Tanzania ni kisiwa cha amani au makao ya waoga?

Tanzania ni kisiwa cha amani au makao ya waoga?

Hujasikia madudu yanayoibuliwa na Waziri Slaa na RC Makonda kwenye masuala ya ardhi? Wamedhulumiwa mpaka wasomi na watu waliowahi kuwa viongozi, maadam tu madhulumati yana hela! Nchi ya amani inaweza kuwa na "upumbavu" kama huo, kiasi cha hukumu ya mahakama kutokuheshimiwa?

Nchi ya amani inazuia watu kutoa maoni yao? Nini kilimpata Ndugai alipolalamika deni la Taifa kuongezeka?

Nchi ya amani inatumia vibaya fedha za wananchi kwa chaguzi zisizo na umuhimu? Kumbuka jinsi wabunge wa upinzani "walafi" walivyorubuniwa kuvihama vyama vyao na kupelekea chaguzi zisizo na tija
Kifupi mwananchi akiwa na uhakika wa kula na kulala ni kazi sana kumwambia aingie barabarani kuandamana kwa Sababu yeyote iwe ya heri au shari Hana mipango hizo porojo bakini nazo wanasiasa ndio maana hawajitokezi.
 
Kifupi mwananchi akiwa na uhakika wa kula na kulala ni kazi sana kamwambia aingie barabarani kuandamana kwa Sababu yeyote iwe ya heri au shari Hana mipango hizo porojo bakini nazo wanasiasa ndio maana hawajitokezi.
Walibya walikuwa na njaa gani hata kuamua kumfurusha Kanali Ghadafi?
1. Akiwapa nyumba bure!
2. Aliwahakikishia ajira, na wale wasiokuwa na ajira akiwapa posho ya kujikimu.

Hivi utailinganisha shibe ya Walibya kabla ya kumpindua Ghadafi na shibe ya Watanzania wa sasa?
 
Walibya walikuwa na njaa gani hata kuamua kumfurusha Kanali Ghadafi?
1. Akiwapa nyumba bure!
2. Aliwahakikishia ajira, na wale wasiokuwa na ajira akiwapa posho ya kujikimu.

Hivi utailinganisha shibe ya Walibya kabla ya kumpindua Ghadafi na shibe ya Watanzania wa sasa?
Hujui kitu Diaspora ukoo wa mfalme wa Libya aliyepinduliwa na Gaddafi ndio walimpindua Ghadaffi wakisaidiwa na nchi kule walikuwa wakiishi ikiwemo Marekani

Wa ndani ya Libya hawakuwa na Shida na Ghadafi walimuona mtu poa tu
 
Mijini na vijijini manung'uniko yametawala!

Watumishi wa umma wanaonekana wana furaha lakini mioyoni wanaugulia maumivu!

Hata tabasamu za wengine zinaweza zikawa na tafsiri tofauti. Labda ni kilio kilichopunguzwa makali!

Watu wanalia lakini hawataki ijulikane kuwa wana majonzi!

Ndivyo kisiwa cha amani kunavyopaswa kuwa?

Mbona kama Kenya ambayo si Kisiwa cha amani wanafaidi zaidi keki ya Taifa lao kuzidi wananchi wa Kisiwa cha amani?

Ni kisiwa cha amani au makao ya waoga?
yaani ukiwa na akili ndogo shida sana sasa kenya wanafaidi nini maandamano kila siku wangekuwa wanafaidi wasinge andamana tanzania ndiyo tunafaidi nchi yetu ndiyo maana unaona imetulia hakuna shida na bughuza zozote
 
yaani ukiwa na akili ndogo shida sana sasa kenya wanafaidi nini maandamano kila siku wangekuwa wanafaidi wasinge andamana tanzania ndiyo tunafaidi nchi yetu ndiyo maana unaona imetulia hakuna shida na bughuza zozote
Sahihi
 
Mijini na vijijini manung'uniko yametawala!

Watumishi wa umma wanaonekana wana furaha lakini mioyoni wanaugulia maumivu!

Hata tabasamu za wengine zinaweza zikawa na tafsiri tofauti. Labda ni kilio kilichopunguzwa makali!

Watu wanalia lakini hawataki ijulikane kuwa wana majonzi!

Ndivyo kisiwa cha amani kunavyopaswa kuwa?

Mbona kama Kenya ambayo si Kisiwa cha amani wanafaidi zaidi keki ya Taifa lao kuzidi wananchi wa Kisiwa cha amani?

Ni kisiwa cha amani au makao ya waoga?
Makao ya waoga
 
Pambio hilo la sie kuwa kisiwa cha amani linakolezwa hasa na walowezi na vibaraka wao kwa vile wanamendea na kumezea mate visima vya amana vilivyojaa Tanzania.
Alipokuwa akihojiwa na BBC, mmoja wa wawekezaji waliotaka kuja kuwekeza Tanzania lakini akawekewa breki dakika za mwisho na utawala wa Mkapa, alipoulizwa juu ya fursa zilizopo Tanzania, aliesema kuwa Tanzania ndiyo nchi pekee unayoweza kwenda ukiwa masikini lakini ukarejea ukiwa tajiri!
 
Mijini na vijijini manung'uniko yametawala!

Watumishi wa umma wanaonekana wana furaha lakini mioyoni wanaugulia maumivu!

Hata tabasamu za wengine zinaweza zikawa na tafsiri tofauti. Labda ni kilio kilichopunguzwa makali!

Watu wanalia lakini hawataki ijulikane kuwa wana majonzi!

Ndivyo kisiwa cha amani kunavyopaswa kuwa?

Mbona kama Kenya ambayo si Kisiwa cha amani wanafaidi zaidi keki ya Taifa lao kuzidi wananchi wa Kisiwa cha amani?

Ni kisiwa cha amani au makao ya waoga?
Ni makao ya waoga hakuna amani.
 
Hakuna amani, ni vile tu Ubinafsi. Ukionewa Juma, kwasababu sio mshkaji wangu au hatuswali pamoja naona poa tu. Washkaji kibao wanapitishwa kwenye misoto na hawa viongozi wetu takataka.
 
Back
Top Bottom