SoC04 Tanzania tuitakayo ni yenye wananchi na viongozi wazalendo na wenye kuipenda nchi yetu

SoC04 Tanzania tuitakayo ni yenye wananchi na viongozi wazalendo na wenye kuipenda nchi yetu

Tanzania Tuitakayo competition threads

Paspii0

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2020
Posts
346
Reaction score
522
UTANGULIZI

Nina kiu na shauku ya kuendelea kuona Tanzania yenye wananchi na viongozi ambao ni wazalendo na wenye kuipenda nchi yetu kwa dhati.

MATARAJIO YANGU

- Wananchi na viongozi wajitolee kwa ajili ya maendeleo ya nchi na wathamini maslahi ya taifa kuliko maslahi binafsi. Uzalendo ujumuishe kujivunia utamaduni, historia, na rasilimali za nchi na kuzitumia kwa manufaa ya wote.

- Viongozi watakaochaguliwa au kuteuliwa watapaswa kuwa waadilifu, waaminifu, na wenye uwezo wa kutatua changamoto zinazokabili wananchi. Watahitaji kuwa na maono na mikakati madhubuti kwa ajili ya maendeleo endelevu.

- Wenye kujituma na kuchangia kwa hali na mali katika ujenzi wa taifa. Wananchi watatakiwa kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na kiuchumi kwa ajili ya kuboresha hali ya maisha yao na ya vizazi vijavyo.

- Viongozi na wananchi wote watapaswa kuwajibika kwa matendo yao. Hii inatupasa kufuata sheria na kanuni za nchi, pamoja na kuwa tayari kutoa hesabu za utekelezaji wa majukumu yao.

- Kuwepo kwa mfumo wa haki unaotenda haki kwa wote bila ubaguzi. Viongozi watapaswa kuwa mfano wa kuigwa kwa kuzingatia maadili mema na kuhakikisha haki inapatikana kwa kila mtu.

NINI KIWAPIME WANANCHI NA VIONGOZI WETU KUHUSU UZALENDO

images.jpeg


NB: picha ya Mwalimu Nyerere kwa hisani ya mtandao

- Wananchi na viongozi wanafuata sheria na kanuni za nchi kwa uadilifu.Wanaheshimu taratibu na mamlaka zilizowekwa kwa ajili ya utawala bora na haki.

- Wananchi wanashiriki katika shughuli za kijamii na kiuchumi ambazo zinachangia maendeleo ya taifa. Viongozi wanatekeleza miradi ya maendeleo ambayo inalenga kuboresha maisha ya wananchi wote.

- Viongozi wanawajibika kwa matendo yao na wako tayari kutoa hesabu kwa wananchi.
Na Wananchi wanawajibika katika nafasi zao na wanawajibisha viongozi wao kwa kutimiza majukumu yao kwa ufanisi.

- Wananchi na viongozi wanathamini na kulinda rasilimali za taifa kama vile mazingira, maliasili, na utamaduni. Matumizi ya rasilimali yanakuwa na malengo ya kudumu na kufaidisha vizazi vya sasa na vijavyo.

- Wananchi wanashiriki kikamilifu katika uchaguzi na michakato mingine ya kidemokrasia. Viongozi wanahakikisha kuwa michakato ya kisiasa ni ya haki na wazi.

- Wananchi wanajituma na kufanya kazi kwa bidii na uaminifu katika sekta mbalimbali. Na Viongozi wanatekeleza majukumu yao kwa ufanisi na uadilifu, bila kutumia nafasi zao kujinufaisha binafsi na familia zao.

- Wananchi na viongozi wanathamini na kuheshimu utamaduni na urithi wa kitaifa. Kwa pamoja Wanashiriki na kukuza utambulisho wa kitaifa kwa njia mbalimbali, kama vile kushiriki katika sherehe za kitaifa na kueneza hadithi za kihistoria.

- Wananchi wanashiriki katika kusaidia jamii zao kwa njia mbalimbali, kama vile kutoa misaada kwa wenye uhitaji. Na Viongozi wanaratibu na kusaidia mipango ya kijamii inayolenga kuboresha hali za maisha ya watu wote.

UZALENDO WA MDOMONI NI WAKUEPUKWA HASA KWA TANZANIA TUITAKAYO

- Uzalendo wa mdomoni ni tatizo Sana Kwa sasa kwani linakwamisha maendeleo ya taifa, na kwa Tanzania tuitakayo, ni muhimu kuepuka. Uzalendo wa mdomoni unahusisha viongozi na wananchi wanaosema wanapenda nchi yao lakini vitendo vyao havioneshi hivyo.

- Viongozi wanatakiwa kuwa wawazi kuhusu mipango na matumizi ya rasilimali za umma. Wananchi wanapaswa kuwawajibisha viongozi kwa matendo yao na kudai uwazi.

Mfano:
Kuweka mikakati ya kupambana na ufisadi na uzembe katika sekta zote. Hii itasaidia kuhakikisha kwamba rasilimali za taifa zinatumika vizuri na kwa manufaa ya wote.

KUBANA MATUMIZI YA SERIKALI NA KUJIKITA ZAIDI KATIKA UJENZI WA TAIFA

- Kwa kuacha kununua magari ya kifahari na kuelekeza rasilimali hizo katika maeneo muhimu, serikali inaweza kuokoa fedha nyingi ambazo zinaweza kutumika kuboresha huduma za jamii na kukuza maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Hatua hii pia inasaidia kujenga imani kwa wananchi kwamba viongozi wao wanajali na wanawajibika kwa matumizi ya fedha za umma.

- Kupunguza kutegemea wahisani katika kuendesha nchi ni hatua muhimu kwa kuhakikisha uhuru wa kiuchumi na maendeleo endelevu. Kwa Kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani, kwa kupanua msingi wa kodi na kuhakikisha kuwa walipa kodi wote wanalipa kodi zao ipasavyo. Tunaweza kufanikisha kwa kuboresha mifumo ya kodi, kupunguza ukwepaji wa kodi, na kupanua wigo wa walipa kodi.

- Kuwajibisha viongozi wanaotumia vibaya rasilimali za umma na kuhakikisha uwazi katika matumizi ya fedha za serikali. Wananchi wanapaswa kujua jinsi fedha zao zinavyotumika na kuweza kuuliza maswali inapobidi.
Report za CAG zinatakiwa kuzingatiwa,kuanzia mapendekezo Yake ,pia kuchukua hatua zaidi Kwa mapungufu ya makusudi.

- Kuboresha usafiri wa umma kutasaidia kupunguza matumizi ya magari binafsi, hivyo kupunguza msongamano wa magari na uchafuzi wa mazingira. Pia, itapunguza gharama za usafiri kwa wananchi na viongozi, na kuhamasisha matumizi bora ya rasilimali za umma kwa ajili ya maendeleo endelevu.

- Kupunguza utitiri wa mashirika ya umma hasa yale yasiyozalisha na yanayoingiza hasara serikalini ni hatua muhimu ya kuongeza ufanisi wa matumizi ya rasilimali za umma na kuboresha huduma kwa wananchi. Hapa dawa ni kutafuta mwekezaji ayaendeshe katika mchakato wa wazi ,au kuyafutilia mbali kama baada ya kuyajenga uwezo yamekuwa unproductive.

SERIKALI IJIKITE KATIKA UTOAJI WA HUDUMA TU KWA WANANCHI

- Kuboresha sera za uchumi na biashara, inahitajika kuwa nzr na kuhamasisha mazingira ya uwekezaji ambayo yanaweza kusaidia sekta binafsi kuchangia kikamilifu katika uchumi. Ushirikiano na sekta binafsi unaweza kuwa muhimu katika kutoa huduma bora, kwa mfano kupitia ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi.

- Kwa kutojihusisha na biashara, serikali inaweza kutumia vizuri zaidi rasilimali za umma kwa ajili ya kutoa huduma bora kwa wananchi. Hii inajumuisha matumizi bora ya kodi na rasilimali nyingine za taifa.

- Mashirika kama ndege , usafiri wa Umma,Bandari yasimamiwe na mwekezaji ili kukidhi ufanisi wake , serikali ibakie kuwa mbia na mnufaika mkuu wa Kodi na mtunga sera.

KWA KUHITIMISHA

  • Naiona taswira ya Tanzania yenye nuru, ambapo upeo wa vijana umekuwa mkubwa, viongozi makini wenye weredi, na ari ya kufanikiwa imekolezwa, ni ya kuvutia na yenye matumaini makubwa.
  • Tumuenzi mama Tanzania ,huu ndio urithi pekee tuliojaliwa.

- Mawazo hayapigwi rungu Bali yanachanganuliwa ipasavyo au 😁tuyapake pake rangi kufunika kombe mwanaharamu apite.

~ mbeba maono! Alamsiki.
 
Upvote 6
Kuboresha usafiri wa umma kutasaidia kupunguza matumizi ya magari binafsi, hivyo kupunguza msongamano wa magari na uchafuzi wa mazingira. Pia, itapunguza gharama za usafiri kwa wananchi na viongozi, na kuhamasisha matumizi bora ya rasilimali za umma kwa ajili ya maendeleo endelevu.
Hii issue ya magari binafsi kuna haja ya kujenga miundombinu inayotoa fursa sawa za watu kulitumia jiji lao hata kwa baiskeli zao. Nayo ni maendeleo makubwa tu... wenzetu hadi wana barabara za baiskeli tu, utalii wa baiskeli.
Screenshot_20240515-122700_Chrome.jpg


Hapa dawa ni kutafuta mwekezaji ayaendeshe katika mchakato wa wazi ,au kuyafutilia mbali kama baada ya kuyajenga uwezo yamekuwa unproductive
Umakini unahitajika hapa, maana mashirika mengine ni ya kimkakati ya usalama wa nchi. Mfano tuulize mleta mada je tunaweza kubinafsisha NIMR, NEMC, TMDA?



Mawazo hayapigwi rungu Bali yanachanganuliwa ipasavyo au 😁tuyapake pake rangi kufunika kombe mwanaharamu api
Mi napiga kura kwenye TUYACHANGANUE.
Kwa kutojihusisha na biashara, serikali inaweza kutumia vizuri zaidi rasilimali za umma kwa ajili ya kutoa huduma bora kwa wananchi. Hii inajumuisha matumizi bora ya kodi na rasilimali nyingine za taifa.
Natamani kuwatetea wabongo ili tupate ajira lakini daaah! Basi at least hizo biashara zisibinafsishwe zooote tungekuwa na makundi mawili: za serikali na za mwekezaji binafsi itasaidia kiasi ili tuwe na machaguo. Mfano mtu akakae foleni ili alipe kiasi kidogo(serikali) au aende mojakwamoja alipe zaidi(binafsi). Achague kwa uhuru na ni salama zaidi au we unaonaje broh!
 
Hii issue ya magari binafsi kuna haja ya kujenga miundombinu inayotoa fursa sawa za watu kulitumia jiji lao hata kwa baiskeli zao. Nayo ni maendeleo makubwa tu... wenzetu hadi wana barabara za baiskeli tu, utalii wa baiskeli.
Ni kweli kaka , mazingira yanaonekana vizuri,naimagine mbezi msakuzi 😄,ipo jitihada kubwa.
 
Umakini unahitajika hapa, maana mashirika mengine ni ya kimkakati ya usalama wa nchi. Mfano tuulize mleta mada je tunaweza kubinafsisha NIMR, NEMC, TMDA?
Naunga mkono hoja yako kuhusu mashirika haya muhimu katika usalama wa nchi na jamii kwa ujumla,nling'amua umuhimu wake hususani kuonesha uzalishaji ,ndio maana nkakazia kujengewa uwezo kwamashirika yote ili yawe na tija ,na kama hakuna tija yanaweza kurudishwa Wizarani Kwa usimamizi yakinifu na Yale yasio na impact kubwa kwa usalama wa nchi yetu uwekezaji unaweza kufanyika kwa tahadhari !!..,Japo nafahamu NIMR,NEMC,TMDA yote yanajiendesha kwa faida na mafanikio makubwa ,na ni taasisi za mfano !!!
 
Naunga mkono hoja yako kuhusu mashirika haya muhimu katika usalama wa nchi na jamii kwa ujumla,nling'amua umuhimu wake hususani kuonesha uzalishaji ,ndio maana nkakazia kujengewa uwezo kwamashirika yote ili yawe na tija ,na kama hakuna tija yanaweza kurudishwa Wizarani Kwa usimamizi yakinifu na Yale yasio na impact kubwa kwa usalama wa nchi yetu uwekezaji unaweza kufanyika kwa tahadhari !!..,Japo nafahamu NIMR,NEMC,TMDA yote yanajiendesha kwa faida na mafanikio makubwa ,na ni taasisi za mfano !!!
Anhaa, basi ni habari njema
 
Natamani kuwatetea wabongo ili tupate ajira lakini daaah! Basi at least hizo biashara zisibinafsishwe zooote tungekuwa na makundi mawili: za serikali na za mwekezaji binafsi itasaidia kiasi ili tuwe na machaguo. Mfano mtu akakae foleni ili alipe kiasi kidogo(serikali) au aende mojakwamoja alipe zaidi(binafsi). Achague kwa uhuru na ni salama zaidi au we unaonaje broh!
Naam kaka ,mtazamo wangu Ni kwamba wananchi Kwanza kwenye kila suala ,katika kumhangaikia mwananchi yote yenye tija na manufaa kwake yafanyike ,Mfano shirika la Umeme Tanesco lipo chini ya Serikali kuna wakati huwa huduma haiendi Sawa , changamoto huwa n nyingi na kusababishia hasara wananchi ,Je? N vibaya kuwa na mashirika mawili au kuwa na shirika mbadala la mwekezaji ili kila mmoja achague wapi kuna manufaa kwake ajiunge huko 😫.
 
Back
Top Bottom