Tanzania na siasa: Lugha ya kutumia Kiswahili au Kiingereza, Tatizo lipo wapi?

Tanzania na siasa: Lugha ya kutumia Kiswahili au Kiingereza, Tatizo lipo wapi?

wanaotetea kufundisha kwa kiswahili wanasema wanafunzi wataelewa zaidi kuliko kwa kiingereza wengine wanasema ni kuenzi utamaduni. hilo la kwanza sidhani kama ni sahihi maana kwa miaka yote watanzania wamekuwa wakipata elimu kwa kiingereza hapa nchini na nje ya nchi na wengi wanatenda kazi vizuri tu. tatizo la sasa la kiingereza linatokana na mfumo mbaya uliobomoa si kiingereza tu bali elimu kwa ujumla. hilo la utamaduni ni finyu maana karibu kila kitu tunachotumia hakina asili yetu; mavazi, vyombo vya usafiri, tv, redio hata elimu yenyewe sasa na hivi tuviache?. wakati dunia inazidi kuwa moja ni makosa kufikiri kuwa kiingereza si sehemu ya utamaduni wa dunia kwa sasa ambamo tumo.
kinachotakiwa kuondoa ni zile sababu zilizofanya kiingereza kishuke na elimu itetereke kama wingi wawanafunzi darasani, uandaaji mbovu wa walimu, uhaba wa vifaa n.k Angalia Rwanda imeamua kutumia kiingereza katika elimu na wanaenda vizuri sisi tunacho tayari lakini tunataka kukitupa eti ndipo tutapata kukielewa zaidi hizo ni ndoto za mchana. wanaotaka kufundisha kwa kiswahili waanzishe shule zao waanze kama majaribio. tena tukiamua kufundisha kwa kiswahili ndipo shule za English medium zitazidi kuongezeka na wanaoshabikia watawapeleka watoto wao huko. taifa litazidi kuparaganyika kwa matabaka.
 
miaka ya nyuma katika shule za sekondari wanafunzi walifanya vizuri sana. walikuwa waandishi wazuri tu wa makala za kiswahili na kiingereza. debates zilikuwa motomoto mashuleni. elimu ilikuwa hai. hakukuwa na malalamiko kuwa wanafunzi hawakuwa wanayaelewa masomo kwa sababu ya lugha. hapo kati kumekuwa na siasa nyingi katika elimu siasa nyingine ni zile za kukiponda kiingereza kwa kukihusiha na ukoloni. sasa wanafunzi, si katika shule pekee bali hata katika elimu ya juu wana tatizo la lugha. badala ya kutafuta ufumzbuzi kwa kuangalia sababu halisi tuna sema tukifanye kiswahili lugha kufundishia. huu ni uvivu wa kupambana na matatizo kwa kutafuta njia rahisi
 
Hatusemi kwamba Kiingereza kitelekezwe,kiwe kama somo ila Kiswahili iwe lugha ya kufundishia,tunataka watu wenye maarifa na sio mabingwa wa kukariri.
 

Mzee Kipara!
kwa kweli huwa nawashangaa watu na wengine ni maproff wa vyuo vikuu wanakazana eti kiswahili kiwe lugha ya kufundishia waaki argue kwamba wajerumani, wajapani, warusi wachina nk wanatymia lugha zao na ndio maana watoto wanaelewa vizuri lakini wanasahau kwamba hao watu wana wataalam wao katika nyanja zoote za sayansi tangu zamani, na wavumbuvi ni wao wenyewe sisi ni siasa tu kila mahali, mfano mdogo tu wanyarwanda juzi tu walikuwa ma franco-phone wamechange kwenda anglo-phone watatupita kama tumesimama!

kama lugha ni tija tuangalie nchi kama Ethiopia wana lugha yao , tena yenye herufi zake! mbona wapo hoi? sisi tunapiga domo eti kiswahili kiswahili! yaani watz tuna mambo wengine utawasikia eti yaani miaka 50 ya uhuru nchi bado masikini, ina uhusiano gani? kama uhuru ni issue Ureno ilikua wakoloni tangu enzi za vasco da gama, lakini leo wanakopa angola iliyopata uhuru juzi! we do not think! kila kwetu ni siasa htutanda mbali!

kimsingi naungana nawe pamoja na mtoa mada and thanks for a very constructive thread!

Kakubaliana na wewe. Kimsingi kutokujua kiingereza kunatugharimu sana mpaka dakika hii, ajira zetu kwenye nyanja nyingi zinazohitaji kujua kiingereza zinachukuliwa na wakenya, kutojua kiingereza kunatukosesha confidence kwenye international bargains, baadhi ya blander ambazo viongozi wetu wanafanya au kuingizwa mkenge ni kwa sababu ya kukosa confidence kunakosababishwa na kutojua kiingereza vizuri. Mimi najua oppotunity kadhaa ambazo taasisi ninayofanyia kazi imezipoteza (zikachukuliwa na wakenya au nchi nyingine), bosi wetu huwa anatoa visingizio lakini reading between the lines mtu unajua tu kwamba swala la wenzake kujua kiingereza zaidi lina mchango.

Tuna sababu nyingi sana za kukuza kiingereza, tusijidanganye, na sehemu nzuri ya kuanzia ni mashuleni, kuanzia shule ya msingi kiingereza kipewe umuhimu wa kutosha, kuwe na mida inayotengwa kwa wanafunzi kufanya mawasiliano yote kwa kiingereza, kujua lugha kunahitaji practice, ukianza kuongea broken English shule ya msingi mpaka ufike chuo kikuu utakuwa umeimprove sana, na kama nilivyosema mwanza, tusiondoe vitabu vilivoandikwa kwa kiingereza, viendelee kubaki hata kama tutachagua kiswahili kitumike kufundishia (jambo ambalo mimi silifurahii sana). Tuondoe mawazo ya kwamba kumlazimisha mwanafunzi kuongea kiingereza ni utumwa, mawazo ya namna hiyo ndo yanatufanya tuwe mamaimuna milele.
 
Sijasema nina mpango wa kuandika kitabu, rudia kusoma vizuri.

Sijasema kwamba kama hatuna Q kwenye Kiswahili tusitumie lugha yetu, hiyo habari ya waarabu ni moot, non sequitur.

Kusema kwamba quantum "imeanza" miaka 300 iliyopita is laughable.

Sijui Wachina, Wajapan, Wakorea walitafuta misamiati kwa njia gani. Najua waingerez walitohoa kutoka kilatini bila ya kuharibu misingi fulani ya kutohoa ambayo imekuwapo tangu wafaransa walivyotohoa kwa Warumi, Warumi walivyotohoa kwa Wagiriki na Wagiriki walivyotohoa kwa Wamisri na Waarabu.

Kwamba kutohoa si jambo geni hakukatai kwamba kutohoa bila kuua misingi ya matamshi ya lugha nako si jambo geni.

Mkuu.

Nimesema Quantum imeanza KAMA miaka 300, na sikusema miaka ilianza miaka 300. Studies and concepts za Quantum zilianza karne ya 17 na 18.

Unasema habari ya waarabu ni moot, non sequitur. Lakini unapoelezea jinsi waingereza walivyotohoa unarudi kulekule kwenye mfano wangu wa waarabu. Unasema wagiriki wametohoa kutoka kwa waMisri na Waarabu. Hii sio kweli. Naweza kukubali kwa shingo upande kuhusu waMisri, lakini sio waarabu. Ni waarabu walitohoa kutoka kwa wagiriki.

Turudi kwenye mada. Kama unaelewa jinsi waingereza walivyotohoa, tuelezee basi jinsi walivyotohoa.
 

Mzee Kipara!
kwa kweli huwa nawashangaa watu na wengine ni maproff wa vyuo vikuu wanakazana eti kiswahili kiwe lugha ya kufundishia waaki argue kwamba wajerumani, wajapani, warusi wachina nk wanatymia lugha zao na ndio maana watoto wanaelewa vizuri lakini wanasahau kwamba hao watu wana wataalam wao katika nyanja zoote za sayansi tangu zamani, na wavumbuvi ni wao wenyewe sisi ni siasa tu kila mahali, mfano mdogo tu wanyarwanda juzi tu walikuwa ma franco-phone wamechange kwenda anglo-phone watatupita kama tumesimama!

kama lugha ni tija tuangalie nchi kama Ethiopia wana lugha yao , tena yenye herufi zake! mbona wapo hoi? sisi tunapiga domo eti kiswahili kiswahili! yaani watz tuna mambo wengine utawasikia eti yaani miaka 50 ya uhuru nchi bado masikini, ina uhusiano gani? kama uhuru ni issue Ureno ilikua wakoloni tangu enzi za vasco da gama, lakini leo wanakopa angola iliyopata uhuru juzi! we do not think! kila kwetu ni siasa htutanda mbali!

kimsingi naungana nawe pamoja na mtoa mada and thanks for a very constructive thread!
yeah, Abysinia wana kila kitu chao.Ila hali bado ipo teh teh.Ingawa ndania kuna makundi yanayojiona kuwa wayahudi wanafanya vitu aggresivel na kwa kiwango ambacho hatufikii katikati ya umasikini na ukame.

Ureno pia wanakopa na kuhamia msumbiji,angola na Brazil.Angalau wao wanakubalika na makoloni yao.Wareno wanahama kwa makundi kwenda hizi nchi.
 
Wingi wa hospitali ni hospitali.

Hospitali hii, hospitali hizi.

nakubalina na wewe ndio maana nikasema watu wengi more confortable kuweka ma~ kama prefix, pale wanapotaka weke uzito wa ukubwa(ingawa hawamaanishi negative sense hapa).Sasa itakuweje hii tafsiri ikiisha ktk vitabu na ktk makundi ya wasomi fulani tuu?

watu wanasema Mahoteli, mashule, mahospital , majizi, magogo, madawati,masikio,masalia, mahusiano,maaskofu, masheikh.

nini kinahalalisha maneno mengine na mengine kutolea.
 
Hatusemi kwamba Kiingereza kitelekezwe,kiwe kama somo ila Kiswahili iwe lugha ya kufundishia,tunataka watu wenye maarifa na sio mabingwa wa kukariri.

Ila unaweza shangaa sana ukija jua kuwa hata wanamuziki wetu huwa wanafuata pattern moja tuu, mara mmoja anapofanikiwa ktk hiyo pattern.N ahuyo aliyefanikiwa unakuja kuta aliiga katk miziki ya nje.Kukariri ni sehemu ya jamii yetu sana.N ahii imeota mizizi sana mashariki ya kati, elimu zao zinaenzi kukariri.

Tabia ya kutopenda tafuta neno sahihi linalowakilisha mawazo yetu ndipo kunapotuponza tunakuwa dhaifu kwa kila kitu,hata kile tunachodhani tunafahamu.
 
nakubalina na wewe ndio maana nikasema watu wengi more confortable kuweka ma~ kama prefix, pale wanapotaka weke uzito wa ukubwa(ingawa hawamaanishi negative sense hapa).Sasa itakuweje hii tafsiri ikiisha ktk vitabu na ktk makundi ya wasomi fulani tuu?

watu wanasema Mahoteli, mashule, mahospital , majizi, magogo, madawati,masikio,masalia, mahusiano,maaskofu, masheikh.

nini kinahalalisha maneno mengine na mengine kutolea.

Mimi si Mtaalamu wa Lugha , ila kwa ufahamu wangu siyo maneno yote yana mabadiliko katika wingi Mfano hayo Hoteli, Hospitali Shule , Meza ,Pesa,Baiskeli, Nadharia,Salamu ,Habari ,Maji, Hewa,n.k Watu tunaweka viambishi awali au tamati kimakosa .

Hilo neno majizi limetumika kama kivumishi cha sifa yaani kuelezea kama mwizi aliyekubuhu , kwa mtazamo wangu naona si fasaha.Labda wataalamu wa kiswahili watafafanua .
 
Mimi si Mtaalamu wa Lugha , ila kwa ufahamu wangu siyo maneno yote yana mabadiliko katika wingi Mfano hayo Hoteli, Hospitali Shule , Meza ,Pesa,Baiskeli, Nadharia,Salamu ,Habari ,Maji, Hewa,n.k Watu tunaweka viambishi awali au tamati kimakosa .

Hilo neno majizi limetumika kama kivumishi cha sifa yaani kuelezea kama mwizi aliyekubuhu , kwa mtazamo wangu naona si fasaha.Labda wataalamu wa kiswahili watafafanua .

Lakini kama kanuni za lugh yetu zinaruhusu kujenga neno kwa staili hiyo, na hatuna neno sahihi la kuwakilisha sifa zilizopitiliza kwa ubaya ,halafu watu wanharamisha hayo maneno ni wazi wanaua nguvu ya lugha.Lugha yenye maneno mafupu yanayobeba maelezo mapana ndio lugha nzuri.
 
Mimi si Mtaalamu wa Lugha , ila kwa ufahamu wangu siyo maneno yote yana mabadiliko katika wingi Mfano hayo Hoteli, Hospitali Shule , Meza ,Pesa,Baiskeli, Nadharia,Salamu ,Habari ,Maji, Hewa,n.k Watu tunaweka viambishi awali au tamati kimakosa .

Hilo neno majizi limetumika kama kivumishi cha sifa yaani kuelezea kama mwizi aliyekubuhu , kwa mtazamo wangu naona si fasaha.Labda wataalamu wa kiswahili watafafanua .

Hiyo ya kuweka viambishi kimakosa ni matokeo ya kutokukijua Kiswahili sanifu! Na kibaya zaidi watu wanahalalisha sana uharibifu wa usanifu wake.
 
companero na wengine naona mpofiti, msijekuwa mmewazidi watuw a tuki,kwani kutakuwa nauwezekano tukawa na versions kibao.
 
Back
Top Bottom