Tanzania tusiwe mbali na BRICS, tutachelewa

Tanzania tusiwe mbali na BRICS, tutachelewa

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Kwa muda mrefu Tanzania tulijiweka katikati ya dunia kupitia siasa ya nje ya kutofungamana na upande wowote, sera hii imetuchelewesha sana kwakuwa hakuna anaetuamini kwa 100% badala yake tuko 50/50. Hii imesababisha kukosa fursa nyingi kutoka Magharibi na Mashariki na Asia (waisalamu).

Kenya yenyewe iko 100% magharibi tangu enzi hizo, hii iliwapatia fursa nyingi kutoka upande huo kuliko sisi. Rwanda hivyohivyo, na inaisumbua DR Congo pamoja na udogo wake.

Huu ni wakati wa kuacha kupepesa macho wakati mfumo mpya wa dunia BRICS unatengenezwa. Lazima tukae siti za mbelembele kwenye tukio hili kwakuwa kwavyovyote vile dunia sasa inaenda kuongozwa na China, India na Urusi kiuchumi, kiulinzi na kiteknolojia kwa pamoja na kuungwa mkono za Brazil na nchi za Kiarabu kama Saud Arabia, South Afrika na Iran.

Tuombe mapema kujiunga na BRICS ili tuwe miongoni mwa waanzilishi wa mfumo huu ambao hata Mwl. Nyerere kama angekuwa hai nadhani angekuwa miongoni mwa waanzilishi wake.

Magharibi wana mashariti mengi sana ya kikoloni ambayo lengo lake ni sisi kuendelea kuwa tegemezi kwao milele.
 
💯💯💯 ni muhimu tueleweke tuko wapi. Siyo hii ya ndumila kuwili
 
Ukiangia Brics kwasasa utakosa misaada ya magharibi, kumbuka 44% ya bajeti yako inategemea misaada kutoka magharibi.
 
Ukiangia Brics kwasasa utakosa misaada ya magharibi, kumbuka 44% ya bajeti yako inategemea misaada kutoka magharibi.
Sio kweli maana hata China na South Afrika wako BRICS lakini bado wanao uhusiano na Magharibi. Ukiwa na rasilimali za kutosaha Magharibi watakuwepo tu.

Historia yetu na Nafasi ya Tanzania duniani na Afrika itakuwa aibu kuwa nje ya mchakato wa kuunda BRICS
 
Kwa muda mrefu Tanzania tulijiweka katikati ya dunia kupitia siasa ya nje ya kutofungamana na upande wowote, sera hii imetuchelewesha sana kwakuwa hakuna anaetuamini kwa 100% badala yake tuko 50/50. Hii imesababisha kukosa fursa nyingi kutoka Magharibi na Mashariki na Asia (waisalamu).

Kenya yenyewe iko 100% magharibi tangu enzi hizo, hii iliwapatia fursa nyingi kutoka upande huo kuliko sisi. Rwanda hivyohivyo, na inaisumbua DR Congo pamoja na udogo wake.

Huu ni wakati wa kuacha kupepesa macho wakati mfumo mpya wa dunia BRICS unatengenezwa. Lazima tukae siti za mbelembele kwenye tukio hili kwakuwa kwavyovyote vile dunia sasa inaenda kuongozwa na China, India na Urusi kiuchumi, kiulinzi na kiteknolojia kwa pamoja na kuungwa mkono za Brazil na nchi za Kiarabu kama Saud Arabia, South Afrika na Iran.

Tuombe mapema kujiunga na BRICS ili tuwe miongoni mwa waanzilishi wa mfumo huu ambao hata Mwl. Nyerere kama angekuwa hai nadhani angekuwa miongoni mwa waanzilishi wake.

Magharibi wana mashariti mengi sana ya kikoloni ambayo lengo lake ni sisi kuendelea kuwa tegemezi kwao milele.
Naunga mkono hoja. Ila haimaanishi hatushirikiana na watu wa Magharibi.

Tanzania kwa miaka mingi ilikuwa na nguvu duniani ikishirikiana na South South, Ukanda wa kusini, Ukanda wa Afrika, UN. Ndio tuliisaidia China kupata kiti kwenye P5 na kukomboa mataifa mengi Afrika kuliko nchi yoyote.

BRICS itakuwa alternative ya IMF, World Bank, G7. Italeta usawa na maendeleo zaidi duniani.
 
Naunga mkono hoja. Ila haimaanishi hatushirikiana na watu wa Magharibi.

Tanzania kwa miaka mingi ilikuwa na nguvu duniani ikishirikiana na South South, Ukanda wa kusini, Ukanda wa Afrika, UN. Ndio tuliisaidia China kupata kiti kwenye P5 na kukomboa mataifa mengi Afrika kuliko nchi yoyote.

BRICS itakuwa alternative ya IMF, World Bank, G7. Italeta usawa na maendeleo zaidi duniani.
Italeta checks and balance kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni. Sasa hivi misaada ya Magharibi inaambatanishwa na masharti mengi sana. Mataifa mengi yanawekewa vikwazo bila sababu za mzingi. Zimbabwe iko kwenye vikwazo kwa muda mrefu sana kwa maslahi ya Uingereza. Hii sio sawa. Tanzania ingekuwa ya kwanza kuomba kujumuishwa BRICS kutoka na historia yake ya kukumbatia haki.
 
Sio kweli maana hata China na South Afrika wako BRICS lakini bado wanao uhusiano na Magharibi. Ukiwa na rasilimali za kutosaha Magharibi watakuwepo tu.

Historia yetu na Nafasi ya Tanzania duniani na Afrika itakuwa aibu kuwa nje ya mchakato wa kuunda BRICS
Utegemezi wa hizo nchi kwenye bajet zao ni kama wetu?
 
Utegemezi wa hizo nchi kwenye bajet zao ni kama wetu?
MIAKA 65 YA UTEGEMEZI WA nchi za Magharibi hatujafanikiwa kujitegemea wenyewe mpaka sasa, labda tujaribu njia mpya sasa badala ya ile ya WB, IMF, WTO, na EU. Ubaya wa njia hii ya Magharibi tunaonekana kama watawaliwa tunaostihili kutawaliwa milele. Tusiogope kupata shida kidogo lakini tupone milele.
 
Back
Top Bottom