Tanzania Premier League 'TPL' Simba SC Vs Ndanda FC Uwanja wa Uhuru Dar Es Salaam

Tanzania Premier League 'TPL' Simba SC Vs Ndanda FC Uwanja wa Uhuru Dar Es Salaam

Lazima tuwachape nchale hata 2 hawa Ndanda kuchele... Watusamehe sana
Nguvu ya Mamba.. Terminater.. MK14 Leo ni zamu yako.
Simba nguvu moja
MK14 ameshaweka 2 peke yake mpaka sasa.
We are The Champions
 
Mkude leo anatikisa, Zana leo sijui kala ugali wa muhogo hajakata viuno nahisi usiku Zahera anatabia ya kishenzi kumtumia wanawake wanamfyonza nguvu usiku kucha hongera zana👏👏
 
Patashika ya Ligi Kuu Tanzania 'TPL' kuendelea kupigwa leo Mei 19, 2019 kunako uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam ambapo Mabingwa watetezi Simba SC, Mnyama Mkali Mwituni, wakiwakaribisha Ndanda FC Wanakuchele kutoka Mtwara.

Ni mechi inayotarajiwa kuwa ngumu ya vuta nikuvute kwa muda wote wa dakika tisini, kwani katika mchezo wa mzunguko wa kwanza timu hizi zilitoka sare ya kutofungana.

Leo wanapambana tena Ndanda FC watawasimamisha Simba SC? Au Simba SC watapata matokeo chanya yatakayowasogeza kushikilia kombe kwa mkono mmoja? Usikose Ukaambiwa.

Kumbuka mchezo kuanzia saa 10:00 jioni na itakuwa mubashara na Azam Sports 2.


View attachment 1102213View attachment 1102214

Wakati wowote Kabumbu litaanza uwanja wa Uhuru

Naaaaam mpira umeanza uwanja wa uhuru

00' Simba SC 0-0 Ndanda FC

05' Gooooooooooooaaaal goooooaal
Maddie Kagere anahesabu bao la kwanza upande wa Simba akipokea pasi ya Bocco

Simba SC 1-0 Ndanda FC

Simba wanatawala mchezo wa kwa pasi za hapa na pale.

10' Goooooooooooooooooooaaal Maddie Kagere anahesabu bao la pili upande wa Simba

Simba SC 2-0 Ndanda FC

15' Mpira unacheza upande wa Ndanda FC pamoja na kushambuliwa langoni mwao!

Bocco anakwenda, lakini anakosea wanachukua Ndanda wanakwenda mbele kujaribu kushambulia lakini Niyonzima anaharibu mipango

20' Simba SC 2-0 Ndanda FC

Ndanda wanapata faulo..Nahodha Makasi anapaisha na kuwa goal kick

25' bado matokeo Simba wako mbele kwa goli mbili bila majibu...

Zana anaonywa na mwamuzi baada ya kumfanyia madhambi

30' Simba SC 2-0 Ndanda FC,

Wachukua Simba kwake Mo Hussein anatokea golikipa anakuokoa

Kagere anakwenda na mpira mashariki ya uwanja, Ndanda wanajaribu kuondosha hatari ile...

Haya Ndanda wanaonana sasa kujaribu kulisogelea lango mchezaji anapiga ndefu lakini unatoka nje ya lango upande wa Simba

35' Simba SC 2-0 Ndanda FC

Kigi Makasi anaonyeshwa kadi ya Njano baada ya kumchezea faulo Zana Coulibaly

Mkopi anapiga ndefu..Lakini Aishi Manula anatokea na kudaka bila wasiwasi.

Mpaka sasa mpira umepungua ile kasi ya mwanzo

40' kuelekea kuwa mapumziko ambapo Simba wanaongoza kwa bao mbili

Hassan Dilunga anapiga shuti kali kwa umbali mrefu..Lakini unatoka nje kuwa goal kick

V. Manyanga anakwenda na anapiga chenga hata hivyo anaukosea..!
Kageree fireeeeeee
Simba nguvu moja
 
Back
Top Bottom