Tanzania: Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 kufanyiwa marekebisho kuhusu umri wa kuolewa

Tanzania: Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 kufanyiwa marekebisho kuhusu umri wa kuolewa

Informer

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2006
Posts
1,606
Reaction score
6,672
Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palagamba Kabudi amesema Serikali imepanga kutekeleza uamuzi wa Mahakama ya Rufani kwa kuandaa Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971, kuhusu umri wa kuolewa.

Profesa Kabudi alisema hayo Novemba 18,2021 alipoeleza mafanikio ya wizara yake katika miaka 60 ya uhuru wa Tanzania Bara.

Muswada huo alisema umepelekwa kamati ya Bunge kwa ajili ya kuupitia lakini iliurejesha serikalini ikitaka kuendelea kwa mashauriano na wadau.

Alisema wanaendelea kuwashirikisha wadau wengine kuona namna nzuri ya kutekeleza mahitaji ya watu ya umri wa kuolewa uwe kuanzia miaka 18.

Kuhusu uwakilishi wa mawakili, Profesa Kabudi alisema mahakama zote za mwanzo zenye mahakimu wenye shahada ya sheria mawakili wanaruhusiwa katika mashauri yao.

Alisema ndani ya mwaka mmoja mahakama za mwanzo zote nchini zitakuwa na mahakimu wenye shahada ili mawakili waweze kutumika.
 
Andika vizuri!!!sema kwa sheria ya sasa Binti anaolewa akiwa na miaka mingapi!na muswada unapendekeza miaka mingapi?
 
Huo umri mkubwa sana , miaka kumi na nane, mngeweka angalau 13 au 16
 
Back
Top Bottom