Tanzania Tycoons List...

Tanzania Tycoons List...

shida ni kwamba Jk na serikali yake wanajua kugawa hela kirushwa rushwa na kutaka watu wafanye biashara ambazo hazina financial plans,au not bound on management basis

It is a failure and more than a shame.
Bravo Ndesa,waambie wafanye biashara kitaaluma zaidi ya kupiga ramli kazini
 
http://nobelprize.org/nobel_prizes/peace/laureates/2006/presentation-speech.html said:


"The Norwegian Nobel Committee has decided to award the Nobel Peace Prize for 2006, divided into two equal parts, to Muhammad Yunus and Grameen Bank for their efforts to create economic and social development from below. Lasting peace can not be achieved unless large population groups find ways in which to break out of poverty. Micro-credit is one such means. Development from below also serves to advance democracy and human rights."


Kwa maoni yangu, Mchango huu wa ndesamburo una mapungufu mengi. Mafanikio makubwa yamepatikana katika kuwainua watu wa kipato cha chini kwa mikopo midogomidogo, na kwa maelezo ya Muhammad Yunus wa huko Bangladesh au hata hapa kwetu, Pride Tanzania n.k. unaonyesha marejesho ya mikopo ni kwa asilimia kubwa kushinda hata wakopaji mipapa. Labda ni kuboresha tu, mfano kutoa elimu ya biashara zao, au Kilimo, kuwatafutia masoko ya uhakika, kuwafikishia pembejeo na kadhalika, lakini dhana yenyewe ni nzuri.

Binafsi sikubaliani na haya katika mchango wa ndesamburo




Alimshangaa Rais Jakaya Kikwete kutoa mikopo maarufu kama ya mabilioni ya JK kwa ajili ya kuwasaidia Watanzania na kuonya kuwa hali hiyo ni hatari na itawalemaza wananchi.

“Tunapochukua fedha tunasambaza kwenye Saccos na kwa machinga hii nchi tunaiharibu fedha za JK hazitarudi, yeye anasema zitarudi namshangaa Tanzania yenyewe ina madeni na serikali haina tabia ya kurudisha madeni. Je, kwa mtu mmoja mmoja itarudi? Wanasema ni zawadi za uchaguzi.




Katika hilo, alisema kuna haja ya Tanzania kutafuta namna ya kuwatajirisha matajiri wachache, ili waweze kuendeleza wengine kuliko kutoa mikopo kwa kila mtu.



“Niliwaambia bungeni kama serikali imeshindwa kufufua viwanda wanipe nifufue….narudia tena serikali nipeni viwanda Moshi nifufue
 
Hata hao matajiri tunaowaona wanajulikana huko kwa wenzetu, ni wale tu walioamua kujulikana, kuna matajiri kibao marekani, wanapata hela kwa madawa ya kulevya, misheni za silaha, na nyara na wanyama au minada ya kisirisiri, makampuni feki (offshore) nk, hao hawako kwenye listi ya forbes na ni matajiri mara mia ya bill gates.
Kama kweli mnachotaka ni kitu cha kueleweka, anzeni na wasio wezi, ili tupate cha kuiga, na wezi wajulikane waone aibu na wasijione mabingwa.
 
nafikiri na yeye ni mfanya bishara mkubwa tuu. na yeye ni fisadi?
 
MBUNGE wa Moshi Vijijini. Philemon Ndesamburo (CHADEMA) ameliambia Bunge kuwa matajiri wa Tanzania ni wezi hasa kutokana na mambo ya kifisadi yalivyofumka bungeni katika siku za hivi karibuni.
 
Mkuu CottonEyeJoe, mimi nitakuwa wa kwanza kumobilize watu wamchangie huyo masikini kuliko wote Tanzania. Shida itakuwa ni kumpata na utatumia vigezo gani? Ni shida ile ile inayotupata kufahamu Tajiri kuliko wote Tanzania ni nani.

By the way, mchana leo nimekutana na Mzee Reginald Mengi mahali, tukiwa katika mazungumzo nikamweleza juu ya thread hii hapa JF akawa interested kujua. Nikamwambia umetajwa na wengine wengi lakini hatujui ni yupi kapata kihalali na yupi kifisadi . . . . LOL. Mengine kapuni.
 
..


Huyo Mbowe hizo fweza mnahesabia na zile anazodaiwa na NSSF? Na huyo kajumulo vipi kweli ana pesa ya kuingia kwenye orodha?? Naona mmemsahau Mjasiliamali Basil Pesambili Mramba hapo

Ongeza All list of Shame people kwenye list. Chenge yeye ana "Vijisent" tu, hawa wengine ndio "wanamihela" na Thamani yake ni EPA+All mikataba bomu+Rushwa toka kwa wafanyabiashara wakwepa kodi+Hali ngumu ya maisha ya watanzania
 
Hapana afadhali yeye analipa Kodi.kufanya biashara si haramu
 
“Tunapochukua fedha tunasambaza kwenye Saccos na kwa machinga hii nchi tunaiharibu fedha za JK hazitarudi, yeye anasema zitarudi namshangaa Tanzania yenyewe ina madeni na serikali haina tabia ya kurudisha madeni. Je, kwa mtu mmoja mmoja itarudi?

I dont agree with this statment, evidence shows at all levels kwamba the low income population have a lower default rate then Higher income individualds and tend to respect sheria zaidi because they know its all they can do kwenye Tanzania yetu ya "wananchi" na "wenyenchi".


Its an assumption CEJ,
inapokuwa ni fedha ya mifuko ya serikali kama hii.. default rate ni kubwa..
maana watu hawatofautishi kati ya loan na grants...
 
You mention the first name Fidahussein but forgot his last name Rashid (to avoid confusion) He is owner of Africarriers and Haidery Plaza but is NOT the owner of Zahra towers or Raha towers - pls correct the mistake
 
kuna na mtu mmoja hapa kanda ya ziwa anaitwa Christopher Gachuma huyu ni mkurugenzi wa Coca Cola (nyanza Bottling Mwanza), yupo Kitano chacha pia
 
Uchambuzi wa: https://www.jamiiforums.com/showthread.php?p=265428#post265428 (Unaweza kuongeza majina unayoyajua katika thread hii) unaonyesha kuwa listi ya Matajiri Tanzania ni hii iliyopo hapa chini.

Ingawa hakuna takwimu juu ya utajiri walionao na kiasi gani cha pesa walichonacho, swali la msingi ni: Je tunajifunza nini kutokana na jitihada zao za biashara au kupata utajiri? Je, inawezekana Watanzania wengine wakafanya jitihada na kufanikiwa kama wao?

The List

  1. Said Salim Bakhressa: AZAM - Grain milling, corporate finance, passenger sea transportation, plastic packaging, marketing, polypropylene bags, other branches of engineering field, food industry, drinking water

  2. Aziz Abood: Abood buses,factories,truck company,tv&radio,properties)
  3. Nasoro: Doll trailers, superstar buses, royal buses, major shareholder-mtibwa sugar,kagera sugar, city water, truck company, properties
  4. Mohamed Dewji: Mohamed enterprises, factories, properties
  5. Rostam Aziz: Caspian; Vodacom
  6. Reginald Mengi: The IPP Group, Financial Consulting firm (IPP Consulting), Coca-Cola (Coca-Cola Kwanza, Bonite Bottlers and Kilimanjaro Spring Water), (IPP Bodycare Ltd (IPP Media). These include The Guardian Ltd; Nipashe, Alasiri, Kasheshe, Independent Television Ltd. (ITV), East Africa Television (EATV, formerly Channel 5)), Radio ONE, Sky-FM (in a joint venture with BBC) and East Africa Radio.
  7. Michael Ngaleko: Presicion Air Ltd
  8. Fidahussein: Africarriers,properties including heidary plaza, raha towers, zahra towers etc
  9. Yusuph Manji: Quality Group; Properties, Trucks
  10. Andrew Chenge: Worth US$ 1million (over 1 billion Tanzania shillings) in an overseas offshore account
  11. Nazir Mustafa Karamagi: Tanzania International Container Terminal
  12. Edward Ngoyayi Lowassa
  13. Mohammed Aboud
  14. Tarimba Abbas
  15. Philemon Ndesamburo
  16. Alex kajumulo
  17. Freeman Mbowe

Kama hii ndio listi basi tunaweza kabisa kusema kuwa kuna unfair wealth distribution na kimtizamo hapo juu ni waarabu,wahindi na waislam tu huku kukiwa na token kama mbili tatu hivi za wachagga...Na ndio maana kweli kuna mvurugano ambao wana ccm wanadai kuwa ni wa wafanya biashara....KWA MFANO TOP FIVE YOTE NI WAARABU/WAISLAM.

Mimi naona ni wakati wa kuwasaidia watanzania wote ili wanufaike na rasilimali zao....Kwasababu kama ni kweli wachagga ndio wenye ukabila na UTAJIRI WA UFISADI...Then hao TOP FIVE YETU NI WACHAGGA AMA NI WAKRISTO?
 
Matajiri wa Tanzania wezi - Ndesamburo

na Ratifa Baranyikwa, Dodoma
Tanzania Daima~Sauti ya Watu


Alimshangaa Rais Jakaya Kikwete kutoa mikopo maarufu kama ya mabilioni ya JK kwa ajili ya kuwasaidia Watanzania na kuonya kuwa hali hiyo ni hatari na itawalemaza wananchi.

“Tunapochukua fedha tunasambaza kwenye Saccos na kwa machinga hii nchi tunaiharibu fedha za JK hazitarudi, yeye anasema zitarudi namshangaa Tanzania yenyewe ina madeni na serikali haina tabia ya kurudisha madeni. Je, kwa mtu mmoja mmoja itarudi? Wanasema ni zawadi za uchaguzi.

“Hii tabia ya kugawa fedha kama karanga inadumaza watu, inalemaza badala ya kufanya uchumi ukue unalemaa…fedha ipo tunakosa Management, ni nini tunafikia huko tunakuwa taifa la kuomba omba. Kisaikolojia ukifikiri wewe ni maskini utakufa maskini,” alisema.

Katika hilo, alisema kuna haja ya Tanzania kutafuta namna ya kuwatajirisha matajiri wachache, ili waweze kuendeleza wengine kuliko kutoa mikopo kwa kila mtu.
Aidha, alisema njia pekee ya kuondokana na utaratibu mbovu wa kutozingatia taratibu wa kibiashara ni kuwa na utaratibu wa kutumia mtaji wa kuanzia biashara.

“Unapokuwa kwenye venture capital itakudhibiti ukikopa fedha kwa ajili ya kujenga shule utajenga shule kuliko ilivyo hivi sasa, unakopa fedha kwa ajili ya kujenga shule zikija unajenga kiwanda na ndiyo kitu kinachotushinda katika kuleta maendeleo na hili jambo tukianza kila mkoa tutaendelea,” alisema.

Akizungumzia viwanda ambavyo vimekufa katika jimbo lake la Moshi, Ndesamburo alisema kama serikali imeshindwa kuendeleza viwanda katika jimbo hilo wampe, ili aweze kuvifufua na hatimaye wakazi wa Moshi waweze kufaidika.

“Niliwaambia bungeni kama serikali imeshindwa kufufua viwanda wanipe nifufue….narudia tena serikali nipeni viwanda Moshi nifufue niviendeleze nitafute wawekezaji, vurugu zitakuwa hakuna kama tunataka viwanda viendelee, serikali ifikiri upya kuwasaidia Watanzania, ” alisema.

Aidha, mbunge huyo amelalamikia njia ya reli inayopita Moshi kufungwa na kuhoji sababu ya kutoiendeleza njia hiyo.

“Njia ya reli ya Moshi imefungwa na ni sehemu kubwa ya uchumi wa nchi yetu, ingekuwa inafanya kazi Burundi wangeitumia na nchi nyingine katika kusafirisha mizigo kutoka katika Bandari ya Mombasa hivi tumepungukiwa akili au maarifa? Mi nafikiri tumepungukiwa kiitikadi,” alisema.


Well, nimesoma hizi habari za Mh. Ndesamburo kwa masikitiko makubwa sana. Mtu ambaye yupo bungeni kama mwakilishi wa wananchi anapoamua dhahiri kuonesha kwamba yupo pale kwa maslahi ya wachache na ubinafsi. Anadiriki kuitaka serikali imneemeshe yeye kwa gharama ya walalahoi? Katika hili jambo, Mh Mbunge hakuona kwamba alistahili kuangalia ni kwa jinsi gani hao wananchi watashirikishwa kuweza kutoka hapo walipo badala ya kuwaona kuwa ni mbumbumbu?

Kauli zake zinaonesha wazi kabisa yupo bungeni kwa ajili ya kutafuta kuendeleza biashara zake na wala si vinginevyo.

Ikumbukwe kwamba huyu Mh. Mbunge ni moja kati ya watu wachache ndani ya chama chake ambao ndiyo wenye kauli ya mwisho. Kwa mantiki hiyo basi ninashawishika kabisa kuwa wale mabinti wawili Lucy (mtoto wa Ndesamburo) na Grace (ambaye ni mfanyakazi wake) walipatiwa viti vile vya ubunge kutokana na shinikizo la Mh Mbunge huyu ambaye alidai alitoa fedha nyingi kwenye kampeni.

Vilevile jicho langu linazidi kufunguka na kuona kuwa hali ndani ya CHADEMA kweli si shwari na ndiyo maana kelele za Mh Wangwe kuwa CHADEMA iwe ya wanachama wote ilileta mtafaruku mkubwa kwani tayari kuna kundi linalohodhi sera ya uchache na ubinafsi ndani ya chama. Hayumkini basi, huenda hata Mh Mbowe alipewa shinikizo na 'wachache' ahakikishe kuwa anamtoa Wangwe kwenye nafasi ya makamu mwenyekiti.

Aidha ninaona kuwa vita aliyoianzisha Mh. Wangwe ilikuwa ni ya hatari mno kwani kwa nyakati tofauti 'wachache' (kundi la wazee wa chama) walimuita kwa lengo la kutaka kumnyamazisha...guess what? kama hakutaka kunyamaza?

HOFU:Kwa kauli yake ya kutaka atajirishwe kwa gharama ya wananchi na apewe viwanda, itakuwaje kama CHADEMA ndiyo imepewa dhamana ya kuongoza serikali? Hofu imenijaa
![/[/COLOR
]SIZE][/COLOR]
 
Tumeishiwa akili sio maarifa. Akili ni raslimali kubwa ambayo kama huna hata uwe mjasiriamali wa aina gani hutafanikiwa utabakia usanii ni tu na ufisadi.
 
Ipo kazi !!

Wazalendo, hakuna muungwana yeyote anayeweza kuwa na List ya Walipa Kodi Wakubwa? Inaweza ikawa ni mahali pazuri pa kuanzia hata kama kutakuwa na mapungufu.

Hata hivyo bado nita compille version 2.0 ya list hii baada ya Matajiri wengine kuongezeka katika michango yenu
 
Wakulu,

Hakuna anayeweza kutupatia orodha ya Walipa Kodi Wakubwa? Huenda ikatusaidia mahali pa kuanzia japo kunaweza kuwa na mapungufu. Sina uhakika kama orodha inaweza kupatikana kwa ajili ya Public use.
 
Kama hii ndio listi basi tunaweza kabisa kusema kuwa kuna unfair wealth distribution na kimtizamo hapo juu ni waarabu,wahindi na waislam tu huku kukiwa na token kama mbili tatu hivi za wachagga...Na ndio maana kweli kuna mvurugano ambao wana ccm wanadai kuwa ni wa wafanya biashara....KWA MFANO TOP FIVE YOTE NI WAARABU/WAISLAM.
Ukabila, udini, ...

Bora ungeuliza kama wanalipa kodi? au wadaiwa na taasisi za fedha? au labda ni pesa za EPA?
 
Ukabila, udini, ...

Bora ungeuliza kama wanalipa kodi? au wadaiwa na taasisi za fedha? au labda ni pesa za EPA?

Naona unataka nianze kukutajia watuhumiwa wa EPA na labda wakwepa kodi..Naomba tubaki kwenye issue kama mleta mada anavyoelekea kutaka...Kuwa kwanza tumention hao matajiri...Mimi nime comment kuhusu TOP FIVE A TANZANIA...Sasa kuna shida gani kusema Top Five ya Matajiri wa Tanzania ni Waarab/waislam...Wewe ulikuwa wapi kwenye mjadala kuwa wachagga ni mafisadi?
Naomba tuumeze ukweli kiuvumilivu huku tukijitahidi kutovuruga mada ama mjadala huu.
Ahsante.
 
Back
Top Bottom