Tanzania Premier League, KMC Vs Yanga Uwanja wa Taifa

Tanzania Premier League, KMC Vs Yanga Uwanja wa Taifa

Nimecheka huo wimbo aisee, ama kweli ushindi unalewesha...katimu kenye hako ka KMC kampya halafu kanawatoa jasho, tuombe uzima tu kutoka kwa Maulana maana baadae huko mtakuja na kilio hapa ooh Simba sijui wanapitisha miamala Yanga ipoteze mechi sijui nini, yaani keleeele moja kwa moja, yetu macho
We Cheka tu Sesten. 😀😀😀

Hakika hili ndio jambo jema tuombeane uzima Insha Allah tu na haya yote yatakwisha yaani itajulikana tu pumba ipi na upi ni mchele. Teh teh.
 
KMC salama yao ilikuwa droo. Lakini nayo walichemka, ila yaonyesha umeshukuru si kitoto dk 85 holaaa

Lunyasi sembo anakuja kukupa wakati mgumu hivi punde..jiandae kisaikolojia[emoji3][emoji3][emoji3]
Hahahaaa. Ndio Mtani kushukuru lazima sababu point tatu ndio kila kitu.

Nimemtag mara nyingi namsubiria tu hapa aje maana si kwa hasira alizonazo huko aliko.

Cc. sembo.
 
KMC salama yao ilikuwa droo. Lakini nayo walichemka, ila yaonyesha umeshukuru si kitoto dk 85 holaaa

Lunyasi sembo anakuja kukupa wakati mgumu hivi punde..jiandae kisaikolojia[emoji3][emoji3][emoji3]
Hawa KMC wameniudhi sana.. Ila baada ya gemu zetu 2 kuanzia sasa.. Ya 3 tunao.. Hapo itakua mda muafaka wa kuonesha hasira zetu kwao.
 
Mmh. Mtanii. Kwani mshacheza nao?

Hahahaaa. Tayari nini maalizia sasa mtani. Au ndio Muamala. 😜😜😜😜
Tukicheza nao wakijikaza sana basi 5 halafu kwanini nyinyi yanga SIMBA ikipiga soka lake la viwango vya dunia la ushindi mnono basi mawazo yenu yanawaza miamala kwa nini msikubali tu kuwa SIMBA ni ya viwango vya dunia
 
Timu inayocheza mpira kama ipi Sesten sema tu.

Naamini hivyo pote pote Sesten. [emoji126][emoji126][emoji126][emoji126][emoji126][emoji126]

[emoji444][emoji444][emoji444]Kwani wao waweze wana nini na sisi tushindwe tuna nini [emoji444][emoji444][emoji444] naimba tu Seten.
Simba mkifanya vibaya ugenini kwa kua mna timu nzuri mnaamini na yanga ni hivyohivyo, msikariri subirini mda utasema
 
Tukicheza nao wakijikaza sana basi 5 halafu kwanini nyinyi yanga SIMBA ikipiga soka lake la viwango vya dunia la ushindi mnono basi mawazo yenu yanawaza miamala kwa nini msikubali tu kuwa SIMBA ni ya viwango vya dunia

Hahaha.. Kwa kua tunachokifanya sisi, wao hawakiwezi.. Hivyo wanahisi kuna nguvu ya ziada (muamal).
Kwa soka tunalotandaza kwa sasa, Simba SC ni ndugu mmoja na Barcelona.
 
Abdul Rwatubyaye beki katili wa timu ya Taifa ya Rwanda muda wowote anatua Jangwani...sipati picha akicheza na Cotton..inanikumbusha Stam na Rio pale Traford
Hahaha.. Nikumegee siri.. Huyo beki katika mazoezi ya timu ya Taifa ya Rwanda, alikua ni uchochoro kwa MK14. Nimeshuhudia, MK14 akimgeuza anavyotaka.

Mkuu jitahidini mumlete kabla mzunguko wa 2 wa TPL haujaanza.. Kama tatizo ni hela, pitisheni bakuli, nitakua wa kwanza kuchanga.
 
Hawa KMC wameniudhi sana.. Ila baada ya gemu zetu 2 kuanzia sasa.. Ya 3 tunao.. Hapo itakua mda muafaka wa kuonesha hasira zetu kwao.

Pole sana Mtani. Utanitag na mie ili nizione hizo hasira zenu Mtani. 😂😂😂
 
Hahaha.. Nikumegee siri.. Huyo beki katika mazoezi ya timu ya Taifa ya Rwanda, alikua ni uchochoro kwa MK14. Nimeshuhudia, MK14 akimgeuza anavyotaka.

Mkuu jitahidini mumlete kabla mzunguko wa 2 wa TPL haujaanza.. Kama tatizo ni hela, pitisheni bakuli, nitakua wa kwanza kuchanga.
Aisee jamaa wameishiwa mpaka beki chochoro wanaiona lulu hahaha wailete hiyo beki ikutane na washambuliaji wanyumbulifu simba nguvu moja
 
Back
Top Bottom