Tanzania "Shamba la bibi" hadi lini? Hii Ruby ni yetu. Iweje iko sokoni Dubai na serikali yetu haijui? Nasaidia, mchimbaji huyu, anzieni hapa!

Tanzania "Shamba la bibi" hadi lini? Hii Ruby ni yetu. Iweje iko sokoni Dubai na serikali yetu haijui? Nasaidia, mchimbaji huyu, anzieni hapa!

Maadam wewe ni mtetezi wa CCM na watawala wake,huna haki ya kulalamikia wala kuhoji mambo haya.

Insanity is doing the same thing over and over again and expecting different results-Albert Einstein.
Huyu jamaa huwa anatetea sana serikali na Chama chake Cha CCM, leo amewageuka!
 
Winza ilikuwa 2006 nakumbuka
2007 mwanzoni hata mm nkikuwa winza

Na ruby ya winza nakumbuka kuna mzee mmoja pale alikuwa anajishugulisha na uchimbaj alikuwa anaitwa mzee mturuchie (marehem sahv)baba Ben yeye ndiyo aliigumia
Ndani kwake walimkuta nayo kama debe 2 aliambulia kupewa fuso na kirolaa
Ndipo mlio ukaitika huko watu tukajazana huko
Ila kwa baday winza mawe yalikata kabisa,sasa najiuliza hii ruby imetokatoka vp huko au iliwekwa
Maana mlio mbona watu hawakuusikia
Kingine nikiangaliaaaaa hiyo ruby mbona inafanana kama ruby ya longido,miamba yake
Maana nakumbuka ruby ya winza ilikuwa ya sensa
Inafanana kdg kama ya mahenge,marombo au mtopwesh

Ova
Mahenge Matombo udongo tofauti!
 
Dunia ina umafia mwingi saaana..

Biashara ya madini inamilikiwa na cartels fulani ambazo zina matawi kila mahala na zipo kuhakikisha maslahi ya mabwanyenye yanastawi.. Kudeal na huu umafia kunahitaji akili kubwa zaidi ya hizi akili za kina Joti na Mpoki...

DRC ni nchi kubwa sana yenye madini kila mahala lakini ukiwa pale Lubumbashi aka Katanga province utakuta raia wana njaa na umasikini japo huko polini mamafia wa dunia wanakamua watakavyo midege ikitua na kuruka
Kifupi nchi imetekwa na wahuni ndio wanaimiliki.

Tanzania iko mikononi mwa wahuni toka enzi za uhuru, madalali wa hao wahuni tuko nao tunaishi nao na wengine tunaamini kama ndugu zetu but they are here purposely, Kupitia hao madalali ndio hata uongozi wa juu na maeneo nyeti wanapatikana watu.... Kuvuka hiki kikwazo na kuukata mnyororo wa wahuni huhitaji demokrasia bali unahitaji kiburi, unyama, kutojali na ukatili mwingi, ukiwavuruga ndipo utapata nafasi ya kuset na kuokoa maslahi ya Taifa...

Watanzania kwa kupenda maisha mazuri mepesi wamegeuka maagent wa cartels na kusaidia ustawi wao pale penye ugumu, Cartels hizi zimejipenyeza Kanisani, misikitini, Kwenye vyama vya siasa na kila penye influence ili kulinda maslahi yao kila yanapoingiliwa..
 
Magufuli alijitoa sana kulinda raslimali za nchi, kulikuwa na ulinzi na utaratibu Kwa wachimbaji, wachimbaji walichimba , kulikuwa na maafisa wa madini na TRA katika sehemu mpya au za zamani ambapo wachimbaji wanafanya shughuli zao, mali ikipatikana itajulikana Kwa maafisa wote wa madini , TRA , itapimwa na mchimbaji kupewa kibali Cha kwenda kuuza Mali yake katika masoko ya ndani yaliyopo, hivyo mchimbaji ataandamana na hao maafisa wa pande mbili.

Akifika sokoni wanunuzi wengi hutaka kununua mali hiyo kulingana na soko au bei iliyopo kwenye soko la dunia Kwa siku hiyo, mnunuzi akipatikana Mali itapimwa kuji ridhisha na kuona kiwango tajwa kutoka maafisa wa madini ni sahihi? Kama ni sahihi basi ana mlipa muuzaji na muamala wa serikali ana kusanya pesa hiyo ana ilipa TRA, utaratibu ambao ulikuwa mzuri sana, uliondoa usumbufu na kutoa soko huru Kwa wachimbaji, hivyo wachimbaji wali hamasika.

Hata kama ikitokea hakuna wanunuzi kulingana na kiwango kikubwa Cha pesa, serikali iikuwa na utaratibu wa kununua, mfano ni zile kilo za tanzanite zilizopatikana Kwa yule mmasai (Laizer), hivyo wanunuzi wa nje walikuja nchini na kujisali kama wanunuzi na kupewa license ya kununua na kuuza popote duniani.

Baada ya Mama kuingia akasema hatua hizo sio sahihi , Zina kimbiza wafanya biashara, aka ruhusu wanunuzi waje kiholela wanunue popote na mahali kokote, tuna fungua nchi, ndio maana madini hyafiki tena katika masoko yaliyowekwa, wanunuzi wanaenda kule kule shimoni/porini/ machimboni na kusubili mali huko na kufanya biashara kule kule na kutorosha mali, hakuna tena TRA, maafisa madini au usalama wa taifa kule, wote wako maofsini maana agenda ni kufungua nchi, tulambe hasari.

Hii nchi binafsi nafikiri siasa Ina zipeleka pabaya, Magufuli alijitahidi sana ila baada ya kumtia moyo tukimwita majina yote mabaya, ana kimbiza wawekezaji, muuaji, hapendi mataraji, Leo tuna pigwa jiwe la bil zaidi ya 250 lakini utasikia time kimbilia world bank, EU, USAID au china kuomba misaada, ni taifa ambalo mindset zetu ni kuomba omba, kiongozi wa nchi lazima uwe extraordinary na kuachana na tabia za kufanya basic things, hatuwezi kuwa taifa Imara Kwa viongozi kufanya vitu vya kawaida ambavyo mtu yeyote anaweza fanya.
 
Wanabodi

Naendelea na zile makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa", na Leo ni kuhusu uzalendo wa kujitolea kuisaidia serikali yako na nchi yako, pale unapoona imeshindwa na inahitaji msaada, je tutaendelea kufanywa Shamba la Bibi Hadi Lini?.

Hili ni bandiko la kuisaidia serikali yetu kuhusu hii Ruby, Swali ni Tanzania tutaendelea kufanywa ni "Shamba la Bibi" hadi lini?!. Hii Burj Alhamal Ruby ni Yetu!, Iweje Iko Sokoni Dubai, lakini serikali yetu haijui chochote?!.

Uzalendo ni kuipenda nchi yako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote na kwa nafsi yako yote na kuilinda na kuitetea kwa moyo wako wote, kwa nguvu zako zote, na kwa uwezo wako wote, na ikibidi kuipigania, uwe tayari kuutoa uhai wako kuifia nchi yako!.

Uzalendo wa kweli hukaa ndani ya mtu, hauonekani kwa macho, bali hukaa moyoni, hivyo kuna watu ukiwaangalia kwa juu juu at face value kwa jinsi wanavyo onekana, wanaonekana kama ni wazalendo, lakini in reality sio wazalendo lolote wala uzalendo chochote, bali ni wapigaji, na baadhi yao ndio mafisadi wakubwa!. Wamejivisha ngozi ya kondoo ya uzalendo,Ila kwa ndani ni mbwa mwitu, fisi, Chui.

Na kuna watu ni hohe hahe, masikini wa kutupwa, wanaoishi kwenye lindi la umasikini uliotopea, lakini ndio wazalendo wa kweli wa taifa hili, Mimi ni mmoja wa wazalendo hawa.

Ukiona kuna kitu serikali yako imeshindwa na wewe unaweza kusaidia, saidia tuu usingoje uombwe.

Baada ya Tundu Lissu kushambuliwa na wasiojulikana, serikali yetu ilishindwa kuwapata, mimi ni miongoni mwa tuliijitolea kuisaidia serikali yetu kuwabaini wasiojulikana hawa,


Kwenye ulinzi wa Rasilimali zetu, kwa muda mrefu Tanzania tumekuwa na kilio cha kufanywa shamba la bibi kwa manyang'au kutuibia Rasilimali zetu as if hazina mwenyewe!.

Hivi ninavyoandika hapa, kuna jiwe la kito cha thamani aina ruby kutoka mgodi wa ruby wa Winza kule Dodoma, lenye uzito wa kilo 2.8, ambalo limechimbwa na Mchimbaji mdogo, serikali haijui, Mchimbaji huyo haijui thamani yake hivyo ameuza bei ya kutupa, serikali haijui. Mnunuzi kaliondoa nchini kinyemela serikali haijui. limeuzwa serikali haijui, mnunuzi kaliuza kwa tajiri wa Kiarabu, serikali haijui. Tajiri wa Kiarabu kalibatiza jina la Burj Alhamal Ruby, serikali haijui.

Sasa Burj Alhamal Ruby liko sokoni Dubai, likisubiria mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan uishe, lipigwe mnada, serikali haijui!.
Mbunge Mhe. Danstan Kitandula, anauliza Bungeni kumuuliza Waziri wa Madini kuhusu jiwe hili, Waziri wa Madini anashanga na yeye kusema serikali haijui Ila na wao wamesikia mitandaoni!.
Serikali sio mtu ni Taasisi, ina jicho kali linaona kila mahali, ina mkono mrefu unafika kila kona, hivyo katika hali ya kawaida, haiwekani haya yote yatokee Tanzania!, tutaendelea kufanywa Shamba la Bibi Hadi Lini?. Kwa vile sasa tunaishi kwenye ulimwengu wa "the world of information world" kila kitu ni kwenye ncha za vidole vyako, kuisaidia serikali yetu ipate PA kuanzia, hizi ni data zote za jiwe hili akiwemo mmiliki.
View attachment 2196654
Huyu jamaa Steve Ulatowski, ndie mtaalamu wa Madini ya ruby aliyepima properties za jiwe hili, akiwa na mmoja wa wachimbaji wa ruby sasa analisagia kunguni jiwe letu la Dubai ili mnada usifanyike kwasababu hilo jiwe limepigwa!.

Burj-Alhamal-1024x891.png

Buyer Beware: Closer Examination of the Burj Alhamal Ruby Casts Doubt on its $120 Million Valuation​

by Jeffery Bergman, AGA ASG, BDC-BGC SSEF
April 21, 2022
An astonishing record-breaking rough ruby of 8,400 carats, weighing 2.8 kilograms, from Winza, Tanzania has gone on display at the Waldorf Astoria Dubai International Financial Centre. According to Patrick Pilati, a director of the company that owns the ruby, SJ Gold & Diamonds of Dubai, said it is one of the largest rubies in the world and is valued at approximately $120 million. As the company’s crown jewel, they have named it ‘Burj Alhamal’.

Is the Burj Alhamal really worth $120 million? Photo attribution: The National.
However, a closer examination of the stone casts doubt on its estimated valuation. A closer look at the details reveals the stone may not be what it seems. For example, a 5.00 carat stone weighs about 1.00 gram. Therefore, a 8,400 carat stone would weigh approximately 1.68kg, not 2.8 kilograms. Second, several rough ruby-in-zoisite specimens 5 to 10 times larger have been documented. Third, rubies from Winza are not found in zoisite. The stone is likely from Longido, Tanzania. Finally – and most importantly – current valuations for ruby-in-zoisite specimens do not support the estimated $120 million valuation for the Burj Alhamal.
So, what could the Burj Alhamal really be worth? Steve Ulatowski of New Era Gems is an expert in ruby-in-zoisite specimens. He has sold a substantial amount of this material at the going rate of around US$350 per kilogram, including the approximately 3kg specimen he is holding in the photo below. “Maybe US$1200 if we were lucky…wholesale, most likely [this would sell for] $750.”
Steve Ulatowski with a miner in Tanzania. [emoji2398]Travis Lejman

New Era Gem’s table at Tucson 2022 selling ruby-in-zoisite specimens from Longido, Tanzania for $350 per kilogram.
Another example that undermines the extraordinary valuation of the Burj Alhamal is the 2 kg ruby-in-zoisite specimen named the “Gem of Tanzania.” It was initially valued at £11m (US$14.35m) and owned by UK Wrekin Construction. The company used the valuation of the stone to help prop up its balance sheet. Forced into bankruptcy, the court-appointed administrators Ernst & Young declared the 2kg stone’s £11m valuation and its accompanying documents as forgery. With 60 offers, it was eventually auctioned for a mere £8,000 (US$10,400), leaving creditors with massive losses exceeding £45m (US$58.7m).
But there’s still more evidence that points to an inflated valuation for the Burj Alhamal. A 228,000 carat (45.6kg) ruby-in-zoisite specimen offered by Bonhams in Los Angeles on 20 May 2014 carried an estimated value of US$100,000-$150,000. This enormous ruby specimen is 16 times larger than the “Burj Alhamal.” It failed to sell at the Bonhams auction. In other words, bidding did not reach the minimum estimated value of US$100,000 (or US$2,200 per kilogram).
Instead, the Bonhams stone, which the listing states was carved from a “single specimen of Tanzanian ruby rough” by a famous Idar-Oberstein carver, had a finished weight of 0.85kg and sold at auction for $13,200 or $15,500/kg. This is another great price/value comparison to the Burj Alhamal which, from its photos, is likely of similar or lesser quality. The National photo of Burj Alhamal shows that the stone may only be about 25% ruby and 75% zoisite. This means the actual ruby content is about 0.7kg – considerably less than the 0.85kg of the Bonhams carved toad.
Several other Bonhams auction records demonstrate that you can purchase ruby-in-zoisite specimens for a few hundred dollars.

New Era Gems website offers a 2.92KGS ruby-in-zoisite specimen for US$700.
The 2.8kg (or 1.68kg?) “Burj Alhamal” is only one of the gems in the SJ Gold & Diamonds Callisto collection, which includes 12 rough rubies that weigh a total of “an astonishing 236,000 carats” according to Tariq Saeed, writing for Dubai’s Periodical Today news website.
SJ Gold & Diamonds should pay closer attention to auction records when publishing any eye-popping valuation of the stones in its collection. Otherwise, experience from the likes of the Gem of Tanzania will dictate the obvious next question: “Why?”
Kwa kuwasaidia wenzangu na mimi ambao hizi lugha ni lugha za watu.

Kwa mujibu wa mtaalamu wa miamba ya madini, anasema japo hili jiwe la hii Ruby limeingizwa soko la kimataifa Kwa makaratasi ya kuonyesha limechimbwa mgodi wa Winza Dodoma, hizo karatasi ni forgery, hili jiwe limechimbwa Longido Arusha, na Mchimbaji mdogo, ambaye hajui thamani ya jiwe hilo, hivyo alishikishwa kidogo dogo cha pesa mbuzi , kwake akaziona nyingi. Jiwe likaondoka Longido.

Ili jiwe liweze kuingia masoko ya kimataifa, ni lazima lisajiliwe na kupatiwa certificate of origin, hivyo ukatafutwa mgodi wa ruby ambao uko tayari ku issue that certificate, and that where mgodi Winza huko Dodoma ulipoingia ukatoa face certification ili mzigo uingie Sokoni. Jamaa wakalipwa chao, wakaingia front kuwa jiwe ni Lao, wakaliandikia certification, na sijui kama kodi za serikali zilipwe ndio maana serikali haijui!.

Hawa mgodi wa Winza, walifanya kosa moja tuu, walipima uzito bila kupima properties na kulisajiji kuwa wamelichimba wao. Hilo jiwe lina properties za kitu kinachoitwa zoisite, ambacho kinapatikana Longido tuu!, iweje ruby ya zoisite ipatikane Dodoma?.

Ni kama jiwe la Tanzanite kinapatikana Mererani pekee, lakini muuzaji mkubwa number 1 wa Tanzanite ni India akifuatiwa na Africa Kusini, Tanzanite inapatikana Mererani pekee nchini Tanzania, hiyo Tanzanite ya India inayoongoza Duniani na Africa Kusini, inatoka wapi?.

Tanzania tunaendelea kufanywa Shamba la Bibi Hadi Lini?.
Wasalaam

Paskali​



Waziri husika ajihuzuru
 
Tulipaswa kuelezwa lilichimbwa lini na kuuzwa lini?

Yote kwa yote, CCM ni ile ile, hakuna kipya. Karibu wote ni wezi na hawana mpango wa kuacha wizi.
 
alikuwa mwizi kama wanasiasa wenzie walivyo wezi ila bado haiondoi ukweli ni mmoja wa ma Rais wachapakazi kuwahi kutokea nchini

kama huamini report ya Ukaguzi wa Mkaguzi mkuu wa Serikali alieteuliwa na yeye mwenyewe unataka nikiwekee ushahidi wa picha wakati anaiba ? gharama ya kutokujua kwako na mahaba yako kwake haihusu watu wenye akili


Julius Nyerere ndio Rais pekee ninaeweza kuamini kuwa hakuwahi kuliibia hili Taifa…waliofuata na watakaokuja watatofautiana viwango vya wizi na kuficha taarifa za wizi wao tu


Mnakaza mafuvu weeee kuwa Jamaa alikuwa Fisadi, haya wekeni hapa ushahidi ufisadi wake ulifanyika vipi [emoji848] hamna hata majibu sahihi [emoji849]

Basi tajeni hata akaunti yake 1 aliyokuwa akificha hizo fedha pia hakuna chochote.

Kawadanganyeni watoto ili muendelee kulipwa posho zenu za kuichafua legacy ya JPM [emoji2]
 
Nahisi hiyo ni kama yale marubi ya longido. Yani dude kuuuubwa ila halina thamani yoyote ya maana. Mpaka yawe tani za kutosha. Halafu madini ya vito huwa yana vigezo vyake vya kitaalam wanaita C's.

Halafu mbona jiwe ni chafu sana. Nilidhani ni safi kwelikweli na lina rangi ya kutosha. Yaani mawe machafu kama hayo yapo mengi sana moro, Longido, mahenge yanauzwa bei ya nyanya 🤣
 
Kwahiyo Kwa akili yako, limetolewa wakati wa JPM ,ila Leo hivi Sasa ndo imejulikana?.




Sent using Jamii Forums mobile app
ungekuwa mfuatiliaji mzuri wa hii sekta ungejua kuwa kuna kipindi around 2yrs back mgodi huo wa Longido ndio ulitema mawe zaidi,rekodi ya kutoka mawe karibuni Mundarara hazipo,kikawaida njia za mawe ni nadra kutoka jiwe 1 tu pekee kama hilo,ukishashika mkondo(njia) yanatoka mfululizo kwa muda fulani mpaka njia ifunge
 
Back
Top Bottom