Tanzania na Japani kupitia Shirika lake la Maendeleo (JICA), zimetiliana saini mkataba wa msaada wa kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto.

Tanzania na Japani kupitia Shirika lake la Maendeleo (JICA), zimetiliana saini mkataba wa msaada wa kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto.

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
3,978
Reaction score
6,739
Tanzania na Japan kupitia Shirika lake la Maendeleo (JICA), zimetiliana saini mkataba wa msaada wa Yen za Japan bilioni 1.527 sawa na shilingi bilioni 27.3 kwa ajili ya kuboresha sekta ya afya nchini.

Mkataba huo umesainiwa katika Ofisi za Hazina Ndogo jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, kwa niaba ya Serikali ya Tanzania, Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Yoichi Mikami na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bw. Hitoshi Ara, kwa niaba ya Serikali ya Japan.
Screenshot_20250315_081503_Lite.jpg


Akizungumza baada ya kusaini mkataba huo, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, alisema kuwa fedha hizo zitatumika katika ununuzi wa vifaa-tiba ili kuimarisha huduma za afya ya mama na mtoto.

Dkt. Mwamba alisema kuwa, ufadhili huo muhimu unaendana na Mpango wa sasa wa Maendeleo wa Miaka Mitano ambao pamoja na masuala mengine, unalenga kutatua changamoto za ubora katika utoaji huduma za afya nchini.

“Ufadhili huu unaunga mkono juhudi za Serikali kwenye sekta ya afya, zinazolenga kuhakikisha huduma bora za afya zinapatikana kwa wakati kwenye jamii,” alisema Dkt Mwamba.

Tusubirie kampeni zianze tupate kusema kuwa maendeleo yote yaliyotokea Tanzania ni juhudi na nguvu za Mama Samia. Ila asanteni sana Wajapani maana kwenye miaka zaidi ya 60 ya uhuru bado watanzania tuna shida kwenye miundombinu ya afya haswa katika kipengele cha afya ya Mama na mtoto. Hakika Mama anaupiga mwingi sana.
 
Bado tunaendelea kusaidiwa😂😂😂 .. We are so stupid.. Huo sip msaada bali ni gawio wanalotupa baada ya kuwa wateja wazuri wa magari yao ..
1 Brand new na ya kifahari kwa serikali.. Hapa Mjapani anapiga pesa mpaka anazikimbia
2. Soko la magari mitumba.. Afrika na Tanzania ikiwemo ni dampo la magari mabovu na yaliyotumika toka Japan.. Hili pekee ni nafuu kubwa sana kwao..
3. Mitambo, mashine na vitu mbalimbali mitumba na vilivyotumika na kupitwa na wakati.. Hapa pia Japan wamepata jalala la kutupia uchafu wao na ni jalala zuri kwakuwa badala ya kulipia gharama za jalala wao ndio wanalipwa
Kwahiyo tukijidanganya kwamba ni msaada tunahitaji kupimwa akili zetu mirembe
 
Bado tunaendelea kusaidiwa😂😂😂 .. We are so stupid.. Huo sip msaada bali ni gawio wanalotupa baada ya kuwa wateja wazuri wa magari yao ..
1 Brand new na ya kifahari kwa serikali.. Hapa Mjapani anapiga pesa mpaka anazikimbia
2. Soko la magari mitumba.. Afrika na Tanzania ikiwemo ni dampo la magari mabovu na yaliyotumika toka Japan.. Hili pekee ni nafuu kubwa sana kwao..
3. Mitambo, mashine na vitu mbalimbali mitumba na vilivyotumika na kupitwa na wakati.. Hapa pia Japan wamepata jalala la kutupia uchafu wao na ni jalala zuri kwakuwa badala ya kulipia gharama za jalala wao ndio wanalipwa
Kwahiyo tukijidanganya kwamba ni msaada tunahitaji kupimwa akili zetu mirembe
Angalia Mkuu wasije kukuita mchochezi maana kuna watu wanabubujikwa na machozi kila siku 😃
 
JAICA ina tofauti gani na USAID? siku japan ikipata waziri mkuu mwenye sera kama za trump tujiandae kisaikolojia
UK Aid Direct, SNV, KOICA, JAICA, nqa wengine ajenda yao ni moja tu
 
UK Aid Direct, SNV, KOICA, JAICA, nqa wengine ajenda yao ni moja tu
umewasahau kina SIDA, DANIDA, NORWEGIAN AID, CANADIAN AID na lile la Finland, hawa wakiiga ya Trump na USAID sijui itakuaje kwenye bajeti yetu ya maendeleo ya nchi
 
umewasahau kina SIDA, DANIDA, NORWEGIAN AID, CANADIAN AID na lile la Finland, hawa wakiiga ya Trump na USAID sijui itakuaje kwenye bajeti yetu ya maendeleo ya nchi
Tutalamba nyasi ila ujinga upo kwa viongozi! Unasema kuwa unakusanya mapato trillions na trillions je zinaenda wapi!?
 
Kuna andiko nililiweka jana eti Ubalozi wa Japani umetusaidia kujenga darasa Arusha 😔 serious?! TRA inakusanya mapato kuliko kipimo halafu madarasa yanajengwa na wafadhili?! Aisee hii nchi
We must be mentally castrated
 
JICA watu poa sana. Sijui walipotelea wapi. Walitujengea irrigation scheme kule Mbarali hadi leo watu wanapiga mpunga(pun intended😂)
 
JICA watu poa sana. Sijui walipotelea wapi. Walitujengea irrigation scheme kule Mbarali hadi leo watu wanapiga mpunga(pun intended😂)
Serikali haijachukua umiliki kweli!??
 
Back
Top Bottom