Tanzania na Utani wa Makabila: Ulishawahi kutaniwa vibaya na mtu wa kabila tofauti ukaumia nafsi yako?

Napenda sana utani wa kikabila....kama ulivyomalizia kuwa ukiwa ugenini ukapata mtani wako haswaa anayejua kutania,hautakuwa mpweke.

Kuna utani wa kabila na kabila,kuna utani wa babu na wajukuu,mjomba na wapwa, na utani wa koo na koo....na kwa kabila letu msiba au harusi hainogi bila kuwepo watani,ndio wachimba kaburi, wapika chakula na kupokea wageni na ndio wasema ukweli..japo katika hali ya utani
 
Imenigusa sana
 
Siku ya msiba wa mjomba wangu, wakaja watani yaani ndo tumetoka kuzika mtu ananivuta mtandio huku anacheka

Nilijikita nimemng'ata ule mkono hadi akatoka ngozi.

Utani wa msiba watu waache kwa kweli.
 
Mimi mndali was songwe Sasa wanyia wa huku wanasemaga wewe changamka unafanya Kama mndali au wacha ushamba Kama mndali bwana na chukiaga sana

Sent from my TECNO B1f using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…