Soma taratibu hapo chini...joka kuu naomba utzame facts zako upya
kighoma malima alichukua fomu za uraisi pia.....
hata kama hakufika mbali.but alichukua fomu
MwanaFalsafa1,
..kwa kumbukumbu zangu walijitokeza wana CCM kama 15 hivi kutaka ridhaa ya chama chao. Ninaowakumbuka ni kama Balozi.Frederick Rutakyamirwa, Njelu Kasaka,Mark Bomani, Joseph Warioba,Pius Msekwa, Horace Kolimba, Benjamin Mkapa,Horace Kolimba,John Malecela, Cleopa Msuya,Jakaya Kikwete, Edward Lowassa,....
The Boss,
..Kighoma Malima stood no chance ya kupewa nafasi na CCM.
..Mabalozi walikuwa wanashinikiza afukuzwe kazi baada ya kuonekana serikali haikusanyi kodi.
Ina maana mkuu JK was not "In it to win it"? Yani alijiunga na kampeni kwa nia ya kumsindikiza Lowassa? Au ilikua kama 2005 walipo ahidiana mmoja atakua raisi na mwingine prime minister.Edward Lowassa na Jakaya Kikwete walikodisha ndege pamoja kwenda Dodoma kuchukua fomu. waliporudi DSM kulikuwa na msisimko mkubwa kutokana na umaarufu aliokuwa nao Lowassa wakati huo. Kikwete yeye alikuwa anasema yuko pale kama kumuunga mkono kijana mwenzake.
wewe unachanganya watu humu
walikuwepo na wangeweza kugombea ni sawa na kugombea???????/
swali hapa ni waislamu wangapi walichukua fomu za kugombea urais mwaka 1995????/
jibu ni kikwete na malima tu
usilete habari za salim na wazanzibari,wakati mtu hakuchukua fomu
na alijibu ana kazi nyingi,na wewe article umeileta hapa,********???????
Mwinyi alimtaka Kikwete baada ya kuona Malecela hakubaliki.Asante mkuu. Na je Mwinyi yeye alikua na mtu wake?
Nina kubaliana na The Boss uzushi dhidi ya Salim ulikuwa 2005mkandara unachanganya madawa hapa
sali alizushiwa hayo mambo kwa uchaguzi wa 2005
muanzisha mada anazungumzia uchaguzi wa 1995
na uchaguzi huo salim hakuwepo kabisa katika wagombea,alisema bado ana majukumu oau
ni kweli mwalimu alimtaka achukue fomu,but hakuchukua
MwanaFalsafa1,
..let my try my two cents.
..Prof.Malima alikuwa hayuko on the picture. Huyu alikuwa na matatizo makubwa na wafadhili walishashinikiza aondolewe kazini. Aliundiwa tume ya uchunguzi ilyoongozwa na Mohamed Aboud, ambaye alikuwa CAG.
..Salim Salim alikuwa awe mrithi wa Mwalimu tangu mwaka 1985 baada ya kuchukua nafasi ya Edward Sokoine[r.i.p]. Mchezo ulikuwa wawekwe Salim Salim na Mzee Mwinyi ambaye alikuwa ni Raisi wa Zanzibar kuanzia 83/84 baada ya Jumbe kutimuliwa. Inasemekana Seif na Salim walimshawishi Mzee Mwinyi amuachie nafasi hiyo Salim Salim kwa kisingizio kwamba yeye ndiyo kwanza ameshika madaraka makubwa Zanzibar. Mzee Mwinyi aliwageuka wenzake baada ya majina yao kufikishwa mbele ya Kamati Kuu ya CCM. Hiki ni kisa ambacho nadhani kipo ktk kitabu cha maisha ya Seif Sharrif Hamad.
..mwaka 1995 inasemekana Nyerere alimtaka tena Dr.Salim lakini this time akamkatilia kwasababu ilidhani itakuwa vigumu kwa Wazanzibar kushika nafasi ya Raisi wa Muungano kwa vipindi viwili. nadhani baada ya hapo ndiyo Nyerere akaona atupe karata yake kwa Mkapa.
..kwa kumbukumbu zangu walijitokeza wana CCM kama 15 hivi kutaka ridhaa ya chama chao. Ninaowakumbuka ni kama Balozi.Frederick Rutakyamirwa, Njelu Kasaka,Mark Bomani, Joseph Warioba,Pius Msekwa, Horace Kolimba, Benjamin Mkapa,Horace Kolimba,John Malecela, Cleopa Msuya,Jakaya Kikwete, Edward Lowassa,....
..nakumbuka Mkapa alichukua fomu ktk mazingira ambayo ilionekana kama hayuko serious na hana nguvu zozote zile. aliwaita waandishi wa habari ofisini kwake wizara ya sayansi na teknolojia na kwa kweli hata habari zilizoandikwa zilikuwa zinaonyesha kwamba hatafika mbali.
..Cleopa Msuya alichukua fomu nadhani wiki ya mwisho na hakukuwa na taarifa zozote zile. nadhani he did it on a weekend akiwa amekatisha ziara zake za kikazi.
..Edward Lowassa na Jakaya Kikwete walikodisha ndege pamoja kwenda Dodoma kuchukua fomu. waliporudi DSM kulikuwa na msisimko mkubwa kutokana na umaarufu aliokuwa nao Lowassa wakati huo. Kikwete yeye alikuwa anasema yuko pale kama kumuunga mkono kijana mwenzake.
..there are different versions of what transpired in the Kamati Kuu ikiwemo fununu kwamba Nyerere alitishia kurudisha kadi ikiwa Malecela asingeondoa jina lake, na pia kumpiga nyundo Lowassa kwamba alikuwa na utajiri usioeleweka. Nadhani in the end majina matatu ndiyo yalikwenda Halmashauri Kuu kupigiwa kura kupelekwa Mkutano Mkuu.
..kwa kumbukumbu zangu, ktk kura za Halmashauri Kuu, Cleopa Msuya alikuwa mshindi, which was a surprise, akifuatiwa na Jakaya Kikwete which was even a bigger surprise. Benjamin Mkapa alishika nafasi ya tatu. baada ya hapo kukawa na kipindi cha mpito kuelekea wa CCM na ikaonekana Kikwete alikuwa amekosewa. Kuanzia hapo nguvu za Cleopa Msuya zikaanza kufifia.
..katika kipindi cha kuelekea mkutano mkuu upinzani mkubwa, haswa magazetini, ulionekana kuwa kati ya JK na Msuya. magazeti mengi yalielekea kumkubali zaidi JK haswa kutokana na haiba yake ya ujana na kuwa askari mstaafu. Cleopa Msuya alionekana kupingwa zaidi kutokana na kashfa ya kusema "kila mtu atabeba msalaba wake." Msuya pia did not help himself kwasababu alikuwa anahimiza ukusanyaji kodi kipindi hicho akiwa Waziri Mkuu na kuna kipindi alifika Tabora na akalalamika kuhusu wananchi kutokuwa na moyo wa kulipa kodi ambayo yeye alikuwa anaona ni kidogo!! magazeti yalimshambulia sana kwa kauli yake hiyo. Msuya pia alikuwa anaonekana ndiye aliyeshinikiza Augustino Mrema atimuliwe kazi na Raisi Mwinyi.
..kampeni ya Mkapa ilionekana kuibuka kuziba vacuum iliyoachwa na kudorora kwa kampeni ya Msuya. Mkapa alionekana kuungwa mkono na kundi la wana CCM waadilifu waliokuwa wakipiga vita rushwa iliyokuwa imeshamiri wakati wa utawala wa Mzee Mwinyi. Mkapa alikuwa anapigiwa kampeni kama mtu msafi mwenye nia na uwezo wa kupambana na rushwa.
..sikubahatika kusikia hotuba za wagombea Uraisi wakati wakiomba kura za wajumbe wa mkutano mkuu. nilisikiliza nasaha za Mzee Mwinyi na Mwalimu Nyerere kwa wajumbe wa mkutano mkuu kabla kura hazijapigwa. Mzee Mwinyi alitoa nasaha kwamba wajumbe wafuate kile ambacho wananchi wanataka kwa kumpigia kura mgombea aliyekuwa anasemwa vizuri na wananchi. kwa hotuba ile ilionekana kwamba Mzee Mwinyi alikuwa akimtaka Jakaya Kikwete. Ilipofika zamu ya Mwalimu yeye aliwaasa wajumbe wampigie kura mgombea anayeweza kupiga vita rushwa, ukabila, na udini. Wengi walitafsiri kwamba alikuwa akimtaka Benjamin Mkapa.
..raundi ya kwanza ya kura mshindi alikuwa Jakaya Kikwete, akifuatiwa na Ben Mkapa, na Msuya akashika mkia. Kura ziliporudiwa ilionekana kama kura zote za Msuya zimehamia kwa Mkapa na hivyo akatangazwa mshindi. There is an interesting sub plot baada ya Mkapa kutangazwa mshindi. Inasemekana kuna kundi la mashabiki wa Kikwete waliokuwa wakizomea ushindi wa Mkapa. Mwalimu alionyesha kufurahishwa mno na ushindi wa Mkapa. I dont remember his exact words. Cleopa Msuya alipopewa nafasi ya kutoa concession speech aliwaasa wana CCM waache siasa za "kuchimbana."
The Boss,
Sidhani Mwalimu Nyerere aliangalia ugombeaji wa kiti cha rais katika misingi ya kidini kama unavyotaka kutuaminisha. CCM ingeweza kusimamisha Waislamu wote na kwa Mwalimu lisingekuwa tatizo. Kadhalika CCM ingeweza kusimamisha Wakristo na wapagani wote na hilo kwa Mwalimu lisingekuwa tatizo. Sidhani alikuwa na mtazamo wa kuangalia kuna Waislamu wangapi wanaogombea na kuna Wakristo wangapi. Hii inadhihirishwa na kauli zake mwenyewe, kama alivyotaja Mkandara somewhere in this thread.
Hapo nimekupata, mkuu.jasusi naona hatukuelewana
ninachoongea mimi ndio hiko hiko unachozungumza wewe
but kuna vitu vingine ni maoni yangu na sio facts kutoka kwa nyerere
mwaka 1995 facts ni kuwa kabla ya kikwete kuchukua fomu,
muislam aliechukua fomu alikuwa kighoma malima peke yake
so hawakutaka chama kionekane kinawabagua waislam
unaweza kupinga udini kwa maamuzi ambayo mwingine anaweza ona ndo udini wenyewe
sisemi nyerere alimwambia kikwete achukue fomu kwa kuwa ni muislam...
Hii ya ndege Kikwete na Lowassa walitumia kama njia ya kujingea jina lakini it turned out to be disaster kwa Lowassa.Magazeti ya kaanza kuuliza pesa wamepata wapi,kumbuka 1995 kupanda ndege ya kukodisha ilikuwa ni jambo kubwa.utetezi wa Lowassa ulikuwa ni wamefadhiliwa, ikawa ni last nail to his coffin kwamba wafadhili ndio wanakupeleka ikulu ukifika huko watakuja kudai fadhila zao.MwanaFalsafa1,
..let my try my two cents.
..Prof.Malima alikuwa hayuko on the picture. Huyu alikuwa na matatizo makubwa na wafadhili walishashinikiza aondolewe kazini. Aliundiwa tume ya uchunguzi ilyoongozwa na Mohamed Aboud, ambaye alikuwa CAG.
..Salim Salim alikuwa awe mrithi wa Mwalimu tangu mwaka 1985 baada ya kuchukua nafasi ya Edward Sokoine[r.i.p]. Mchezo ulikuwa wawekwe Salim Salim na Mzee Mwinyi ambaye alikuwa ni Raisi wa Zanzibar kuanzia 83/84 baada ya Jumbe kutimuliwa. Inasemekana Seif na Salim walimshawishi Mzee Mwinyi amuachie nafasi hiyo Salim Salim kwa kisingizio kwamba yeye ndiyo kwanza ameshika madaraka makubwa Zanzibar. Mzee Mwinyi aliwageuka wenzake baada ya majina yao kufikishwa mbele ya Kamati Kuu ya CCM. Hiki ni kisa ambacho nadhani kipo ktk kitabu cha maisha ya Seif Sharrif Hamad.
..mwaka 1995 inasemekana Nyerere alimtaka tena Dr.Salim lakini this time akamkatilia kwasababu ilidhani itakuwa vigumu kwa Wazanzibar kushika nafasi ya Raisi wa Muungano kwa vipindi viwili. nadhani baada ya hapo ndiyo Nyerere akaona atupe karata yake kwa Mkapa.
..kwa kumbukumbu zangu walijitokeza wana CCM kama 15 hivi kutaka ridhaa ya chama chao. Ninaowakumbuka ni kama Balozi.Frederick Rutakyamirwa, Njelu Kasaka,Mark Bomani, Joseph Warioba,Pius Msekwa, Horace Kolimba, Benjamin Mkapa,Horace Kolimba,John Malecela, Cleopa Msuya,Jakaya Kikwete, Edward Lowassa,....
..nakumbuka Mkapa alichukua fomu ktk mazingira ambayo ilionekana kama hayuko serious na hana nguvu zozote zile. aliwaita waandishi wa habari ofisini kwake wizara ya sayansi na teknolojia na kwa kweli hata habari zilizoandikwa zilikuwa zinaonyesha kwamba hatafika mbali.
..Cleopa Msuya alichukua fomu nadhani wiki ya mwisho na hakukuwa na taarifa zozote zile. nadhani he did it on a weekend akiwa amekatisha ziara zake za kikazi.
..Edward Lowassa na Jakaya Kikwete walikodisha ndege pamoja kwenda Dodoma kuchukua fomu. waliporudi DSM kulikuwa na msisimko mkubwa kutokana na umaarufu aliokuwa nao Lowassa wakati huo. Kikwete yeye alikuwa anasema yuko pale kama kumuunga mkono kijana mwenzake.
..there are different versions of what transpired in the Kamati Kuu ikiwemo fununu kwamba Nyerere alitishia kurudisha kadi ikiwa Malecela asingeondoa jina lake, na pia kumpiga nyundo Lowassa kwamba alikuwa na utajiri usioeleweka. Nadhani in the end majina matatu ndiyo yalikwenda Halmashauri Kuu kupigiwa kura kupelekwa Mkutano Mkuu.
..kwa kumbukumbu zangu, ktk kura za Halmashauri Kuu, Cleopa Msuya alikuwa mshindi, which was a surprise, akifuatiwa na Jakaya Kikwete which was even a bigger surprise. Benjamin Mkapa alishika nafasi ya tatu. baada ya hapo kukawa na kipindi cha mpito kuelekea wa CCM na ikaonekana Kikwete alikuwa amekosewa. Kuanzia hapo nguvu za Cleopa Msuya zikaanza kufifia.
..katika kipindi cha kuelekea mkutano mkuu upinzani mkubwa, haswa magazetini, ulionekana kuwa kati ya JK na Msuya. magazeti mengi yalielekea kumkubali zaidi JK haswa kutokana na haiba yake ya ujana na kuwa askari mstaafu. Cleopa Msuya alionekana kupingwa zaidi kutokana na kashfa ya kusema "kila mtu atabeba msalaba wake." Msuya pia did not help himself kwasababu alikuwa anahimiza ukusanyaji kodi kipindi hicho akiwa Waziri Mkuu na kuna kipindi alifika Tabora na akalalamika kuhusu wananchi kutokuwa na moyo wa kulipa kodi ambayo yeye alikuwa anaona ni kidogo!! magazeti yalimshambulia sana kwa kauli yake hiyo. Msuya pia alikuwa anaonekana ndiye aliyeshinikiza Augustino Mrema atimuliwe kazi na Raisi Mwinyi.
..kampeni ya Mkapa ilionekana kuibuka kuziba vacuum iliyoachwa na kudorora kwa kampeni ya Msuya. Mkapa alionekana kuungwa mkono na kundi la wana CCM waadilifu waliokuwa wakipiga vita rushwa iliyokuwa imeshamiri wakati wa utawala wa Mzee Mwinyi. Mkapa alikuwa anapigiwa kampeni kama mtu msafi mwenye nia na uwezo wa kupambana na rushwa.
..sikubahatika kusikia hotuba za wagombea Uraisi wakati wakiomba kura za wajumbe wa mkutano mkuu. nilisikiliza nasaha za Mzee Mwinyi na Mwalimu Nyerere kwa wajumbe wa mkutano mkuu kabla kura hazijapigwa. Mzee Mwinyi alitoa nasaha kwamba wajumbe wafuate kile ambacho wananchi wanataka kwa kumpigia kura mgombea aliyekuwa anasemwa vizuri na wananchi. kwa hotuba ile ilionekana kwamba Mzee Mwinyi alikuwa akimtaka Jakaya Kikwete. Ilipofika zamu ya Mwalimu yeye aliwaasa wajumbe wampigie kura mgombea anayeweza kupiga vita rushwa, ukabila, na udini. Wengi walitafsiri kwamba alikuwa akimtaka Benjamin Mkapa.
..raundi ya kwanza ya kura mshindi alikuwa Jakaya Kikwete, akifuatiwa na Ben Mkapa, na Msuya akashika mkia. Kura ziliporudiwa ilionekana kama kura zote za Msuya zimehamia kwa Mkapa na hivyo akatangazwa mshindi. There is an interesting sub plot baada ya Mkapa kutangazwa mshindi. Inasemekana kuna kundi la mashabiki wa Kikwete waliokuwa wakizomea ushindi wa Mkapa. Mwalimu alionyesha kufurahishwa mno na ushindi wa Mkapa. I dont remember his exact words. Cleopa Msuya alipopewa nafasi ya kutoa concession speech aliwaasa wana CCM waache siasa za "kuchimbana."
umenikumbusha mbali sana historia ya huyu Bwana ktk nchi hiiDogo kulikuwa na mtu alikuwa anaitwa Tuntemeke sanga huyu aliishia kwenye 5bora lakn huyu alikuwa na uwezo mkubwa kwani alikuwa anafanya maamuzi mazuri hata akiwa bungeni, lakini alikuwa haivi na nyerere hivyo akatoswa.
Kumbe kuna watu walishayaona haya yanayotiokea sasa hivi tangu zamani na kuonya!... Cleopa Msuya alipopewa nafasi ya kutoa concession speech aliwaasa wana CCM waache siasa za "kuchimbana."
Kumbe kuna watu walishayaona haya yanayotiokea sasa hivi tangu zamani na kuonya!
Kilichojitokeza ni kwamba wale wafuasi wa Msuya walimwunga mkono Che Nkapa na wale Wazenj walikuwa wamepewa maelekezo na Komandoo Salimin (alikuwa bado anakipindi kimoja cha kukaa madarakani) kwamba wasithubutu kumchagua "Play Boy - Kikwete". Kwa hiyo hata Komandoo hakutaka kuwa chini ya Kikwete
Je unaweza kuniambia alikua anafanya nini kabla ya kugombea uraisi? Yania alishawahi kushika nyadhifa zipi. Na baada ya kushindwa uraisi akaishia wapi?
Nakumbuka baadhi ya mambo licha ya kwamba nilikuwa bwana mdogo.Gari ya Mrema nilisukuma.Wengi tuliamini angeingia ikulu kama si mwalimu.Mwalimu angemchagua JK maybe ingekuwa bora zaidi kwasababu angekuwa chini ya uangalizi wake.Mkapa ni mnafiki mkubwa,mwalimu alifanya kosa hapo.Kama alikjuwa kin EL wanamipesa,basi angemshurutisha Mkapa awawajibishe.Ama angetilia msisitizo kuwa wawajibishwe na si kuwanyima nafasi za kisiasa.Sasa alipotutoka tunaona tatizo bado lipo,na this time mafisadi ndo wenye nguvu because mwalimu was an one army man.
Ntarudi.