Tanzania tumedhalilishwa sana nchini Kenya. Isijirudie la sivyo tutalipiza kwa Uhuru Kenyatta desemba 9/2021

Nenda chuo Cha diplomasia Kurasini pengine ukajua ninaongea nini.
Nina mambo ya msingi sana yakufanya siwezi kufuatilia nivae rangi gani,Tanzania tuna watu wa ajabu sana,wananchi hawana maji,huduma za afya haziko vizuri,barabara hazipitiki,badala yakuhangaika na mambo ya msingi unahangaika na uvaie rangi gani!
 
Huyu mlalamikaji bila shaka ni masalia ya roho mbaya ya mwendazake.
 
Hilo la Amina na Suluhu nakupa mji.

Bila shaka Amina atavuna sana enzi hii ya Samia.
 
Tumesikitika au wewe ndio umesikitika?? Acha kutuweka kwenye mambo yako binafsi we TAGA
 
Masalia ya mzee mkurupukaji bado mna nguvu tu za kupambana?
 
Mtoa mada hujui sheria za usalama pindi Rais akiwa nje ya nchi.
 
Hili genge la wakurupukaji achana nalo. Linakosa cha kukosoa. Hawamini kama dikiteta kashadanja.
 
Acheni hoja hazina nguvu hizo imeshatokea hata hapa Tanzania ......hata wakati sadcc ilikuwa hivyo...
 
mda mwingine watanzania tubadilike, tuache nongwa za kjinga.

sawa kupokolewa alipokelewa na waziri wa mambo ya nje.

wakati wa kuondoka, uhuru kenyatta kamsindikiza mama hadi uwanja wa ndege.

hilo unazungumziaje ndg. mleta mada?.
nimambo yakijinga nakishamba mno
 
jipige ngumi nzito kifuani halafu tamka maneno haya: mimi ni mjinga.
 
Ndivyo ilivyo duniani kote, uliwahi kuona rais wa marekani au taifa lingine kubwa rais wake anaenda airport kupokea mgeni wake, mbona Mwendazake alikuwa haendi airport nasijawahi kuona unalalamika.
 
Hahaha kwa hili hauko sahihi...ni suala la protocol..Mama Samia alipokelewa rasmi Ikulu ambako alikagua gwaride la heshima na nyimbo za taifa kupigwa...Hilo la Jomo Kenyatta international airport achana nalo ni normal procedures kiprotocol..
 
Sidhani kama uko sahihi! Kila nchi ina itifaki yake kwenye shughuli za aina hiyo. Kenya itifaki rasmi inaanzia Ikulu na siyo airport. Ndivyo ilivyo kwa nchi nyingi ulimwenguni. UK, USA, RUSSIA na hata CHINA. Tanzania itifaki rasmi inaanzia JKIA.
 
Nongwa, yaani tuna nongwa kufaa, labda ndio moja ya sababu ya umaskini wetu baada ya uvivu, elimu, ujinga na siasa bora...
 
Kwani kwenye sherehe za uhuru hawezi kumtuma waziri wake wa mambo ya nje?,
 
Sisi "wasukuma" tuliokuwa tunakula raha saaana kuliko watu wote wakati wa mwenda zake tuache unaaa au unafiki na kujifanya tuna uchungu na kila kitu! Mama kapewa heshima kubwa sana na Uhuru Kenyatta na Mama Samia ni very intelligent pengine kuliko mwendazake kwenye masuala ya Uchumi.
Baada ya Mama na Uhuru kufungua kongamano unaona Rostam Aziz akabaki kumvua Uhuru Kenyatta nguo hadharani kuhusu "Equity" ya biashara kati ya Kenya na Tanzania.
Sisi Wasukuma tutulie tuache Mama Samia aongoze kwani ana maarifa kuliko Uhuru na Mwendazake!
 
Mi sikupenda wakati wa kupiga futari,niliona Mama kakaa na Aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya nje Kenya,Amina Mohamed,huyu ni jasusi hakutakiwa kuwa karibu na Raisi bila majasusi wetu kuwa karibu,
Nashukuru mama Mulamura waziri wetu wa mambo ya nje,alikuwepo
 
Yani wewe ndugu yangu kwenye ziara yote ya Mheshimiwa Rais ulichofanikiwa kuona na kusikia ni hicho tu? Kwa mtaji huo wakenya watazidi kuwekeza na kutajirika nchini na sisi kubaki watazamaji wasioridhika na mchezo siku zote.
 
Kwa hiyo kwenye ndege ndio mlikuwa mnajadili hili pekee, badala ya hayo ma-deal mlioingia! Kama ndio hivyo, hayo ma-deal hatujaingizwa mjini kweli?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…