Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Patashika ya Ligi Kuu Tanzania TPL, kuelekea leo Novemba 22, 2018 kwa viwanja viwili kutimua vumbi, ambapo mkoani Shinyanga wenyeji Mwadui FC watawakaribisha Yanga SC kwenye uwanja wa Kambarage.
Kama haitoshi Azam FC vinara wa ligi kuu, watapapatuana na Ruvu Shooting kwenye dimba la Azam Complex.
Vikosi vya mchezo wa Mwadui FC na Yanga SC, kama ifuatavyo. Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 10:00 jioni.
View attachment 942699
Kuanzia sasa mpira utaanza uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga huku timu zote zikifanya ukaguzi
Naaaaaaaam mpira umeanza kunako dimba la Kambarage
00' Mwadui FC 0-0 Yanga SC
10' Goooal Goooaal Makambo anaandika bao kwa upande wa Yanga baada ya shuti lake la kushoto kwenda moja kwa moja wavuni na kumuacha golikipa akichumpa bila mafanikio
Mwadui FC 0-1 Yanga SC
20' Mwadui wametawala mchezo lakini mashambulizi yao yanashindwa kuzaa matunda.
40' Gooooooooooaaal Salim Aiyee anasawazisha bao upande wa Mwadui FC baada ya shuti la Charles Ilanfya kutemwa na golikipa Kindoki
Mwadui FC 1-1 Yanga SC
Naaaaaaaam mpira ni mapumziko
Awamu ya pili ya mchezo wa TPL inaanza uwanja wa CCM Kambarage
Mwadui FC 1-1 Yanga SC
55' Ngasaaaaaaa gooooal.. Mchezaji wa Mrisho Ngasa anaandika bao la pili baada ya kupiga shuti katikati ya ngome ya Mwadui FC
Mwadui FC 1-2 Yanga SC
Mashambulizi ni kwa pande zote, huku Mwadui FC wakitafuta bao la kusawazisha ili kubaki walau na alama moja
Wakati wowote mpira utakwisha uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga
90' Naaaaaaaam mpira umekwisha ambapo Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao mawili kwa moja dhidi ya Mwadui FC
Mabao ya Yanga yakifungwa na Makambo dakika 10 na Ngasa kunako dakika ya 55 huku bao la Mwadui FC likiwekwa wavuni na Salim Aiyee kunako dakika 40 za mchezo wa TPL
Timu ya JF tumekuletea mtanange huu
Asanteni.. Ghazwat
Kama haitoshi Azam FC vinara wa ligi kuu, watapapatuana na Ruvu Shooting kwenye dimba la Azam Complex.
Vikosi vya mchezo wa Mwadui FC na Yanga SC, kama ifuatavyo. Kumbuka mchezo ni kuanzia saa 10:00 jioni.
Kuanzia sasa mpira utaanza uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga huku timu zote zikifanya ukaguzi
Naaaaaaaam mpira umeanza kunako dimba la Kambarage
00' Mwadui FC 0-0 Yanga SC
10' Goooal Goooaal Makambo anaandika bao kwa upande wa Yanga baada ya shuti lake la kushoto kwenda moja kwa moja wavuni na kumuacha golikipa akichumpa bila mafanikio
Mwadui FC 0-1 Yanga SC
20' Mwadui wametawala mchezo lakini mashambulizi yao yanashindwa kuzaa matunda.
40' Gooooooooooaaal Salim Aiyee anasawazisha bao upande wa Mwadui FC baada ya shuti la Charles Ilanfya kutemwa na golikipa Kindoki
Mwadui FC 1-1 Yanga SC
Naaaaaaaam mpira ni mapumziko
Awamu ya pili ya mchezo wa TPL inaanza uwanja wa CCM Kambarage
Mwadui FC 1-1 Yanga SC
55' Ngasaaaaaaa gooooal.. Mchezaji wa Mrisho Ngasa anaandika bao la pili baada ya kupiga shuti katikati ya ngome ya Mwadui FC
Mwadui FC 1-2 Yanga SC
Mashambulizi ni kwa pande zote, huku Mwadui FC wakitafuta bao la kusawazisha ili kubaki walau na alama moja
Wakati wowote mpira utakwisha uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga
90' Naaaaaaaam mpira umekwisha ambapo Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao mawili kwa moja dhidi ya Mwadui FC
Mabao ya Yanga yakifungwa na Makambo dakika 10 na Ngasa kunako dakika ya 55 huku bao la Mwadui FC likiwekwa wavuni na Salim Aiyee kunako dakika 40 za mchezo wa TPL
Timu ya JF tumekuletea mtanange huu
Asanteni.. Ghazwat