SoC04 Tanzania Tutakayo: Bei ya nauli ya SGR izingatie hali halisi ya uchumi wa wananchi

SoC04 Tanzania Tutakayo: Bei ya nauli ya SGR izingatie hali halisi ya uchumi wa wananchi

Tanzania Tuitakayo competition threads

Goddid

New Member
Joined
Apr 25, 2024
Posts
2
Reaction score
1
Rai yangu ni kuona bei ya nauli zinazopangwa na mamlaka husika zinazingatia hali ya maisha ya wananchi ili reli hii iwafae wengi kutokana na usalama wa safari, safari kutumia muda mchache pia kutokana na kutumia nishati mbadala ya umeme badala ya mafuta sababu tumekuwa tukishuhudia kupanda kwa bei ya mafuta ambako hupelekea kupanda kwa bei za nauli za mabasi.

Tumekuwa tukishuhudia miradi ikijengwa lakini mwisho wa siku watumiaji ni wachache tofauti na kusudi haswa kutokana na gharama mfano ilitarajiwa mradi wa daraja la kigamboni ungesitisha matumizi ya vivuko hivyo kusaidia safari za mjini -kigamboni kwa haraka na usalama lakin kutokana na tozo kubwa inayotozwa kwenye daraja hili imepelekea wananchi kuendelea kutumia vivuko, serikali imeweka tozo ili kuweza kulipa mkopo uliotumika kujengea daraja.
 
Upvote 0
Rai yangu ni kuona bei ya nauli zinazopangwa na mamlaka husika zinazingatia hali ya maisha ya wananchi ili reli hii iwafae wengi kutokana na usalama wa safari, safari kutumia muda mchache pia kutokana na kutumia nishati mbadala ya umeme badala ya mafuta sababu tumekuwa tukishuhudia kupanda kwa bei ya mafuta ambako hupelekea kupanda kwa bei za nauli za mabasi.
Wafanye wafanyavyo lakini tusisikie tu mambo ya mradi unaendeshwa kwa hasara.

Na kama ulivyosema, gharama za umeme wa maji ni nafuu. Ijidhihirishe kwenye bei watakazopanga.
 
Back
Top Bottom