia masuala hayo.
Kwani Mwigulu Mchemba na Mama Samia hawajaliona hilo tatizo.?
 
TRA wataona kodi yangu wakiwezesha mtu kulipa kodi akiwa ofisini kwake,na sio kwenda kupanga Foleni.

Tofaut na Hapo watanijua kwa majina Mengi sana... Saivi hadi babu yangu ana duka lake nalisimamia mimi.
 
Nimesoma quote ya mtu mmoja hapa jf, imenifurahisha sana. Ni kuhusu sakata la Diamond na TRA. Ni ukweli usiopingika mfumo wa ulipaji Kodi Tanzania bado ni changamoto. Hii efilling system ina watesa sana watu. Nashauri TRA wakae chini walitafakari hili, na kuja na mfumo rahisi na wezeshi kwa kulipa Kodi

Nawasilisha
System yao ni mbovu na nahisi hawaitengenezi ili waendelee kupiga hela za faini kwa kuchelewesha kufanya returns za mwezi. Brela nao system yao ya annual fee payment ni majanga matupuu
 
Back
Top Bottom