Tanzania(Taifa Stars) yanyolewa bila wembe na Algeria goli 4 kwa 1

Tanzania(Taifa Stars) yanyolewa bila wembe na Algeria goli 4 kwa 1

Yani bora ingeenda ata timu ya shule ya Makongo, hivi MTU anachezaje timu ya taifa pass accuracy chini ya 70%?
 
Timu ya Taifa(Taifa Stars) imeambulia kipigo cha mabao 4 kwa 1 kutoka kwa timu ya Taifa ya Algeria katika mchezo wa kirafiki

> Goli pekee la kufutia machozi la Taifa Stars limefungwa na Simon Msuva anayekipiga katika Klabu ya Difaa El Jadid ya nchini Morocco

View attachment 722670

Kiufundi Mimi nimefurahi hata kama tumefungwa hizo goli kwani kuna Kitu kikubwa mno tumejifunza kwa Kucheza na Watu ambao wametuzidi kwa kila kitu. Tena leo tumejitahidi kwani katika ile mechi ya Kimashindano tulifugwa Wiki / Goli Saba ( 7 ) nzuri tu lakini leo tumezipunguza na kufikia hizo Nne ( 4 ) hali ambayo inaonyesha kuwa tumejitahidi na taratibu Timu yetu ikiwa inapata mechi za Kirafiki na Mataifa makubwa na yaliyotuzidi basi huko mbeleni tutakuja kuwa wazuri mno.
 
Soka ni mchezo katili sana ila ndio kawaida kufunga au kufungwa big up taifa stars
 
Yani ulivoitoa iyo hbr kama vile sio mtanzania, nadhan nyinyi wengine mnafurahia tunapopata matatizo kama taifa.
Yaan siasa zinaharibu kila kitu,kuna watu wanakera sana kwa kweli,i wish i could be someone.....
 
Golikipa nimemuelewa sana. Bado tuna safari ndefu
 
Vijana wa tanzania wamecheza mpira mzur sana hasa simon msuva na samatha sema uwanja ulikuwa unatereza alaf lefalii katunyima penat baada ya samata kuangushwa ndan ya kumi na nane

Vijana wamecheza vizur sana sema hawakuwa na bahat

Nawapongeza sana vijana wa tz mkiendelea kupiga ball kama mlilolipiga leo hakika mtafika mbali sana

Mungu awabaliki sana
Acha utani
 
kwa bao hz bd wamejitahidi tuu Algeria wanatengeneza mpira kwankufuata principles zake sisi bado soka ni sehemu ya siasa tuendeleeee tuu........
 
Hivi maxoezi walifanya lini ? Wanatuaibisha tu bora wangecheza na Somalia
 
wachezaji wa taifa stars wanahitaji mtu wa kuwapandisha morali ...morali yao ipochini sana wanakosa ile ari ya upambanaji
 
Kwetu huo ni ushindi safari ile walitunyoa saba kwa sufuri. Sio watu wazuri hao.
 
Warekebishe pass accuracy tu hilo ndilo tatizo linalotunyima ushindi mechi kama hizi, kocha kafundisha butua butua
 
Tanzania tunachojua ni majungu... Udaku/umbea roho mbaya na vitu vya kijinga sio Mpira wala vitu vya msingi...... Then hili litimu lifutiliwe mbali huko wanamaliza hela tu msiiiiiieeew
 
Tanzania tunachojua ni majungu... Udaku/umbea roho mbaya na vitu vya kijinga sio Mpira wala vitu vya msingi...... Then hili litimu lifutiliwe mbali huko wanamaliza hela tu msiiiiiieeew
Kwanini mmechezesha Yanga????[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Yani ulivoitoa iyo hbr kama vile sio mtanzania, nadhan nyinyi wengine mnafurahia tunapopata matatizo kama taifa.
Sasa mkuu unadhani tufanye nini kwani mpira ni sayansi, na sio kutegemea miujiza!! Kwa maandalizi gani mliyofanya hadi kumfunga Algeria?!! Nyie ni fitina tu mala kumfungia mtu maisha, mala vilee!! Hata congo wiki ijayo huwezi mfunga.
 
Back
Top Bottom